Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w11 7/1 kur. 30-31
  • Jinsi ya Kukataa Kishawishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kukataa Kishawishi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari Zinazolingana
  • Ashtakiwa kwa Uwongo!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Uharibifu wa Sodoma na Gomora
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Yesu Ashinda Vishawishi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Yesu Awashangaza Wasikilizaji Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
w11 7/1 kur. 30-31

Kwa Ajili ya Vijana

Jinsi ya Kukataa Kishawishi

YOSEFU—SEHEMU YA 1

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wakuu wanavyohisi. Wazia kwamba masimulizi haya ni halisi kabisa.

Wahusika wakuu: Yosefu na mke wa Potifa

Muhtasari: Yosefu akataa kishawishi cha kufanya ngono na mke wa Potifa.

1 CHUNGUZA TUKIO HILI.​—SOMA MWANZO 39:1-12.

Eleza ukubwa wa nyumba ya kifahari ya Potifa kama unavyoiwazia.

․․․․․

Unafikiri Yosefu alikuwa na sura ya aina gani? (Dokezo: Soma tena mstari wa 6.)

․․․․․

Unatambua hisia gani katika sauti ya Yosefu anapozungumza na mke wa Potifa katika mstari wa 8 na 9?

․․․․․

2 CHIMBA ZAIDI.

Ni nini ambacho kingeweza kufanya Yosefu ashawishike kulegeza msimamo wake kuhusu maadili mema? (Dokezo: Soma Wafilipi 2:12 na ufikirie hali za Yosefu. Kwa mfano, wakati huo watu wa familia yake na waabudu wengine wa Yehova walikuwa wapi?)

․․․․․

Unafikiri ni kwa nini Yosefu aliona kwamba ni dhambi mbele za Mungu kufanya ngono na mke wa Potifa ingawa wakati huo Mungu hakuwa ametoa sheria iliyokataza uzinzi? (Dokezo: Soma na utafakari kuhusu maandiko yanayofuata: Mwanzo 2:24; 12:17, 18; Waroma 2:14, 15; na Waebrania 5:14.)

․․․․․

3 TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Uhusiano kati ya kujizuia na kujiheshimu.

․․․․․

Manufaa ambayo wale wanaofuata viwango vya Mungu kuhusu maadili wanapata.

․․․․․

Uhitaji wa kuzoeza ‘nguvu zako za ufahamu.’ (Waebrania 5:14)

․․․․․

NJIA NYINGINE UNAYOWEZA KUTUMIA MAMBO HAYO.

Ni katika hali gani maishani unapoweza kufanya uamuzi thabiti wa kukataa kishawishi cha kufanya ngono? (Dokezo: Soma na utafakari kuhusu Ayubu 31:1; Zaburi 119:37; Waefeso 5:3, 4.)

․․․․․

4 NI MAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI AMBAYO YAMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․

Ikiwa huna Biblia, waombe Mashahidi wa Yehova wakupe moja, au soma habari zaidi katika Intaneti kwenye www.watchtower.org

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki