Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w10 11/1 uku. 6
  • Dumisha Mtazamo wa Kuwa na Shukrani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Dumisha Mtazamo wa Kuwa na Shukrani
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Uonyeshe Uthamini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Mafuta
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
  • Mafuta Hutoka Wapi?
    Amkeni!—2003
  • Yehova Ni Mungu Anayethamini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
w10 11/1 uku. 6

Njia ya 3

Dumisha Mtazamo wa Kuwa na Shukrani

BIBLIA INAFUNDISHA NINI? “Kuhusiana na kila jambo toeni shukrani.”—1 Wathesalonike 5:18.

KWA NINI INAWEZA KUWA VIGUMU? Tumezungukwa na watu wenye kiburi na wasio na shukrani, na tunaweza kuanza kuwaiga. (2 Timotheo 3:1, 2) Zaidi ya hilo, tunaweza kuhisi kwamba tunasukumwa kuwa na mambo mengi zaidi ya kufanya katika maisha yetu ambayo tayari yana shughuli nyingi. Tunaweza kulemewa na matatizo au kufuatilia sana mapendezi yetu wenyewe hivi kwamba tunakosa kuthamini mambo mazuri ambayo tayari tunayo, au kuwashukuru wengine kwa mambo wanayotufanyia.

UNAWEZA KUFANYA NINI? Tenga wakati wa kutafakari mambo mazuri ambayo sasa unafurahia. Bila shaka, unaweza kuhisi kwamba umelemewa na matatizo. Lakini fikiria mfano wa Mfalme Daudi. Wakati fulani alihisi kuwa amevunjika moyo na kulemewa na majaribu. Hata hivyo, alisali kwa Mungu hivi: “Nimetafakari juu ya utendaji wako wote; kwa kupenda niliendelea kuhangaikia kazi ya mikono yako mwenyewe.” (Zaburi 143:3-5) Ingawa alipatwa na majaribu, Daudi alidumisha mtazamo wa kuwa mwenye shukrani na mwenye kuridhika.

Fikiria mambo ambayo wengine wamefanya ili kukusaidia, na uwashukuru kwa jitihada zao. Yesu aliweka kielelezo kizuri sana katika jambo hilo. Kwa mfano, wakati rafiki yake Maria alipommiminia kichwani na miguuni mafuta ya bei ya juu, watu fulani waliuliza: “Kwa nini hasara hii ya mafuta yenye marashi?”a Walalamikaji hao walihisi kwamba mafuta hayo yalipaswa kuuzwa, kisha maskini wapewe pesa hizo. Yesu aliwajibu hivi: “Mwacheni. Kwa nini mnataka kumsumbua?” Kisha akaongeza: “Amenifanyia tendo zuri.” (Marko 14:3-8; Yohana 12:3) Badala ya kukazia kile ambacho Maria hakufanya, Yesu alishukuru kwa kile alichofanya.

Watu fulani huanza kuthamini watu wa familia, marafiki, au baraka nyingine baada ya kupoteza watu hao au baraka hizo. Unaweza kuepuka hali hiyo kwa kutafakari kuhusu mambo mazuri unayofurahia sasa! Tunakutia moyo ufikirie au kuandika mambo ambayo yanakufanya uwe mwenye shukrani.

Kwa kuwa “kila zawadi njema” hutoka kwa Mungu, tunafanya vizuri kumshukuru katika sala. (Yakobo 1:17) Kufanya hivyo kila wakati, kunaweza kutusaidia kudumisha mtazamo wa kuwa wenye shukrani na wenye kuridhika.—Wafilipi 4:6, 7.

[Maelezo ya Chini]

a Katika karne ya kwanza, kumimina mafuta juu ya kichwa cha mgeni ilikuwa ishara ya kumkaribisha; kummiminia mafuta miguuni ilikuwa ishara ya unyenyekevu.

[Picha katika ukurasa wa 6]

Je, unawashukuru wengine kwa mambo wanayokufanyia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki