Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w06 11/15 uku. 31
  • Wafundishe Watoto Wako Kutoa Maelezo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wafundishe Watoto Wako Kutoa Maelezo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Habari Zinazolingana
  • Msifu Yehova Katika Kutaniko
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Tianeni Moyo Katika Mikutano ya Kutaniko
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Ni Njia Gani Bora ya Kujitayarisha kwa Ajili ya Mikutano?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Lishike Sana Ungamo la Tumaini Lako Lisigeuke
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
w06 11/15 uku. 31

Wafundishe Watoto Wako Kutoa Maelezo

PERLA kutoka Mexico anakumbuka kwamba alipokuwa msichana mdogo, mama yake alimsaidia kutayarisha maelezo mafupi ya kutoa katika Funzo la Mnara wa Mlinzi. Sasa Perla ana mtoto mvulana mwenye umri wa miaka mitano. Yeye humsaidiaje? “Kwanza ni lazima nitayarishe. Ninapofanya hivyo, ninatafuta fungu ambalo mtoto wangu anaweza kuelewa,yaani, lile ambalo anaweza kuelezea kwa maneno yake mwenyewe. Kisha, tunakazia fikira fungu hilo ambalo yeye huliita ‘fungu langu.’ Mimi humwomba atoe maelezo kuhusiana na fungu hilo akitumia mifano ya kawaida maishani. Halafu, tunafanya mazoezi ya kutoa maelezo hayo mara kadhaa. Tunatumia kitu kinachofanana na kikuza-sauti ili ajue jinsi ya kushika kikuza-sauti anapotoa maelezo. Ninafurahi sana kwa sababu yeye huinua mkono wake au kutoa maelezo katika kila mkutano. Mara nyingi, kabla ya mkutano kuanza, yeye humfikia yule atakayeongoza na kumwambia fungu ambalo angependa kutoa maelezo.”

Jens, mzee anayeshirikiana na kikundi cha lugha ya Kihindi, ana watoto wawili wavulana, mmoja ana umri wa miaka miwili na yule mwingine miaka minne. Wakati Jens na mke wake wanapotayarisha mikutano pamoja na watoto wao, wanatumia njia ambayo Jens alijifunza kutoka kwa wazazi wake. Anasema hivi: “Tunachagua sehemu ambazo watoto wanaweza kuelewa. Kisha, tunajaribu kuwaeleza kwa ufupi habari inayozungumziwa au jambo kuu la makala hiyo. Halafu, tunawauliza maswali ambayo tunataka wajibu mikutanoni. Mara nyingi, tunashangaa tunaposikia majibu wanayotoa kwa maneno yao wenyewe. Maelezo yao yanaonyesha kikweli mambo ambayo wanaelewa. Kwa njia hiyo, maelezo yao yanamletea Yehova sifa na yanaonyesha imani yao.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki