Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w06 7/1 uku. 32
  • Ziara Iliyobadili Mtazamo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ziara Iliyobadili Mtazamo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
w06 7/1 uku. 32

Ziara Iliyobadili Mtazamo

“NILITAKA sana kuieleza familia yangu kuhusu ‘malaika’ wawili ambao Mungu alinitumia.” Hayo ni maneno ya mtu mmoja aliyetembelewa na wasichana wawili ambao ni Mashahidi wa Yehova. Majuma kadhaa kabla ya kutembelewa na wasichana hao, mke wake alikuwa amekufa. Walikuwa wameoana kwa miaka 45. Mtu huyo alihuzunika sana. Watoto wake ambao ni watu wazima walikuwa wamemfariji, lakini waliishi mbali sana. Marafiki na majirani hawakumtembelea.

Wasichana hao walipomtembelea, mtu huyo alisema hivi: “Nimeacha kusali kwa Mungu kwa sababu sihisi tena kwamba nina uhusiano wa karibu pamoja naye.” Hata hivyo, wasichana hao walimhurumia, nao wakamwachia trakti yenye kichwa Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa?, ambayo inazungumzia Biblia. Aliisoma jioni hiyohiyo na kufarijika.

Baada ya muda usio mrefu, wasichana hao walirudi. Walikumbuka jinsi alivyokuwa mwenye huzuni katika ziara yao ya kwanza, hivyo walitaka kumjulia hali. Mtu huyo aliandika hivi baadaye: “Nilishangaa kwamba watu wawili nisiowajua walinijali na kunihangaikia.” Mambo waliyomweleza kutoka katika Biblia yalimfariji. Wasichana hao walisema watarudi. Mtu huyo alifurahi, naye akachochewa kuandika maelezo hayo yaliyonukuliwa hapo juu katika barua aliyotuma kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova la kwao.

Kabla ya kuhamia karibu na mahali ambapo mtoto wake mmoja anaishi, mtu huyo alihudhuria mkutano wa Kikristo wa Mashahidi wa Yehova, na akala pamoja na familia ya mmoja wa wale wasichana waliomhubiria. Aliandika hivi: “Ninaondoka eneo hili, lakini nitaendelea kukumbuka na kusali kwa ajili ya wasichana hao na kanisa lenu. Naam, siku hizi ninasali sana. Nimebadili mtazamo wangu kabisa. Wasichana hao walinisaidia sana kufanya hivyo, nami nitawashukuru milele.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki