Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w07 6/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Habari Zinazolingana
  • “Mlee Mvulana Kulingana na Njia Inayomfaa”
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
  • Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Kuwapa Watoto Uangalifu Wanaohitaji
    Amkeni!—2005
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
w07 6/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Je, Methali 22:6 inatoa uhakikisho kamili wa kwamba ikiwa watoto Wakristo wanazoezwa kwa njia inayofaa, hawataacha njia ya Yehova?

Andiko hilo linasema hivi: “Mlee mvulana kulingana na njia inayomfaa; hata atakapozeeka hatageuka kando na kuiacha.” Kama vile tu kukunja tawi changa kunavyousaidia mti kukua kwa njia inayofaa, watoto wanaozoezwa kwa njia inayofaa wanakuwa na mwelekeo mkubwa zaidi wa kuendelea kumtumikia Yehova wanapokuwa watu wazima. Kama kila mzazi anavyojua, mazoezi hayo yanahitaji wakati na jitihada. Ili watoto wao wawe wanafunzi Wakristo, ni lazima wazazi wawafundishe watoto, wawashauri, wawahimize, na kuwatia nidhamu kwa uangalifu na vilevile kuwawekea mfano mzuri. Ni lazima wafanye hivyo kwa kuendelea na kwa upendo kwa miaka mingi.

Lakini je, hilo linamaanisha kwamba ikiwa mtoto ataacha kumtumikia Yehova, wazazi hawakumzoeza kwa njia inayofaa? Katika visa fulani, huenda wazazi hawakujitahidi vya kutosha kuwalea watoto wao katika nidhamu na mwongozo wa akilini wa Yehova. (Waefeso 6:4) Kwa upande mwingine, methali hiyo si uhakikisho kamili wa kwamba mazoezi mazuri yatawafanya watoto wawe waaminifu kwa Mungu. Wazazi hawawezi kufanya watoto wao wawe vile wanavyopenda. Watoto wana uhuru wa kuchagua kama vile tu watu wazima, na ni lazima wachague njia watakayofuata katika maisha yao. (Kumbukumbu la Torati 30:15, 16, 19) Hata wazazi wakijitahidi sana, watoto fulani wanakosa uaminifu, kama Sulemani ambaye aliandika andiko tunalozungumzia. Hata Yehova alikuwa na wana ambao hawakuendelea kuwa waaminifu.

Kwa hiyo, andiko hilo halimaanishi kwamba katika kila kisa mtoto “hatageuka kando na kuiacha” njia, lakini linamaanisha kwamba kwa kawaida matokeo yatakuwa hayo. Hilo ni jambo lenye kuwatia moyo sana wazazi! Wazazi wanapaswa kutiwa moyo kujua kwamba jitihada zao nyingi za kuwazoeza watoto wao kufuata njia ya Yehova zitafanikiwa. Kwa kuwa daraka lao ni la maana na uvutano wao ni mkubwa, wazazi wanahimizwa wachukue daraka lao kwa uzito.—Kumbukumbu la Torati 6:6, 7.

Hata watoto wanapogeuka na kuacha kumtumikia Yehova, wazazi ambao wamekuwa wakiwazoeza watoto wao kwa bidii wanaweza kutumaini kwamba watoto wao watarudiwa na fahamu. Kweli ya Biblia ina nguvu, na mazoezi ya wazazi hayasahauliki kwa urahisi.—Zaburi 19:7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki