Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w80 10/1 kur. 19-24
  • Upendo—“Njia Bora Zaidi”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Upendo—“Njia Bora Zaidi”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KAMA VILE YESU ALIVYOWAPENDA WANAFUNZI WAKE
  • PAULO AONYESHA “NJIA BORA ZAIDI”
  • MIFANO YA UPENDO YA KUIGWA NA SISI
  • ‘WAPENDE SANA’ WAAMINI WENZAKO
  • WAONYESHE UPENDO JAMAA NA JIRANI
  • ZAIDI YA YOTE, MWONYESHE MUNGU UPENDO
  • “Endeleeni Kutembea Katika Upendo”
    Mkaribie Yehova
  • Mpende Mungu Anayekupenda
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Upendo katika Matendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Upendo wa Kikristo Wenye Msingi wa Upendo wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
w80 10/1 kur. 19-24

Upendo​—“Njia Bora Zaidi”

“Ninawaonyesheni “njia bora zaidi”​—1 Kor. 12:31, HNWW.

1. Mwanahistoria mzee alionyesha muhtasari ya uchunguzi wake wa matukio ya mambo ya wanadamu kwa kutoa shauri gani?

“PENDANENI.” Mwanahistoria wa miaka 92 alitoa muhtasari fupi ya uchunguzi wake wa muda mrefu wa matukio ya mambo ya wanadamu kwa kutoa shauri hilo fupi. “Somo langu la mwisho la historia,” akaeleza Will Durant, “ni kama lile la Yesu. . . . lijaribuni tu. Upendo ndilo jambo linalofaa zaidi ulimwengu.”

2. Alipokuwa akiwapa wafuasi wake “amri mpya,” Yesu Kristo alisema nini?

2 Katika usiku wake wa mwisho wa maisha yake ya kidunia Yesu Kristo aliwaambia wafuasi wake hivi: “Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.” (Yohana 13:34, 35) Hivyo, basi, ni sifa gani ya kuwatambulisha wanafunzi wa Yesu ingekuwa yenye kutokeza zaidi? Kwa wazi, wangekuwa na upendo kwa mmoja na mwenzake, wangekuwa na upendo wenye kutokeza zaidi kati yao wenyewe. Lakini hiyo ilikuwa “amri mpya” namna gani? Wangependanaje kama vile Yesu alivyokuwa amewapenda?

KAMA VILE YESU ALIVYOWAPENDA WANAFUNZI WAKE

3. Amri ya Yesu juu ya upendo ilikuwa “mpya” katika njia gani?

3 Muda mfupi kabla ya kuwapa hiyo “amri mpya,” kwa unyenyekevu Yesu aliosha miguu ya mitume wake. Tendo lake la wakati huo laonyesha Wakristo kwamba inawapasa kuwatumikia waamini wenzao kwa upendo, hata kwa kuwafanyia kazi zisizo za heshima. (Yohana 13:1-16) Lakini si hayo tu yaliyotiwa ndani ya “amri mpya.” Amri hiyo juu ya upendo ilikuwa “mpya” kwa vile ilihitaji zaidi ya yale yaliyotakiwa na sheria waliyopewa Waisraeli kupitia kwa Musa, ambayo Yesu na wanafunzi wake walikuwa chini yake katika wakati huo. Sheria hiyo ilisema waziwazi hivi: “Umpende jirani yako kama nafsi yako.” (Law. 19:18; Mt. 22:39) Iliwahitaji waonyeshe upendo wa jirani, walakini haikuwahitaji waonyeshe upendo wa kujinyima ambao ungehitaji hata mtu atoe uhai wake kwa ajili ya mwanadamu mwenzake.

4. Yesu alionyeshaje upendo unaotakiwa na hiyo “amri mpya”?

4 “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu,” akasema Yesu, “wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.” (Yohana 15:13) Walakini, hivyo ndivyo alivyofanya Yesu alipoutoa uhai wake kuwa ukombozi kwa ajili ya wanadamu wasiokamilika, wenye dhambi na wanaokufa. (Mt. 20:28; Yohana 3:16; 10:14-18; Rum. 5:12; 6:23) Kwa kweli, maisha ya Yesu ya kidunia na kifo chake vilitoa mfano wa upendo unaotakiwa kuonyeshwa na hiyo “amri mpya.” Chini ya uongozi wa Kristo, Mkristo hapaswi kufanya mema wakati tu nafasi inapojitokeza, bali apaswa achukue hatua ya kwanza katika kuwasaidia wengine kiroho na katika njia nyinginezo.

5. Mmojawapo wa wonyesho ulio mkubwa zaidi wa upendo ni wonyesho upi?

5 Ndiyo, mfuasi wa Yesu Kristo apaswa kufanya kazi akitenda kwa faida ya jirani zake. Nayo ni ipi iliyo njia yenye kutokeza zaidi ya kuonyesha upendo? Basi, ni kuwahubiri wengine na kuwafundisha “habari njema,” kwa kuwa hiyo itawawezesha kupata uzima wa milele! Vivyo hivyo, Mkristo apaswa ‘kutoa si habari njema za Mungu tu, bali vilevile na nafasi yake’ anapofanya kazi na kuwasaidia wale wanaokubali ujumbe huu. (1 The. 2:8) Kwa hakika, anapaswa kuwa tayari kutoa nafsi yake, au uhai, kwa ajili yao.​—1 Yohana 3:16.

6. Wafuasi wa Yesu walipaswa kumpenda kadiri gani?

6 Akitenda katika njia ya upendo, Yesu hakufuata njia iliyo rahisi zaidi. Mahali pake, ‘mashutumu ya wale waliokuwa wakimshutumu Mungu yalimwangukia yeye,’ naye kwa uthabiti alifuata njia iliyomletea upinzani mwingi sana kutoka kwa Shetani na mawakili wake. (Rum. 15:3) Kwa hiyo maisha hayangekuwa rahisi kwa wafuasi wa kweli wa Kristo. Vivyo hivyo, Yesu alionyesha kwamba iliwapasa wampende yeye zaidi kuliko washiriki wa karibu sana wa jamaa na hata kuliko nafsi zao zenyewe. (Luka 14:25-27) Bila shaka, wanafunzi wa Yesu walipaswa kuwapenda washiriki wenzao katika utumishi wa Yehova nao walihitajiwa kuzaa matunda ya kiroho, hata wanapokabiliana na mateso makali.​—Marko 10:29, 30; Yohana 15:8.

PAULO AONYESHA “NJIA BORA ZAIDI”

7, 8. “Njia bora zaidi” iliyotajwa na mtume Paulo katika 1 Wakorintho 12:31 ni njia gani, nayo ilikuwa bora zaidi kuliko nini?

7 Mtume Mkristo Paulo alikazia maana ya upendo alipokuwa akiwaandikia waamini wenzake katika Korintho. Katika siku hizo, nakala za Maandiko zilikuwa chache sana, nayo maarifa kutoka kwa Maandiko yalipitishwa kwa wengine kupitia kwa mafundisho ya mdomo. Kwa hiyo karama za mwujiza (maarifa ya kipekee, kusema katika lugha, na vivyo hivyo) yalikuwa mambo ya maana kwa kundi. “Nami sasa,” akaandika Paulo, “nitawaonyesheni njia bora zaidi.” (1 Kor. 12:4-11, 27-31, HNWW) Hiyo “njia bora zaidi” ilikuwa njia gani?

8 Ilikuwa njia ya upendo, naye alionyesha namna ilivyokuwa ya maana katika maneno haya: “Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika [kwa kuwa roho wana lugha yao wenyewe], kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo [nikikosa upendo]. Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima [ama matatizo yaliyo kama milima au milima halisi, ikiwa ni mapenzi ya Mungu], kama sina upendo, si kitu mimi. Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.”​—1 Kor. 13:1-3; Marko 11:23.

9. Ikiwa hatuishi kulingana na “njia bora zaidi” ya upendo, zinakuwaje jitihada zetu katika utumishi wa Mungu?

9 Ndiyo, hata matendo ambayo yangekuwa ya maana yanakuwa ‘kazi bure’ ikiwa hayatokani na kumpenda Mungu na jirani. (Mt. 22:37-39; Ebr. 6:1) ‘Kujitaabisha katika upendo’ ni jambo la lazima. (1 The. 1:2, 3, NW) Jitihada zetu zote pamoja na kujinyima kunakuwa kazi bure ikiwa hatuishi kulingana na “njia bora zaidi” ya upendo. Si Wakristo wote wa kwanza waliokuwa na uwezo wa kufanya miujiza, kuponya, kusema kwa lugha na kufasiri wakiwa chini ya uongozi wa roho ya Mungu. (1 Kor. 12:29, 30) Walakini wote wangeweza kuonyesha upendo, ambao ni tunda la roho takatifu ya Yehova wanalopaswa Wakristo wote kusitawisha.​—Gal. 5:22; 1 Yohana 4:16.

MIFANO YA UPENDO YA KUIGWA NA SISI

10. Yehova ametuwekeaje mfano katika kuonyesha upendo?

10 Wote wawili Yehova Mungu na Mwanawe Yesu Kristo wametuwekea mifano katika kuonyesha upendo. Ebu fikiria hili: Uumbaji uonekanao ni wonyesho wa upendo wa Mungu, kwa kuwa unatoa ushuhuda mwingi juu ya namna Mungu anavyohangaikia afya, furaha na hali njema ya wanadamu. Wanadamu hawakuumbwa ili wawepo tu. Kwa kawaida wao wanaweza kuonja chakula, wanuse harufu nzuri ya maua, waone rangi mbalimbali zenye kupendeza za uumbaji, na kufurahia ushirika wa wanadamu wenzao na kuchekelea michezo yenye kuchekesha ya wanyama, bila kutaja mambo mengine mengi yenye kufurahisha maishani. (Zab. 139:14) Wonyesho wa Yehova wa kutoa bila choyo katika upendo unatia ndani kumfanya mwanadamu kwa sura Yake na mfano Wake, akiwa na uwezo wa kupenda na kufahamu mambo ya kiroho. (Mwa. 1:26, 27) Mpango wa makao ya paradiso na ahadi hakika ya kurudishwa kwa paradiso ya kidunia yaonyesha vilevile upendo wa Mungu. Vilevile kujifunua kwake kwa wanadamu kupitia kwa Neno lake aliloliongoza na kwa roho takatifu kwaonyesha upendo. (Luka 23:43, NW; 1 Kor. 2:10-13) Na bila shaka, Yehova alionyesha vilevile upendo wake kwa wanadamu kwa kufanya mpango wa kuwakomboa kutokana na dhambi na mauti.​—Rum. 5:7, 8.

11, 12. Mwana wa Mungu amewaonyesha wanadamu upendo katika njia gani?

11 Mwana wa Mungu aliwapenda wanadamu hata wakati wa maisha yake ya kabla ya kuwa mwanadamu. Akifananishwa na hekima, anatambulishwa kuwa “stadi wa kazi” wa Mungu aliyetumikia kwa furaha, naye alisema hivi: “Furaha yangu ilikuwa pamoja na wanadamu.” (Mit. 8:30, 31; Yohana 1:1, 14) Hivyo, akifikiria uhitaji wa wanadamu wa kukombolewa, Yehova alimchagua yule aliyependezwa sana na wanadamu​—Mwanawe pekee, ambaye “alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu.” (FIp. 2:5-7) Ndiyo, Mwana wa Mungu alionyesha upendo wa kujinyima alipokubali kuwa mwanadamu.

12 Yesu Kristo alionyesha upendo wake vilevile katika mafundisho yake na katika kuwafikiria wengine katika njia ya upendo. Wakati alipouona mkutano mkubwa, “akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao.” “Kwa sababu walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji,” Yesu aliwahurumia “akaanza kuwafundisha mambo mengi.” (Mt. 14:14; Marko 6:34) Bila shaka, Yesu Kristo alionyesha upendo ulio bora zaidi kwa kufa juu ya mti wa mateso ili “kuwakomboa watu wengi.” (Mat. 20:28, HNWW; Flp. 2:8) Katika njia hii na katika njia nyingine nyingi, wote wawili Yehova Mungu na Yesu Kristo wametoa mifano ya upendo ya kuigwa na Wakristo.​—Yohana 13:34; 1 Yohana 4:10.

‘WAPENDE SANA’ WAAMINI WENZAKO

13. (a) Petro aliwahimiza waamini wenzake wawe na upendo wa namna gani mtu na mwenzake, na je! kuna ushuhuda wo wote kuonyesha kwamba walikuwa na upendo wa namna hiyo kati yao? (b) Upendo una matokeo gani juu ya Wakristo wa leo?

13 Upendo unaonyeshwa kwa kuwa na nia ya kujitoa nao ni jambo la maana sana katika maisha ya wale wanaomwogopa Mungu. (Zab. 110:3) Mtume Petro aliwahimiza waabudu wenzake wa Yehova ‘wapendane sana.’ (1 Pet. 4:8) Kwamba upendo wa namna hiyo ulikuwamo kati ya Wakristo wa kwanza inaonyeshwa na usemi wao, kwa kuwa wanajulikana kwamba walikuwa ‘wakiitana kwa maneno yanayoonyesha upendo​—“watoto wangu wapenzi,” “mpenzi, nimpendaye katika kweli,” na vivyo hivyo. (1 Kor. 4:14, HNWW; 3 Yohana 1) Upendo kama uo huo kati ya Wakristo wa kweli leo unatia moyo, ukimtegemeza mtu wakati wa majaribu. “Hujenga.” (1 Kor. 8:1) Mateso na misiba vijapokuwapo, hatuachwi bila rafiki katika ulimwengu usio na upendo. Wakristo wanajua kwamba ndugu na dada zao wa kiroho wanawapenda kweli kweli, nacho hiki “kifungo cha ukamilifu” kinawasaidia waukabili wakati ujao wakiwa na uhakika.​—Kol. 3:14.

14. (a) Paulo anaonyeshaje muhtasari ya upendo katika 1 Wakorintho 13:4-8? (b) Ni maulizo gani yanayoweza kumsaidia Mkristo aonyeshe upendo kulingana na maneno ya Paulo?

14 Lakini ulizo ni hili, Sisi binafsi tunawaonyesha upendo waamini wenzetu kadiri gani? Muhtasari ya upendo ya mtume Paulo iliyoongozwa na Mungu inatusaidia tujaribu ubora wa upendo wetu kwa wengine. Tafadhali soma 1 Wakorintho 13:4-8. Kisha utumie wakati uyafikirie maneno hayo kwa kutumia maulizo haya yanayofuata:

Je! mimi ‘ninavumilia na kufadhili,’ nikionyesha subira katika hali zisizofaa?

Je! mimi ninajiepusha na wivu, kama vile katika wakati ninapoachwa na ndugu mwingine kupewa mapendeleo fulani kundini?

Je! mimi ni mnyenyekevu badala ya kujisifu juu ya yale ambayo Yehova ananiruhusu kutimiza katika utumishi wake?

Je! mimi ‘ninakosa kuwa na adabu,’ katika tabia au katika njia ninayotumia kuwatendea Wakristo wenzangu?

Je! mimi ‘ninatafuta faida zangu mwenyewe,’ kama vile katika mambo madogo kwa kulinganisha katika kwenda mbele ya wengine katika makusanyiko ya Kikristo?

Kwa mfano, kama mzee, ‘ninaona uchungu’ kwa sababu tu wengine wanashindwa kuitikia mara moja mashauri ya Kimaandiko?

Je! mimi ‘ninahesabu mabaya,’ makosa ya miaka mingi iliyopita, au ninawasamehe ndugu na dada zangu katika imani, kama vile na mimi ninavyotamani kusamehewa?

Katika mazungumzo, je! mimi ninaonyesha kwamba najiepusha na udhalimu wa ulimwengu, mahali pake, nikifurahi katika kweli?

Je! mimi “huvumilia yote,” bila kutazamia ukamilifu kutoka kwa Wakristo wenzangu wasiokamilika?

Je! mimi ni mtu ‘anayeamini yote,’ bila kuwatungia nia mbaya waamini wenzangu isivyo haki?

Maulizo kama hayo yaweza kumsaidia Mkristo katika jitihada zake za kuonyesha upendo.

15. Upendo umewasukuma watu wa Yehova wawafanyie nini waabudu wenzao walio na uhitaji?

15 Kwa kweli, njia za kuwaonyesha upendo waamini wenzetu ni nyingi. Kwa mfano, upendo unatuongoza tuwape msaada wa mambo ya kimwili kunapokuwa na uhitaji. (Yak. 2:14-17) Kwa hiyo, watu wa Yehova waliwasaidia waabudu wenzao katika nchi zilizopatwa na maafa ya vita baada ya Vita ya Ulimwengu ya Pili. Katika mpango wa kipindi cha miaka miwili na nusu ya kutoa misaada ulimwenguni pote, upendo ulionyeshwa wakati mashahidi wa Yehova katika United States, Canada, Switzerland, Sweden na nchi nyinginezo walipotoa misaada ya nguo na fedha za kuwanunulia chakula Wakristo katika Austria, Belgium, Bulgaria, China, Czechoslovakia, Denmark, Uingereza, Finland, Ufaransa, Ujeremani, Ugiriki, Hungary, Italia, Netherlands, Norway, Filipino, Poland na Romania. Zaidi ya hayo, katika muda wote wa miaka, Mashahidi wa Yehova wametoa kwa furaha misaada ya mambo ya kimwili, kama vile ilivyohitajiwa, wakati waamini wenzao wamepatwa na misiba ya asili.

16. Upendo wapaswa kuwa na matokeo gani juu ya wazee waliowekwa kundini?

16 Vilevile upendo wa Kikristo unawafanya wazee wa kundi waliowekwa wawe wenye kuambilika, na wenye kufahamu. Ndivyo inavyopaswa kuwa ikiwa wao wanaiga njia za Yehova, ambaye kwa habari zake imesemwa hivi: “[Kama vile] mbingu zilivyoinuka juu ya nchi, kadiri ile ile rehema zake ni kuu kwa wamchao.” (Zab. 103:10-14) Nia ya upendo na ya unyenyekevu inawaongoza waangalizi Wakristo wajitahidi kwa bidii katika kuwasaidia waamini wenzao kiroho.

17. Wakristo walio wazee au walio na udhaifu wa mwilini waweza kuonyeshwa upendo katika njia gani?

17 Walakini, upendo wa Kikristo utawasukuma watu wote wanaomwogopa Mungu, wala si wazee waliowekwa peke yao, washirikiane na kuwa wenye kusaidia katika kushughulika na waabudu wenzao wa Yehova. Kwa mfano, upendo waweza kutusukuma tuwafanyie Wakristo wazee au wenye udhaifu wa mwili kazi ya kwenda dukani na kuwanunulia vitu wanavyohitaji. Waweza kutusukuma tuwasomee Biblia na vitabu vya Kikristo vya kueleza Biblia, ikiwa lazima. Ndiyo, na kwaweza kuwa na nafasi za kuwasaidia kazi za nyumbani, kwenda pamoja nao katika utumishi wa Mungu, na kushiririkiana nao kwa furaha katika nyakati nyinginezo. Upendo utatuongoza tuwafanyie wengine mema katika njia mbali-mbali​—vijana kwa wazee—​pasipo kungojea tuombwe kufanya hivyo.

WAONYESHE UPENDO JAMAA NA JIRANI

18. Je! tunahitaji amri zinazohusu kila sehemu ya maisha ili tuonyeshe upendo?

18 Mtume Paulo aliandika hivi: “Msiwe na deni kwa mtu ye yote, isipokuwa tu deni la kupendana.” (Rom. 13:8, HNWW) Kwa hakika Wakristo wana deni ya kuwapenda wengine. Walakini ili tuonyeshe sifa hii hatuhitaji amri zinazotia ndani kila sehemu ya maisha. Dhamiri ya kibinadamu pamoja na hekima ya kimungu kutoka kwa Maandiko vyatuonyesha namna ya kuonyesha upendo katika maneno na matendo. (Rum. 2:14, 15) Hivyo, kwa kawaida, kama wakristo tunajua kama tumeonyesha upendo au sivyo katika hali fulani. Hata hivyo, ni jambo moja kujua kwamba inatupasa kuonyesha upendo na kuuonyesha.

19. Ni nini kinachoweza kutusaidia kuonyesha upendo katika jamaa, nao unaweza kuonyeshwa katika njia gani?

19 Kati ya jamaa, huenda nyakati nyingine tukawa na maelekeo ya kuwa wepesi wa hasira, wasioonyesha upendo. Sababu gani? Kwa sababu tunafahamiana vizuri sana na washiriki wa jamaa nasi huenda tukakosa kuwasubiri kama vile tunavyowasubiri wengine. Hata hivyo, kanuni zile zile za Biblia zinatumika jinsi ile ile kati ya washiriki wa jamaa kama vile katika kushughulika na watu wengine mmoja mmoja, kama vile wale walio katika kundi la Kikristo la mahali petu. Bila shaka twaweza na twapaswa kutafuta msaada wa Yehova kupitia kwa sala katika kuwaonyesha upendo washiriki wa jamaa yetu. Katika jambo hili tutapata msaada tukikumbuka kwamba Yehova Mungu anafurahi wakati waume wanapowapenda wake zao “kama miili yao wenyewe,” wakati wanawake wanapowapenda waume wao na watoto wao, na wakati watoto wanapowapenda wazazi wao, na kuwatii. (Efe. 5:28; 6:1-3; Tito 2:4) Hata watoto ambao wamekuwa watu wazima wanaweza kuwaonyesha upendo wazazi wao wanaozeeka, kwa kuwaangalia kiroho na kimwili kulingana na mahitaji yao. Utawa unatia ndani kuchukua daraka hilo. Na bila shaka, waume Wakristo wanaonyesha upendo wanapohakikisha kwamba washiriki wa jamaa zao wametoshelezewa mahitaji yao ya mambo ya kiroho na ya kimwili.​—Linganisha Mithali 19:26; 1 Timotheo 5:4, 8.

20. Upendo wa jirani waweza kuonyeshwa katika njia gani, sana sana na Wakristo?

20 Upendo wa jirani waweza kuonyeshwa kwa matendo ya fadhili za kibinadamu katika hali mbalimbali. Wakaaji wa Melita walimwonyesha mtume Paulo pamoja na wengine waliovunjikiwa merikebu “fadhili zisizokuwa za kawaida.” (Matendo 28:1, 2) Dhamiri za wapagani hao wakaaji wa kisiwa ziliwaongoza watende hivyo. Dhamiri za Wakristo zilizozoezwa kwa Maandiko zapaswa kuwaongoza waonyeshe upendo wa jirani kwa kadiri kubwa hata zaidi! Upendo huo wa jirani ndio sana sana unaotusukuma tushiriki “habari njema” pamoja nao. Hakuna jambo jingine jema zaidi au la upendo zaidi kuliko kuwasaidia kupata hali inayokubalika mbele za Yehova.​—1 Tim. 1:8-11.

ZAIDI YA YOTE, MWONYESHE MUNGU UPENDO

21, 22. (a) Ni ipi iliyo njia kubwa ya kumwonyesha Yehova upendo? (b) Kwa hiyo ni maulizo gani tunayoweza kujiuliza nasi twapaswa kuwa na azimio gani kama ‘wapenda Yehova’?

21 Kweli kweli, mojayapo ya njia zilizo kubwa zaidi za kuonyesha upendo kwa wanadamu wenzetu ni ile ya kuwafundisha “habari njema,” na hivyo kuwasaidia wawe na hali yenye kukubalika mbele za Yehova Mungu. Na kwa Mkristo, utendaji huo ni mojayapo ya njia kubwa za kumwonyesha upendo Yeye anayestahili zaidi kuonyeshwa upendo​—Mungu wetu atupendaye, Yehova. Mwanawe alisema hivi: “Mpende [Yehova] Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote.”​—Luka 10:27.

22 Je! sisi ‘tunaendelea kusimama imara kana kwamba twamwona Yeye asiyeonekana’? (Ebr. 11:27, NW) Je! sisi tunalichukua jina lake lisilolinganika, Yehova, tukiwa mashahidi wake waaminifu? Je! tunafurahia sana kwa moyo kusema juu yake na juu ya makusudi yake? Na kwa kweli, je! hiyo si ndiyo sababu kubwa ya kuwapo kwa kundi la watu wake? Kwa hakika, ndiyo! Tukiwa chini ya uongozi wa roho yake takatifu, twaweza kuendelea kufuata “njia bora zaidi” ya upendo tukiwa pamoja na wanadamu wenzetu. Na zaidi ya yote, na tuendelee bila woga kuzitangaza sifa za Mungu wetu, tukipenda yaliyo mema na kushangilia katika yeye tukiwa ‘wapenda Yehova’ wenye kushika ukamilifu.​—Zab. 97:10-12, NW.

[Picha katika ukurasa wa 20]

Tendo la Yesu la unyenyekevu laonyesha kwamba inatupasa kuwatumikia wengine kwa upendo

[Picha katika ukurasa wa 24]

Tafuta msaada wa Yehova katika kuonyesha upendo katika jamaa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki