Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/94 uku. 1
  • Lishike Sana Ungamo la Tumaini Lako Lisigeuke

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Lishike Sana Ungamo la Tumaini Lako Lisigeuke
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Tianeni Moyo Katika Mikutano ya Kutaniko
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Msifu Yehova Katika Kutaniko
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Waangalizi Wanaoongoza —Kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Msifu Yehova ‘Katikati ya Kutaniko’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 3/94 uku. 1

Lishike Sana Ungamo la Tumaini Lako Lisigeuke

1 Funzo la Mnara wa Mlinzi ni njia ya msingi ambayo ‘chakula cha kiroho kwa wakati wake’ kinaandaliwa kwa watu wa Mungu leo. (Mt. 24:45) Twahudhuria mkutano huu wa maana kwa malengo mawili makuu—kujengwa kiroho na kufanya ungamo la tumaini letu kwa wengine.—Ebr. 10:23-25.

2 Kujinufaisha Wenyewe: Inakadiriwa kwamba katika makutaniko mengi ni theluthi moja tu ya wasikilizaji wanaojifunza somo hilo mapema. Karibu idadi hiyohiyo ndiyo hushiriki kujibu. Chakula kigumu kilichomo katika Funzo la Mnara wa Mlinzi hakiwezi kushikwa kabisa kikamili wakati wa mkutano tu. Wahitaji kukomboa wakati ili kujifunza habari hiyo mapema.

3 Unapotayarisha funzo, huenda ukaona inasaidia kusoma kwanza na kufikiri juu ya maswali yaliyomo katika sanduku lililo karibu na mwisho wa makala hiyo. Jambo hilo laweza kukusaidia ukazie fikira zako mambo makuu yatakayozungumzwa katika somo.

4 Sikiliza kwa uangalifu yale yanayosemwa wakati wa funzo. Toa uangalifu kwenye maelezo ya kufungua ya kiongozi wa funzo; maelezo hayo hutoa utangulizi wa funzo. Huenda akatokeza maswali matatu au manne ambayo yatajibiwa, au huenda akapitia mambo makuu ya somo la juma lililopita ikiwa somo la juma hili ni wendelezo wa habari hiyohiyo. Ikiwa kuna marekebisho fulani katika kuelewa kwetu unabii wa Biblia au kanuni ya Kimaandiko, yeye ataelekeza fikira zetu kwenye jambo hilo. Bila shaka, ni lazima maelezo ya mwenye kuongoza yawe mafupi, kwa kuwa lengo moja la funzo ni kutolea kutaniko fursa ya kueleza tumaini lao. Sikiliza kwa uangalifu wengine wanapotoa maelezo ya mambo ambayo wamejifunza; jambo hilo laweza kusaidia kuimarisha imani yako.

5 Tangaza Tumaini Lako: Je! wewe hutoa maelezo kwa kawaida wakati wa funzo? Maelezo mafupi, yenye kulenga shabaha yanafaa. (Linganisha Luka 21:1-4.) Jibu rahisi kutoka moyoni linathaminiwa na wote. Kwa kawaida jibu la kwanza kwa swali lapaswa kuwa fupi na la moja kwa moja. Hilo huruhusu wengine wataje andiko au kuelekeza uangalifu kwenye jambo fulani la ziada katika fungu. Kwa njia hii wengi wanaweza kuungama peupe tumaini lao. Maelezo yapaswa kuwa ya mwelekeo unaofaa na yenye kujenga sikuzote.

6 Ikiwa umeanza tu kuhudhuria funzo hili au unaona haya kujibu, unaweza kuuliza kiongozi akusaidie. Mwombe atafute mkono wako wakati fungu fulani linaposhughulikiwa. Labda waweza kujitolea kusoma andiko lililowekwa bila manukuu na kueleza kifupi jinsi liwezavyo kutumiwa. Unaweza kuandika maandishi machache kandokando ya kukusaidia ukumbuke unalotaka kusema unapotoa elezo. Ikiwa wewe ni kijana, kumbuka kwamba maelezo yako yanapokelewa na yanathaminiwa.—Mt. 21:16.

7 Ni muhimu kwamba tuonyeshe imani yetu, na Funzo la Mnara wa Mlinzi hutoa fursa nzuri ya kufanya hivyo. Ikiwa unasita-sita kutoa elezo, fanya uwezalo ili ushinde tatizo hilo, na jisukume utoe angalau jibu moja. Utakuwa umechangia mkutano, nawe utahisi vizuri ukifanya hivyo. Kwa hiyo kwa nini usipange kutoa angalau elezo moja kwenye Funzo lifuatalo la Mnara wa Mlinzi?—Mit. 15:23.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki