Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w09 5/15 uku. 18
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Ufalme wa Mungu Wazaliwa!
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
  • Watawala Katika Makao ya Roho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Uwe Macho​—Shetani Anataka Kukumeza!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Mjue Adui Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
w09 5/15 uku. 18

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Shetani alitupwa kutoka mbinguni wakati gani?—Ufu. 12:1-9.

Ingawa kitabu cha Biblia cha Ufunuo hakitaji wakati hususa ambapo Shetani alitupwa, kinataja matukio ya mfululizo ambayo yanaweza kutusaidia kukadiria wakati ambapo alitupwa kutoka mbinguni. Tukio la kwanza kati ya matukio hayo ni kusimamishwa kwa Ufalme wa Kimasihi. Kabla ya tukio hilo, ‘vita vilitokea mbinguni,’ ambapo Shetani alishindwa na mwishowe akatupwa kutoka mbinguni.

Maandiko yanaonyesha waziwazi kwamba mwaka wa 1914 ndio mwaka ambao “nyakati zilizowekwa za mataifa” zilikoma na Ufalme ukasimamishwa.a (Luka 21:24) Vita vilivyotokea mbinguni vilianza baada ya muda gani kupita tangu hapo, ndipo Shetani akatupwa kutoka mbinguni?

Andiko la Ufunuo 12:4 linasema: “Huyo joka mkubwa [Shetani] akaendelea kusimama mbele ya yule mwanamke aliyekuwa karibu kuzaa, ili, atakapozaa, ammeze mtoto wake.” Hilo linaonyesha kwamba Shetani alitaka kuuangamiza Ufalme huo mara moja, ikiwezekana, mara tu ulipozaliwa. Ingawa Yehova aliingilia kati na kumzuia Shetani kutimiza kusudi lake ovu, Shetani aliazimia na alijitahidi sana kuuangamiza Ufalme huo uliokuwa umesimamishwa. Kwa hiyo, ni jambo linalopatana na akili kwamba “Mikaeli na malaika zake” wangechukua hatua ya haraka ya kumwondoa huyo “joka mkubwa na malaika zake” kutoka mbinguni ili Ufalme huo usipate madhara. Hilo linadokeza kwamba Shetani alishindwa na kutupwa kutoka mbinguni muda mfupi baada ya Ufalme kuzaliwa mwaka wa 1914.

Jambo lingine la kufikiria ni ufufuo wa Wakristo watiwa-mafuta, ambao kama Maandiko yanavyoonyesha, ulianza muda mfupi baada ya Ufalme kusimamishwa.b (Ufu. 20:6) Kwa kuwa Maandiko hayataji kwamba ndugu yeyote mtiwa-mafuta wa Kristo alikuwa pamoja na Yesu alipopigana na yule joka na malaika zake, vita vilivyotokea mbinguni na kutupwa kwa Shetani na roho wake waovu lazima kuwe kulikuwa kumekamilika wakati ufufuo wa ndugu za Kristo ulipoanza.

Hivyo basi, Biblia haifunui wakati hususa ambapo Shetani na roho wake waovu walitupwa kutoka mbinguni. Hata hivyo, ni wazi kwamba tukio hilo lilifuata kwa ukaribu kuwekwa kwa Yesu Kristo kuwa mfalme mbinguni mwaka wa 1914.

[Maelezo ya chini]

a Ona ukurasa wa 215-218 wa kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?

b Ona Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 2007 (1/1/2007), ukurasa wa 27-28, fungu la 9-13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki