Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w10 11/1 uku. 5
  • Epuka Kujilinganisha na Wengine

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Epuka Kujilinganisha na Wengine
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Anataka Nini Kwetu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Yehova Anataka Nini Kwako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Jinsi Unavyoweza Kuzuia Hisia Zisizofaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Mika 6:8—“Kwenda kwa Unyenyekevu na Mungu Wako”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
w10 11/1 uku. 5

Njia ya 2

Epuka Kujilinganisha na Wengine

BIBLIA INAFUNDISHA NINI? “Fanya kazi yako vizuri, na utakuwa na jambo la kujivunia. Lakini usijilinganishe na wengine.”—Wagalatia 6:4, Contemporary English Version.

KWA NINI INAWEZA KUWA VIGUMU? Huenda tukawa na mwelekeo wa kujilinganisha na wengine—nyakati nyingine na wale wenye vitu vichache kuliko tulivyo navyo, lakini mara nyingi na wale wenye nguvu nyingi zaidi, wenye utajiri zaidi, au wenye uwezo mwingi zaidi. Vyovyote vile, matokeo huwa si mazuri. Tunajidanganya kwa kufikiri kwamba thamani ya mtu inapimwa kulingana na vitu alivyo navyo au yale anayoweza kufanya. Huenda pia tukachochea hisia za wivu na roho ya mashindano.—Mhubiri 4:4.

UNAWEZA KUFANYA NINI? Jaribu kujiona kama vile Mungu anavyokuona. Ruhusu maoni yake yaongoze jinsi unavyojiona. “Mwanadamu huona kile kinachoonekana kwa macho, lakini Yehovaa huona jinsi moyo ulivyo.” (1 Samweli 16:7) Yehova anapima thamani yako si kwa kukulinganisha na mtu mwingine, bali kwa kusoma moyo wako, na kwa kuchunguza mawazo, hisia, na nia yako. (Waebrania 4:12, 13) Anaelewa udhaifu wako na angependa wewe pia utambue hali hiyo. Ikiwa unapima thamani yako kwa kujilinganisha na wengine, utaishia ama kuwa na majivuno au kukosa uradhi sikuzote. Hivyo, uwe mnyenyekevu na ukubali kwamba huwezi kufanikiwa katika kila jambo.—Methali 11:2.

Unapaswa kufanya nini hasa ili uwe na thamani machoni pa Mungu? Mungu alimwongoza nabii Mika kuandika hivi: “Ee mtu wa udongo, yeye amekuambia yaliyo mema. Na Yehova anataka nini kutoka kwako ila kutenda haki na kupenda fadhili na kuwa na kiasi katika kutembea na Mungu wako?” (Mika 6:8) Ikiwa utafuata shauri hilo, Mungu atakutunza. (1 Petro 5:6, 7) Bila shaka, hiyo ni sababu kubwa sana ya kutufanya turidhike.

[Maelezo ya Chini]

a Jina la Mungu kama linavyopatikana katika Biblia.

[Picha katika ukurasa wa 5]

Yehova anapima thamani yetu kwa jinsi tulivyo moyoni

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki