“Ziara Yangu Kwenye Jumba la Ufalme”
Laura,a mwanafunzi wa chuo, alipewa mgawo wa kuhudhuria ibada za kidini na kuandika ripoti kuhusu yale ambayo angeona. Alichagua kuzuru Mashahidi wa Yehova, na kichwa cha insha yake kilikuwa, “Ziara Yangu Kwenye Jumba la Ufalme.” Ni nini ambacho Laura aliona kuwa tofauti kuhusu Mashahidi? Yafuatayo ni baadhi ya mambo mengi aliyoyataja.
Watoto: “Watoto wote walikuwa katika chumba kimoja pamoja na watu wazima. Katika makanisa yote ambayo nimehudhuria, watoto huwaacha wazazi wao nyumbani na kuhudhuria Shule ya Jumapili.”
Upatano wa kijamii: “Kwa kawaida makanisa huvutia waumini wa jamii fulani au kabila fulani. . . . Lakini Mashahidi wa Yehova walikuwa wameketi wote pamoja wala si jamii fulani-fulani.”
Roho ya ukaribishaji: “Watu wengi walikuja wakazungumza nami. . . . Wengine hata wakaniuliza kama ninajifunza Biblia na yeyote. Hata hivyo, sikuona kama wananishurutisha. Wao . . . waliniacha niamue.”
Hakuna michango: “Jambo moja lililonishangaza sana ni kwamba hakuna mtu aliyechukua michango. . . . Kwenye makanisa ambayo nimehudhuria michango hata ilichukuliwa katika madarasa ya watoto.”
Kuna takriban makutaniko 90,000 ya Mashahidi wa Yehova ulimwenguni kote. Mbona usizuru mojawapo lililo karibu nawe?
[Maelezo ya Chini]
a Jina limebadilishwa.