HAZINA ZA NENO LA MUNGU | METHALI 22-26
“Mlee Mvulana Kulingana na Njia Inayomfaa”
Kitabu cha Methali kina mashauri yanayofaa kwa ajili ya wazazi. Kukunja matawi machanga kunasaidia sana ukuzi wake. Vivyo hivyo, kuwazoeza watoto kunawasaidia kuendelea kumtumikia Yehova hata wanapokuwa watu wazima.
Kuwazoeza watoto vizuri kunachukua muda na jitihada nyingi
Wazazi wanapaswa kuweka mfano mzuri na wanapaswa kuwa makini kuwazoeza, kuwaonya, kuwatia moyo, na kuwatia nidhamu watoto wao
Nidhamu ni mazoezi yanayotolewa kwa upendo yanayosahihisha akili na moyo
Kila mtoto anahitaji nidhamu inayomfaa yeye binafsi