Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bm seh. ya 11 uku. 14
  • Nyimbo Zilizoongozwa na Roho Ambazo Zinafariji na Kufundisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nyimbo Zilizoongozwa na Roho Ambazo Zinafariji na Kufundisha
  • Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Habari Zinazolingana
  • Kitabu Cha Biblia Namba 19—Zaburi
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Kwanza cha Zaburi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Kitabu cha Zaburi-Dawa ya Moyo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
Pata Habari Zaidi
Biblia—Ina Ujumbe Gani?
bm seh. ya 11 uku. 14
Daudi akipiga kinubi huku akiwa anaimba

Sehemu ya 11

Nyimbo Zilizoongozwa na Roho Ambazo Zinafariji na Kufundisha

Daudi na wengine watunga nyimbo kwa ajili ya ibada. Kitabu cha Zaburi kina nyimbo 150

KITABU kikubwa zaidi katika Biblia ni mkusanyo wa nyimbo takatifu. Kitabu hicho kilichukua miaka 1,000 hivi kuandikwa. Kitabu cha Zaburi kina maneno yenye kupendeza na yenye kuchochea sana ya imani kuliko kitabu kingine chochote. Nyimbo hizo za sifa zinafunua hisia mbalimbali za wanadamu, kama vile, shangwe, shukrani, huzuni, sikitiko, na toba. Ni wazi kwamba mtunga-zaburi alikuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Mungu naye alimtumaini. Fikiria baadhi ya mambo yaliyo katika nyimbo hizo.

Yehova ana haki ya kutawala, kuabudiwa na kusifiwa. Katika Zaburi 83:18 tunasoma: “Wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.” Zaburi nyingi zinamsifu Yehova kwa kazi zake za uumbaji, kama vile mbingu zenye nyota, viumbe vya ajabu duniani, na jinsi mwanadamu alivyoumbwa kwa njia ya ajabu. (Zaburi 8, 19, 139, 148) Zaburi nyingine humtukuza Yehova kuwa Mungu ambaye huwawaokoa na kuwalinda washikamanifu wake. (Zaburi 18, 97, 138) Na katika zaburi nyingine anatajwa kuwa Mungu mwenye haki, anayewafariji walioonewa na kuwaadhibu waovu. —Zaburi 11, 68, 146.

Yehova huwasaidia na kuwafariji wanaompenda. Huenda zaburi inayojulikana sana ni ya 23. Katika zaburi hiyo, Daudi anamtaja Yehova kuwa Mchungaji mwenye upendo anayewaongoza, kuwalinda, na kuwajali kondoo wake. Zaburi 65:2 inawakumbusha waabudu wa Mungu kwamba Yehova ni “msikiaji wa sala.” Wengi ambao wametenda dhambi nzito wamefarijiwa sana na Zaburi ya 39 na ya 51. Katika zaburi hizo, Daudi anatubu kwa unyoofu dhambi nzito alizofanya nayo maneno yake yanaonyesha wazi anaamini kwamba Yehova husamehe. Zaburi 55:22 inatuhimiza tumtegemee Yehova na kumtupia mizigo yetu yote.

Yehova ataubadili ulimwengu kupitia Ufalme wa Masihi. Sehemu mbalimbali za kitabu cha Zaburi zinamhusu moja kwa moja Masihi, Mfalme aliyeahidiwa. Zaburi ya 2 inatabiri kwamba Mtawala huyo ataharibu mataifa maovu yanayompinga. Zaburi ya 72 inaonyesha kwamba Mfalme huyo ataondoa njaa, ukosefu wa haki, na uonevu. Kulingana na Zaburi 46:9, Mungu atakomesha vita na kuharibu silaha zote za vita kupitia Ufalme wa Kimasihi. Katika Zaburi ya 37, tunasoma kwamba waovu wataharibiwa, lakini waadilifu wataishi milele duniani, wakifurahia amani na upatano.

—Inatoka kwenye Kitabu cha Zaburi.

  • Zaburi zinaunga mkono jinsi gani haki ya Yehova ya kutawala?

  • Ni zaburi gani zinazoonyesha jinsi Mungu anavyowasaidia na kuwafariji wanaompenda?

  • Kulingana na kitabu cha Zaburi, Yehova ataubadili ulimwengu jinsi gani?

WIMBO ULIO BORA

Katika Wimbo wa Sulemani, mfalme anafunua kwamba hata mtu awe na mali nyingi kiasi gani haimaanishi kwamba anaweza kupata chochote anachotaka hasa kuhusu masuala ya mahaba. Anaandika jinsi alivyojaribu kumshawishi bikira mrembo ambaye tayari alikuwa anampenda mvulana mchungaji. Wimbo huo ulioongozwa na roho unaonyesha kwamba hata watu wanapovutiwa na wengine kimahaba wanapaswa kujizuia wasijiendeshe kwa njia isiyofaa. Mchungaji huyo na mwenzake ni mfano mzuri wa sifa ya kujizuia, kudumisha usafi wa kiadili, na kuwa washikamanifu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki