Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w03 12/1 uku. 8
  • Kipindi cha Televisheni Kilimfanya Amtukuze Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kipindi cha Televisheni Kilimfanya Amtukuze Mungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Watu Wote Wanaalikwa!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Je, Hii Yaweza Kuwa Kazi-Maisha Inayokufaa Zaidi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Je, Waweza Kujitolea?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Kutazama “Nyumba ya Mungu” kwa Uthamini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
w03 12/1 uku. 8

Ripoti ya Watangazaji wa Ufalme

Kipindi cha Televisheni Kilimfanya Amtukuze Mungu

MTUME Paulo alisema kwamba “wengine wanamhubiri Kristo kwa wivu na kushindana, lakini wengine pia kwa nia njema.” (Wafilipi 1:15) Nyakati nyingine, hata wale wanaojaribu kuwavunjia heshima watu wa Yehova wamewasaidia bila kujua watu wenye moyo mnyoofu wavutiwe na kweli.

Mwezi wa Novemba 1998, kipindi kilichoonyesha picha za Betheli, majengo ya ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova huko Louviers, Ufaransa, kilionyeshwa katika televisheni ya kitaifa ya Ufaransa. Ijapokuwa watu walikuwa na maoni yaliyotofautiana kukihusu, kipindi hicho kilitokeza mambo mazuri yasiyotazamiwa.

Anna-Paula alikuwa mmoja wa wale waliotazama kipindi hicho, naye aliishi kilometa 60 tu kutoka Betheli. Anna-Paula, ambaye ni mama aliyetalikiwa mwenye watoto wawili, alikuwa anatafuta kazi. Basi asubuhi iliyofuata, alipiga simu Betheli ili kuuliza kazi ya kuajiriwa hapo. Akasema, “nilikuwa na maoni kwamba palikuwa mahali pazuri na kwamba kazi inayofanywa hapo ilikuwa yenye faida.” Lo! Jinsi alivyoshangaa kusikia kwamba wale wote wanaotumikia Betheli ni wahudumu wa kujitolea! Baada ya mazungumzo mafupi kuhusu kazi za Mashahidi wa Yehova, alikubali Shahidi amtembelee.

Wakati Léna, mtumishi wa wakati wote katika kutaniko la hapo, alipomtembelea, mazungumzo marefu yakaanza, naye Anna-Paula akakubali kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele.a Kwenye ziara iliyofuata, tayari Anna-Paula alikuwa amekisoma kitabu hicho chote naye alikuwa na maswali mengi. Alikubali mara moja funzo la Biblia. Anna-Paula alisema: “Kwangu mimi, hiyo ilikuwa nafasi ya kuligundua Neno la Mungu. Sikuwa nimewahi kushika Biblia hapo zamani.”

Anna-Paula alitembelea Betheli mwezi wa Januari, na juma lililofuata akahudhuria mkutano wake wa kwanza wa Kikristo. Muda mfupi baadaye, akaanza kujifunza Biblia na watoto wake wawili na kuwahubiria marafiki wake. Anasema, “sikuweza kujizuia nisiwaambie wengine yale niliyokuwa nikijifunza. Nilitaka kuwaambia wengine kweli za Biblia na kuwafariji.” Baada ya kujitahidi kushinda matatizo yake mwenyewe, Anna-Paula alianza kuhudhuria mikutano kwa ukawaida. Alifanya maendeleo haraka na kubatizwa mnamo Mei 5, 2002.

Zaidi ya hayo, kutokana na mfano bora na kuhubiri kwa bidii kwa Anna-Paula, mama yake alianza kujifunza Biblia naye akabatizwa muda mfupi baadaye. “Shangwe niliyo nayo haiwezi kuelezwa kwa maneno,” asema Anna-Paula. “Ninamshukuru Yehova kila siku kwa kunikubali mimi na kwa baraka zote ambazo amenipa.”

[Maelezo ya Chini]

a Kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

[Picha katika ukurasa wa 8]

Juu: Anna-Paula

Chini: Lango la ofisi ya tawi ya Ufaransa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki