Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w10 12/1 uku. 11
  • Anajua “Moyo wa Wanadamu”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Anajua “Moyo wa Wanadamu”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Sulemani Atawala kwa Hekima
    Biblia—Ina Ujumbe Gani?
  • Je, Yeye Ni Mfano Mzuri au Ni Onyo Kwako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • “Ataacha Umpate”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Sulemani Anajenga Hekalu
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
w10 12/1 uku. 11

Mkaribie Mungu

Anajua “Moyo wa Wanadamu”

2 MAMBO YA NYAKATI 6:29, 30

NI NANI ambaye hajawahi kulemewa na hali ngumu na matatizo ya maisha? Nyakati nyingine huenda ikaonekana kwamba hakuna mtu anayeweza kuelewa kikweli mahangaiko tunayokabili au maumivu tunayohisi. Hata hivyo, kuna yule anayeelewa kwa ukamili jinsi tunavyohisi—Yehova Mungu. Tunaweza kufarijiwa na maneno ya Sulemani, yanayopatikana katika 2 Mambo ya Nyakati 6:29, 30.

Sulemani anatoa sala katika uzinduzi wa hekalu huko Yerusalemu mwaka wa 1026 K.W.K. Katika sala yake ambayo huenda ilichukua dakika kumi hivi, Sulemani anamsihi Yehova Mungu wa ushikamanifu, Mtimizaji wa ahadi, na Msikiaji wa sala.—1 Wafalme 8:23-53; 2 Mambo ya Nyakati 6:14-42.

Sulemani anamsihi Mungu asikilize maombi ya waabudu wake. (Mstari wa 29) Ingawa Sulemani anaorodhesha matatizo mengi (mstari wa 28), anagundua kwamba kila mwabudu anajua “pigo lake” na kuhisi “maumivu yake mwenyewe.” Huenda mtu fulani akahuzunishwa na jambo fulani hali mwingine anabeba mzigo mwingine tofauti kabisa.

Hata hali iwe namna gani, watu wenye kumhofu Mungu hawahitaji kubeba mizigo yao peke yao. Katika sala yake, Sulemani anamfikiria mwabudu fulani ambaye huenda akasukumwa ‘kunyoosha mikono yake,’ anapomkaribia Yehova katika sala ya kutoka moyoni.a Labda Sulemani anakumbuka kwamba Daudi baba yake alipokuwa na mahangaiko mengi, alisema hivi: “Mtupie Yehova mzigo wako.”—Zaburi 55:4, 22.

Yehova ataitikia jinsi gani sala za unyofu za kuomba msaada? Sulemani anamsihi Yehova hivi: “Na usikie ukiwa mbinguni, makao yako, nawe usamehe na kumpa kila mmoja kulingana na njia zake zote.” (Mstari wa 30) Sulemani anajua kwamba “Msikiaji wa sala” anawajali waabudu wake si wakiwa kikundi tu, bali pia wakiwa mtu mmoja-mmoja. (Zaburi 65:2) Yehova hutoa msaada unaohitajika, kutia ndani kumsamehe mtenda-dhambi anayemrudia kwa moyo wake wote.—2 Mambo ya Nyakati 6:36-39.

Kwa nini Sulemani ana hakika kwamba Yehova atasikiliza sala za mwabudu anayetubu? Akiendelea na sala yake, Sulemani anasema: “Kwa sababu [Yehova] unaujua moyo wake (kwa maana ni wewe peke yako unayejua vema moyo wa wanadamu wote).” Yehova anajua pigo au maumivu ambayo kila mwabudu wake mwaminifu anabeba katika moyo wake, na Anajali mahangaiko yake.—Zaburi 37:4.

Tunaweza kufarijiwa na sala ya Sulemani. Huenda wanadamu wenzetu wasielewe hisia zetu za ndani—‘pigo letu’ na ‘maumivu yetu’ wenyewe. (Methali 14:10) Lakini Yehova anaujua moyo wetu, na anatujali sana. Kumweleza hisia zetu za moyoni kupitia sala, kunaweza kufanya mizigo yetu iwe rahisi kubeba. Biblia inasema: ‘Tupeni mahangaiko yenu yote juu yake, kwa sababu yeye anawajali ninyi.’—1 Petro 5:7.

[Maelezo ya Chini]

a Katika nyakati za Biblia, ‘unyooshaji wa mikono,’ viganja vikielekea juu, ulikuwa ishara ya sala.—2 Mambo ya Nyakati 6:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki