Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w03 7/1 uku. 3
  • Upendo Ni wa Maana Sana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Upendo Ni wa Maana Sana
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Mpende Mungu Anayekupenda
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Maana ya Kumpenda Jirani Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Upendo—“Njia Bora Zaidi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Mjengwe na Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
w03 7/1 uku. 3

Upendo Ni wa Maana Sana

WATU wa kila umri, tamaduni, lugha, au jamii wanatamani sana kupendwa. Ikiwa tamaa hiyo haitoshelezwi, wanakosa furaha. Mtafiti mmoja wa kitiba aliandika: “Upendo na urafiki ni sababu kuu zinazoweza kutufanya tuwe wagonjwa au tujisikie vizuri, wenye huzuni au wenye furaha, tuteseke au tupone. Ikiwa dawa mpya ya kitiba ingekuwa na matokeo kama hayo, karibu kila daktari nchini angeipendekeza kwa wagonjwa wake. Lingekuwa jambo baya kutokuwaandikia dawa hiyo.”

Hata hivyo, jamii ya kisasa, na hasa vyombo vya habari na watu ambao wanaonwa kuwa mifano ya kuigwa, inatilia mkazo kuwa na mali, mamlaka, umashuhuri, na ngono, badala ya uhitaji wa kibinadamu wa kuwa na shauku, na uhusiano wenye upendo. Walimu wengi wanatilia mkazo miradi ya kimwili na kazi ya kudumu, nao wanatumia mambo hayo kukadiria mafanikio ya mtu. Ni kweli, elimu na kukuza uwezo mbalimbali wa akili ni mambo ya maana, lakini je, mambo hayo yanapaswa kufuatiliwa sana hivi kwamba mtu hana wakati kwa ajili ya familia na marafiki? Mwandikaji mmoja wa kale mwenye elimu ambaye alikuwa mchunguzi mwenye hekima wa tabia ya wanadamu alilinganisha mtu mwenye akili lakini ambaye hana upendo na “kipande cha shaba-nyeupe inayovuma au toazi lenye kulia.” (1 Wakorintho 13:1) Watu kama hao wanaweza kuwa matajiri, na hata kuwa wenye umashuhuri, lakini hawawezi kamwe kuwa na furaha ya kweli.

Yesu Kristo, ambaye alikuwa na uelewevu mwingi na upendo wa pekee kwa wanadamu, aliona upendo kwa Mungu na kwa jirani kuwa wenye maana kubwa katika mafundisho yake. Alisema hivi: “Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote. . . . Lazima umpende jirani yako kama wewe mwenyewe.” (Mathayo 22:37-39) Ni wale tu wanaofuata maneno hayo wanaoweza kwa kweli kuwa wanafunzi wa Yesu. Hivyo, alisema hivi: “Kwa hilo wote watajua kwamba nyinyi ni wanafunzi wangu, mkiwa na upendo miongoni mwenu wenyewe.”—Yohana 13:35.

Hata hivyo, mtu anawezaje kukuza upendo katika ulimwengu wa leo? Nao wazazi wanawezaje kuwafundisha watoto wao upendo? Makala inayofuata itazungumzia maswali hayo.

[Picha katika ukurasa wa 3]

Ni jambo gumu kukuza upendo katika ulimwengu wenye kuongozwa na tamaa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki