Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 10/1 uku. 7
  • Habari Njema kwa Watu Wote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Habari Njema kwa Watu Wote
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Tovuti Yetu Rasmi—Imetengenezwa ili Itunufaishe Sisi na Wengine
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Ukristo wa Kweli Washinda!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Ni Nani Watakaoenda Mbinguni​—Je, Ni Watu Wote Wazuri?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Sikia Ambacho Roho Husema kwa Makundi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 10/1 uku. 7
[Picha katika ukurasa wa 7]

HABARI KUU | BIBLIA INA UJUMBE GANI?

Habari Njema kwa Watu Wote

Ufufuo wa Yesu uliimarisha imani ya wanafunzi wake na kufanya wawe na bidii. Kwa mfano mtume Paulo alisafiri kotekote katika eneo la Asia Ndogo na Mediterania, akipanga makutaniko na kuwaimarisha Wakristo ili wakabiliane na majaribu na upinzani mkali. Licha ya matatizo hayo, idadi ya Wakristo ilizidi kuongezeka.

Baadaye, mtume Paulo alifungwa gerezani. Hata akiwa huko aliandikia makutaniko ya Wakristo barua ili kuwashauri na kuwatia moyo. Aliwaonya kuhusu hatari kubwa zaidi, yaani, uasi-imani. Akiongozwa na roho takatifu ya Mungu Paulo alitabiri kwamba “mbwa mwitu wenye kukandamiza” wanaosema “mambo yaliyopotoka” wangeingia miongoni mwao na “kuwavuta wanafunzi wawafuate wao wenyewe.”​—Matendo 20:29, 30.

Kufikia mwishoni mwa karne ya kwanza, uasi-imani huo ulikuwa umeanza. Karibu na kipindi hicho, Yesu aliyefufuliwa alimpa mtume Yohana Ufunuo, yaani, maono kuhusu wakati ujao. Kama Yohana alivyoandika, wapinzani na walimu wa uwongo hawatamzuia Mungu kutimiza kikamili kusudi lake la awali kwa ajili ya dunia na wanadamu. Watu kutoka “kila taifa na kabila na lugha” watatangaziwa habari njema za Ufalme wa Mungu. (Ufunuo 14:6) Paradiso itarudishwa duniani, na kila mtu anayefanya mapenzi ya Mungu ataishi humo!

Una maoni gani, je, hizo ni “habari njema”? Ikiwa ndivyo, basi soma mengi kuhusu ujumbe wa Mungu kwa wanadamu unaopatikana katika Biblia na uone jinsi unavyoweza kukunufaisha sasa na wakati ujao.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Unaweza kusoma Biblia kwenye Intaneti ukitumia anwani ya www.jw.org/sw. Katika Tovuti hiyo, unaweza pia kusoma broshua Biblia​—Ina Ujumbe Gani? na Habari Njema Kutoka kwa Mungu! na kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? pamoja na machapisho mengine yanayozungumzia kwa nini tunaweza kuiamini Biblia na jinsi tunavyoweza kutumia ushauri wake katika familia na maisha yetu. Au umwombe Shahidi yeyote wa Yehova akupe habari zaidi.

​—Habari hii inategemea Matendo, Waefeso, Wafilipi, Wakolosai, Filemoni, 1 Yohana, Ufunuo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki