Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w12 6/1 uku. 9
  • “Uzima wa Milele Ndio Huu”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Uzima wa Milele Ndio Huu”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Kupata Ujuzi Sasa na Milele
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • “Hii Yamaanisha Uhai Udumuo Milele”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Ujuzi Kutoka kwa Mungu Hujibu Maswali Mengi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Rudia Wale Walioonyesha Kupendezwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 6/1 uku. 9

“Uzima wa Milele Ndio Huu”

“Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.”—YOHANA 17:3.

UJUZI unaweza kuokoa uhai. Nouhou mwenye umri wa miezi kumi alipougua, mama yake, ambaye ni mhudumu wa afya nchini Niger, alijua hatua aliyopaswa kuchukua. Alimtayarishia mwana wake kinywaji kwa kuchanganya maji safi, sukari, na chumvi. Kulingana na Hazina ya Watoto ya Umoja wa Mataifa (UNICEF), kwa sababu ya “hatua hiyo ya haraka aliyochukua, mtoto wake alipona mara moja.”

Pia, ujuzi wa Biblia unaweza kuokoa uhai wa watu. Musa, mwandikaji wa kwanza wa Biblia, alisema hivi: “Si neno lisilo na thamani kwenu, bali linamaanisha uhai wenu, na kwa neno hili mnaweza kurefusha siku zenu.” (Kumbukumbu la Torati 32:47) Je, kweli Biblia inaweza kurefusha siku zetu? Inawezaje kumaanisha uhai kwetu?

Makala tano zilizotangulia katika mfululizo huu zimeonyesha kwamba Biblia ni kitabu ambacho hakiwezi kufananishwa na kitabu kingine chochote kwa sababu ya unabii wenye kutegemeka, usahihi wa kihistoria na kisayansi, upatano wa vitabu vyake, na mwongozo unaofaa. Mambo hayo yanathibitisha kwamba Biblia ni kitabu cha kipekee. Hivyo basi, Biblia inapotaja kwamba inaweza kukuelekeza katika njia ya kupata maisha marefu, yaani, uzima wa milele, je, hupaswi kuichunguza kwa makini?

Tunakutia moyo ujifunze jinsi ujuzi sahihi wa Biblia unavyoweza kufanya uwe na amani ya akili sasa na furaha ya kudumu wakati ujao. Mashahidi wa Yehova watafurahia kukuonyesha jinsi unavyoweza kupata ujuzi huo sahihi.

[Sanduku/​Picha katika ukurasa wa 9]

Biblia ni kitabu cha kipekee kwa sababu hakuna kitabu kingine kinachotoa majibu yenye kuridhisha kwa maswali muhimu tunayojiuliza kama vile:

• Ni nini kusudi la maisha?

• Kwa nini wanadamu wanateseka sana?

• Je, kuna tumaini kwa wapendwa wangu waliokufa?

Unaweza kupata majibu yanayotegemea Biblia katika kitabu hiki, Biblia Inafundisha Nini Hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki