Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w06 8/15 kur. 2-3
  • Wapole Watairithi Dunia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wapole Watairithi Dunia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Habari Zinazolingana
  • “Tutaonana Paradiso!”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Paradiso Inayotajwa Katika Biblia Iko Wapi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • “Duniani Kama Ilivyo Mbinguni”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • “Utakuwa Pamoja na Mimi katika Paradiso”
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
w06 8/15 kur. 2-3

Wapole Watairithi Dunia

“Ninawazia kwamba ulimwengu utageuzwa na kufanywa upya. . . . Si kesho asubuhi, bali baada ya muda mrefu sana, wakati ambapo kutakuwa na mbingu mpya na dunia mpya.”—Jean-Marie Pelt, mtaalamu Mfaransa wa mambo ya mazingira.

WAKIWA wenye kufadhaika kwa sababu ya hali za mazingira na za kijamii duniani, watu wengi wangefurahi sana kuona dunia ikigeuzwa kuwa paradiso. Naam, tumaini hilo si ndoto tu ya karne ya 21. Biblia ilitabiri zamani kwamba dunia itakuwa Paradiso tena. Maneno ya Yesu kwamba “walio na tabia-pole . . . watairithi dunia” na “mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni,” ni miongoni mwa maneno yanayojulikana sana katika Biblia. (Mathayo 5:5; 6:10) Lakini, leo, si wengi wanaoamini kwamba dunia itakuwa paradiso itakayokaliwa na watu wapole. Watu wengi wanaodai kuwa Wakristo hawaamini kwamba dunia itakuwa Paradiso tena.

Gazeti moja la Ufaransa la kila juma (La Vie) linaeleza kwa nini imani kuhusu paradiso duniani au mbinguni imetupiliwa mbali, hasa katika Kanisa Katoliki: “Baada ya kufundishwa kwa karne 19 hivi katika dini ya Katoliki, [wazo la] paradiso halitajwi tena kwenye makesha, mahubiri ya Jumapili, mafundisho ya theolojia, na masomo ya katekisimu.” Inasemekana kuwa neno ‘paradiso’ ‘halieleweki,’ kwamba ni ‘fumbo na hutokeza mvurugo.’ Wahubiri fulani huliepuka kimakusudi kwa sababu “linawafanya watu wawazie mambo mengi kuhusu maisha yenye furaha duniani.”

Frédéric Lenoir, mtaalamu wa elimu ya jamii na dini, anasema kwamba wazo la paradiso “limekuwa la kawaida tu.” Vivyo hivyo, Jean Delumeau, mwanahistoria na mtungaji wa vitabu vingi vinavyozungumzia paradiso, anadhani kwamba ahadi za Biblia hazitatimizwa kwa njia halisi. Anaandika hivi: “Kuhusu swali, ‘Je, kuna tumaini lolote kuhusu Paradiso?’ fundisho la Kikristo linajibu hivi: Kwa sababu ya ufufuo wa Mwokozi, siku moja sote tutaungana na kushuhudia utimizo wa tumaini letu.”

Je, ujumbe unaosema kwamba dunia itakuwa paradiso bado ni muhimu? Dunia hii itakuwaje wakati ujao? Je, wakati ujao unajulikana vizuri au haujulikani? Makala inayofuata itajibu maswali hayo.

[Picha katika ukurasa wa 2 zimeandaliwa na]

COVER: Emma Lee/Life File/Getty Images

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki