Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w00 4/1 uku. 23
  • “Mnaijua Biblia Sana”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mnaijua Biblia Sana”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Si Wachuuzi wa Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Naweza Kuwasaidiaje Wenye Uhitaji?
    Amkeni!—2006
  • Ninawezaje Kuwa na Uhusiano Mzuri na Mwalimu Wangu?
    Vijana Huuliza
  • Kwa Nini Tunahitaji Walimu?
    Amkeni!—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
w00 4/1 uku. 23

Wapiga-mbiu wa Ufalme Waripoti

“Mnaijua Biblia Sana”

Wakati Yesu mwenye umri wa miaka 12 alipozungumza kwa ujasiri na viongozi wa kidini huko Yerusalemu, “wote wale waliokuwa wakimsikiliza walikuwa katika mshangao wa daima juu ya uelewevu wake na majibu yake.” (Luka 2:47) Vivyo hivyo leo, vijana wengi ambao ni watumishi wa Yehova hupiga moyo konde na kuzungumza na walimu wao na wanafunzi wenzao juu ya Mungu na Biblia, na mara nyingi wao hupata matokeo kama hayo yenye kuridhisha.

Tiffany mwenye umri wa miaka 14, alikuwa kwenye darasa ambapo unabii wa Biblia wa majuma 70 ya miaka, upatikanao kwenye Danieli 9:24-27, ulizungumzwa. Mwalimu alitaja mambo machache kuhusu mistari hiyo na kuifafanua habari hiyo kijuujuu tu.

Mwanzoni, Tiffany alisita kuinua mkono. “Lakini kwa sababu fulani,” yeye asema, “nikasumbuka sana kwamba mistari hiyo haikufafanuliwa kikamili. Na kwa ghafula, nikainua mkono.” Mwalimu alishangaa kwamba nilikuwa na jambo la kusema kuhusu habari hiyo, kwa kuwa wengi wa wanafunzi walishindwa kuielewa.

Alipopewa fursa ya kuufafanua unabii huo, Tiffany alisimama na kuzungumza bila kujiandaa. Alipomaliza, wanafunzi wakanyamaza kimya. Tiffany akawa na wasiwasi kidogo. Kisha wanafunzi wakapiga makofi sana.

“Maelezo hayo yanavutia sana, Tiffany, yanavutia sana,” mwalimu akasema tena na tena. Alikiri kwamba alijua ni lazima mistari hiyo iwe na maana zaidi, lakini Tiffany ndiye aliyekuwa mtu wa kwanza kumfafanulia mistari hiyo waziwazi. Baada ya somo hilo, mwalimu alimwuliza Tiffany jinsi alivyopata ujuzi mwingi hivyo kuihusu Biblia.

“Ni kwa sababu mimi ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova,” yeye akajibu. “Iliwabidi wazazi wangu wanieleze unabii huo mara kadhaa kabla ya kuuelewa.”

Wanafunzi wenzake pia walishangazwa na ujuzi wake wa Biblia. Mwanafunzi mmoja alimwambia Tiffany: “Sasa ninajua ni kwa nini nyinyi Mashahidi wa Yehova huenda nyumba hadi nyumba; ni kwa sababu nyinyi mnaijua Biblia sana.” Wengine wakamwahidi kwamba hawatamtania tena kuhusu itikadi zake.

Tiffany alipowaeleza wazazi wake jambo hilo, walipendekeza kwamba ampelekee mwalimu wake kitabu cha Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Alipompelekea na kumwonyesha sehemu inayofafanua unabii wa Danieli, mwalimu alichukua kitabu hicho mara moja naye akamshukuru.

Ni kweli kwamba vijana Wakristo wanapozungumzia kwa ujasiri yale ambayo wazazi wao wamewafundisha kuhusu Mungu na Biblia, wanamletea Yehova sifa na heshima na kujiletea baraka.—Mathayo 21:15, 16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki