Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 7/1 uku. 4
  • Je, Dini Inategemeka Kuhusiana na Pesa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Dini Inategemeka Kuhusiana na Pesa?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • BIBLIA INAFUNDISHA NINI?
  • MASHAHIDI WA YEHOVA WANAFANYAJE?
  • Maoni Yenye Usawaziko Kuhusu Pesa
    Amkeni!—2015
  • Kupanga Matumizi ya Pesa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Jinsi Kazi za Ufalme Zinavyogharimiwa
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Pesa
    Amkeni!—2014
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 7/1 uku. 4
[Picha katika ukurasa wa 4]

Je, Dini Inategemeka Kuhusiana na Pesa?

Estellea alikuwa akienda kanisani kwa ukawaida pamoja na watoto wake. Anasema hivi: “Nilimwambia mchungaji kwamba nilitaka kujifunza Biblia.” Lakini hakuwahi kumfundisha. Mwishowe akaacha kwenda kanisani. Anaendelea kusema: “Viongozi wa kanisa waliniandikia barua na kusema ikiwa nisingeenda kanisani basi nitume pesa. Nilijiambia, ‘Hawajali kama nitaenda kanisani au la, wanachotaka tu ni pesa.’”

Angelina ambaye sikuzote amekuwa mfuasi wa dini anasema: “Kanisani kwetu kikapu kilipitishwa mara tatu kila kipindi cha ibada, na tulipaswa kutoa sadaka mara zote. Walikuwa wakiomba pesa sikuzote. Nikajiambia, ‘Hawana roho ya Mungu.’”

Je, dini katika eneo lenu huomba pesa moja kwa moja au kwa njia zisizo za wazi? Je, hilo linapatana na Biblia?

BIBLIA INAFUNDISHA NINI?

Yesu, mwanzilishi wa Ukristo, alisema: “Mlipokea bure, toeni bure.” (Mathayo 10:8) Ujumbe wa Biblia haupaswi kuuzwa na unapaswa kupatikana kwa kila mtu anayetaka.

Wakristo wa mapema walipataje pesa za kutegemeza ibada?

Kila mmoja alitoa mchango “kama alivyoazimia moyoni mwake, si kwa kutopenda wala kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda mtoaji mchangamfu.” (2 Wakorintho 9:7) Mtume Paulo alisema: “Ilikuwa kwa kufanya kazi usiku na mchana, ili tusimtwike yeyote kati yenu mzigo wenye gharama, kwamba tuliwahubiria ninyi habari njema.” (1 Wathesalonike 2:9) Paulo alifanya kazi ya kutengeneza mahema ili kutegemeza huduma yake.​—Matendo 18:2, 3.

MASHAHIDI WA YEHOVA WANAFANYAJE?

Kwa kawaida, Mashahidi wa Yehova hukutana katika majengo yanayoitwa Majumba ya Ufalme. Wanapataje pesa za kulipia gharama? Hawapitishi sahani za michango wakati wa ibada, wala kutoa bahasha za kuomba michango. Badala yake, mtu yeyote anaweza kuweka mchango kwenye sanduku la michango katika Jumba la Ufalme.

Shughuli za kidini zinapaswa kugharimiwaje?

Bila shaka, pesa zinahitajika ili kuchapisha na kusafirisha gazeti hili. Hata hivyo, hutaona matangazo yoyote ya kibiashara au ya kuomba pesa. Jambo linalokaziwa ni kutangaza ujumbe wa Biblia.

Je, kufanya hivyo kunapatana na maneno ya Yesu pamoja na mfano wa Wakristo wa mapema?

a Baadhi ya majina katika makala hizi yamebadilishwa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki