Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w03 4/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Kitabu Cha Biblia Namba 19—Zaburi
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Nyimbo Zilizoongozwa na Roho Ambazo Zinafariji na Kufundisha
    Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Kwanza cha Zaburi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Mtunga Zaburi Aimba Sifa ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
w03 4/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Kwa nini sura na mistari ya kitabu cha Zaburi hutofautiana katika tafsiri mbalimbali za Biblia?

Tafsiri ya Kifaransa iliyochapishwa na Robert Estienne mwaka wa 1553 ndiyo Biblia nzima ya kwanza iliyokuwa na sura na mistari. Hata hivyo, yaonekana kitabu cha Zaburi kilikuwa na sura na mistari muda mrefu sana kabla ya mwaka huo, kwa kuwa kilikuwa ni mkusanyo wa zaburi mojamoja, au nyimbo, zilizotungwa na watu kadhaa.

Yaonekana, kwanza Yehova alimwongoza Daudi kukusanya zaburi hizo ili zitumiwe katika ibada. (1 Mambo ya Nyakati 15:16-24) Inaaminika kwamba baadaye Ezra, kuhani na “mwandishi mwepesi,” alikusanya kitabu chote cha Zaburi kama kilivyo leo. (Ezra 7:6) Kwa hiyo, kitabu cha Zaburi kilikuwa na zaburi mojamoja kilipokusanywa.

Katika hotuba ambayo mtume Paulo alitoa katika sinagogi la Antiokia (Pisidia) katika safari yake ya kwanza ya umishonari, alinukuu kitabu cha Zaburi na kusema: “Hata kama vile imeandikwa katika zaburi ya pili, ‘Wewe ni mwana wangu, mimi nimekuwa Baba yako siku hii.’” (Matendo 13:33) Maneno hayo bado yanapatikana katika Biblia leo kwenye zaburi ya 2, mstari wa 7. Hata hivyo, sura na mistari ya kitabu cha zaburi hutofautiana katika tafsiri mbalimbali za Biblia. Hiyo ni kwa sababu Biblia fulani zimetafsiriwa kutoka maandishi ya Kiebrania ya Wamasora, ilhali nyingine zimetafsiriwa kutoka Septuagint ya Kigiriki, ambayo ni tafsiri ya maandishi ya Kiebrania yaliyokamilishwa karne ya pili K.W.K. Kwa mfano, katika Biblia nyingi za Wakatoliki ambazo zimetafsiriwa kutoka kwa Biblia ya Kilatini ya Vulgate, zaburi zinafuata mpangilio wa sura na mistari ya Biblia ya Septuagint, ilhali New World Translation na Biblia nyingine hufuata mpangilio wa maandishi ya Kiebrania.

Kuna tofauti gani hususa? Maandishi ya Kiebrania yana jumla ya Zaburi 150. Lakini, tafsiri ya Septuagint inaunganisha Zaburi ya 9 na ya 10, na pia Zaburi ya 114 na 115. Isitoshe, inagawanya Zaburi ya 116 kuwa Zaburi mbili na pia Zaburi ya 147. Ingawa idadi ya zaburi hizo ni sawa katika tafsiri ya Septuagint, idadi hiyo inapungua kwa zaburi 1 kuanzia Zaburi ya 10 hadi 146 inapolinganishwa na maandishi ya Kiebrania. Hivyo, Zaburi ya 23 ambayo inajulikana sana imeorodheshwa kuwa Zaburi ya 22 katika tafsiri ya Douay Version, ambayo mpangilio wake wa sura na mistari unafuata tafsiri ya Kilatini ya Vulgate, ambayo inafuata tafsiri ya Septuagint.

Hatimaye, huenda mistari ya zaburi kadhaa ikatofautiana katika tafsiri mbalimbali. Kwa nini? Hiyo ni kwa sababu tafsiri fulani hufuata “desturi ya Wayahudi ya kuyaona maandishi ya utangulizi kuwa mstari wa kwanza,” yasema Cyclopedia ya McClintock na Strong, lakini nyingine hazifanyi hivyo. Kwa kweli, mara nyingi ikiwa maandishi ya utangulizi ni marefu, yanagawanywa kuwa mistari miwili, hivyo kuongeza idadi ya mistari katika zaburi inayohusika.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki