Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w09 2/1 uku. 8
  • Je, Mungu Ananijali?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Mungu Ananijali?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Watawala Katika Makao ya Roho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Kwa Nini Kuna Mateso Mengi Ulimwenguni?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Mungu Ana Kusudi Gani kwa Dunia
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Adui wa Uzima wa Milele
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
w09 2/1 uku. 8

Je, Mungu Ananijali?

Watu wengi wanajibu hivi:

▪ “Mungu ni mtu wa maana sana hivi kwamba hawezi kufikiria matatizo yangu.”

▪ “Sidhani ananijali.”

Yesu alisema nini?

▪ “Shore watano huuzwa kwa sarafu mbili za thamani ndogo, sivyo? na bado hakuna hata mmoja wao husahaulika mbele za Mungu. Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope; ninyi ni wenye thamani kuliko shore wengi.” (Luka 12:6, 7) Bila shaka, Yesu alifundisha kwamba Mungu anatujali.

▪ “Msihangaike kamwe na kusema, ‘Tutakula nini?’ au, ‘Tutakunywa nini?’ au, ‘Tutavaa nini?’ kwa maana vyote hivi ndivyo vitu ambavyo mataifa yanafuatilia kwa tamaa. kwa maana Baba yenu wa mbinguni anajua mnahitaji vitu hivi vyote.” (Mathayo 6:31, 32) Yesu alikuwa na uhakika kwamba Mungu anajua mahitaji ya kila mmoja wetu.

BIBLIA inataja waziwazi kwamba Mungu anatujali. (Zaburi 55:22; 1 Petro 5:7) Lakini ikiwa anatujali, kwa nini tunateseka sana leo? Ikiwa Mungu ni mwenye upendo na mwenye nguvu zote, kwa nini hachukui hatua yoyote ili kumaliza kuteseka?

Jibu linahusiana na jambo ambalo watu wengi hawajui, yaani, Shetani Ibilisi ndiye mtawala wa ulimwengu huu mwovu. Alipokuwa akimjaribu Yesu, Shetani alimwahidi kwamba atampa falme zote za ulimwengu, aliposema: “Hakika nitakupa mamlaka yote hii na utukufu wake, kwa sababu nimepewa, na yeyote ninayetaka mimi humpa.”—Luka 4:5-7.

Ni nani aliyemweka Shetani kuwa mtawala wa ulimwengu? Wazazi wetu wa kwanza, Adamu na Hawa, walipomtii Shetani na kumpa Mungu kisogo, ni kana kwamba walimchagua Shetani kuwa mtawala wao. Tangu uasi huo, kwa subira Yehova Mungu ameruhusu wakati upite ili athibitishe kwamba utawala wa Shetani umeshindwa kabisa. Yehova hajawalazimisha watu wamtumikie, lakini amefungua njia ili tumrudie.—Waroma 5:10.

Kwa kuwa Mungu anatujali amefanya mipango ili Yesu atukomboe kutoka kwa utawala wa Shetani. Hivi karibuni, Yesu ‘atamwangamiza yule aliye na uwezo wa kusababisha kifo, yaani, Ibilisi.’ (Waebrania 2:14) Kwa kufanya hivyo, ‘atazivunja kazi za Ibilisi.’—1 Yohana 3:8.

Dunia hii itafanywa tena kuwa Paradiso. Wakati huo, Mungu “atafuta kila chozi kutoka katika macho [ya watu], na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani [yatakuwa] yamepitilia mbali.”—Ufunuo 21:4, 5.a

[Maelezo ya chini]

a Kwa habari zaidi kuhusu kwa nini Mungu anawaacha watu wateseke, ona sura ya 11 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

[Blabu katika ukurasa wa 8]

Dunia hii itafanywa tena kuwa Paradiso

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki