Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w07 12/15 uku. 32
  • “Zawadi Yako Yenye Thamani Sana”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Zawadi Yako Yenye Thamani Sana”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
w07 12/15 uku. 32

“Zawadi Yako Yenye Thamani Sana”

HIVYO ndivyo alivyosema waziri mkuu wa zamani wa Ubelgiji kuhusu kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi.a Jirani yake alimtembelea, na waziri huyo mkuu akakubali kitabu hicho. Baadaye, aliandika barua ya shukrani: “Ziara yako ya kirafiki ilinigusa moyo, na nilivutiwa hata zaidi na zawadi yako yenye thamani sana: kile kitabu kinachozungumza kuhusu ‘Yule Mtu Mkuu Zaidi.’”

Waziri huyo mkuu wa zamani alikuwa amekichunguza kitabu hicho na kukata kauli hivi: “Kama watu wangependezwa zaidi na ujumbe wa Injili na kufuata kanuni za Yesu Kristo, ulimwengu ungekuwa tofauti sana leo. Hatungehitaji Baraza la Usalama; wala hakungekuwa na mashambulizi ya kigaidi, na jeuri ingepigwa marufuku ulimwenguni.” Ingawa alikubali kwamba hali haziwezi kuwa hivyo, alimshukuru sana jirani yake kwa sababu ya kumtembelea.

Barua hiyo iliendelea kusema hivi: “Unashikiriana na kikundi kinachostahili kusifiwa cha watu wenye nia njema ambao hawatazamii mema au mabaya tu lakini wanaamini kwamba wanadamu na pia ulimwengu unaweza kuwa bora.”

Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba Mungu ndiye atakayeleta ulimwengu bora wala si jitihada za wanadamu. Wanajitahidi kumwiga yule mtu mkuu zaidi, Yesu Kristo. Je, Mashahidi wa Yehova wamekutembelea hivi karibuni? Inaelekea utafurahia kuzungumza nao kumhusu yule mtu mkuu zaidi aliyepata kuishi. Nao watafurahi kukupa kitabu kilimchovutia sana yule waziri mkuu wa zamani.

[Maelezo ya Chini]

a Kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki