Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 11/1 uku. 6
  • Uwongo Unaomfanya Mungu Aonekane Kuwa Mkatili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwongo Unaomfanya Mungu Aonekane Kuwa Mkatili
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Moto wa Mateso Ni Halisi? Kuzimu Ni Wapi Kulingana na Biblia?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Hadithi ya Pili ya Uwongo: Waovu Wanateseka Katika Moto wa Mateso
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Ni Nani Wanaoenda Kuzimu?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Je, Kweli Kuna Mahali Penye Moto wa Mateso?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 11/1 uku. 6

HABARI KUU | UWONGO UNAOFANYA WATU WASIMPENDE MUNGU

Uwongo Unaomfanya Mungu Aonekane Kuwa Mkatili

MAONI YA WATU WENGI

“Punde tu baada ya kifo nafsi za watu wanaokufa wakiwa watenda dhambi zinaenda motoni, ambako zinateseka milele.” (Catechism of the Catholic Church) Baadhi ya viongozi wa kidini wanasema kwamba mtu akifa anatengwa kabisa na Mungu.

UKWELI WA BIBLIA

“Nafsi inayotenda dhambi​—hiyo yenyewe itakufa.” (Ezekieli 18:4) Wafu “hawajui lolote kamwe.” (Mhubiri 9:5) Ikiwa nafsi inayokufa haijui lolote inawezaje kuteseka kwenye “moto wa mateso”?

Katika Biblia neno ambalo hutafsiriwa “kuzimu” kihalisi linarejelea kaburi la watu wote. Kwa mfano, Ayubu alipopatwa na ugonjwa mbaya sana, alisali hivi: “Laiti ungenificha kuzimuni.” (Ayubu 14:13, Biblia Habari Njema) Ayubu alitaka kupumzika kaburini na si mahali penye mateso.

KWA NINI NI MUHIMU?

Ikiwa Mungu ni mkatili hatuwezi kumpenda, tutamchukia. “Tangu nikiwa mtoto nilifundishwa kuhusu moto wa mateso,” anasema Rocío, anayeishi Mexico. “Niliogopa sana na kudhani Mungu ni mkatili. Nilifikiri kwamba alikuwa mwenye hasira na asiye na upendo.”

Rocío alibadili maoni yake kumwelekea Mungu aliposoma katika Biblia kuhusu hukumu za Mungu na hali ya wafu. Anasema, “Nilijihisi huru​—ni kama nilikuwa nimeondolewa mzigo mkubwa wa kihisia. Nilianza kuamini kwamba Mungu anataka tufanikiwe, anatupenda, na ninaweza kumpenda. Yeye ni kama baba anayewapenda na kuwajali watoto wake.”​—Isaya 41:13.

Watu wengi wamejitahidi kumcha Mungu kwa sababu wanaogopa kuteswa motoni, hata hivyo, Mungu hataki umtumikie kwa sababu unamwogopa. Badala yake, Yesu alisema hivi: “Lazima umpende Yehova Mungu wako.” (Marko 12:29, 30) Zaidi ya hayo, tukiwa na uhakika kwamba Mungu anatenda kwa haki sasa, tunaweza kutazamia kwamba atahukumu kwa haki wakati ujao. Kama Elihu, rafiki ya Ayubu, tunaweza kusema: “Hasha, Mungu wa kweli asitende kwa uovu, na Mweza-Yote kutenda isivyo haki!”​—Ayubu 34:10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki