Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 11/1 uku. 5
  • Uwongo Unaomfanya Mungu Asieleweke

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwongo Unaomfanya Mungu Asieleweke
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Utatu Hufafanuliwaje?
    Je, Uamini Utatu?
  • Ule “Utatu Uliobarikiwa”—je! Umo Katika Biblia?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Sehemu ya 1—Je! Yesu na Wanafunzi Wake Walifundisha Fundisho la Utatu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Yesu Kristo Mwana Mpendwa wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 11/1 uku. 5

HABARI KUU | UWONGO UNAOFANYA WATU WASIMPENDE MUNGU

Uwongo Unaomfanya Mungu Asieleweke

MAONI YA WATU WENGI

“Wakatoliki, Kanisa Othodoksi la Mashariki, na Waprotestanti huamini Utatu, yaani Mungu mmoja katika nafsi tatu: Mungu Baba, Mungu Mwana, na Mungu Roho Mtakatifu. Kulingana na fundisho la Ukristo, si kwamba hao ni miungu watatu badala yake ni nafsi tatu katika mungu mmoja.”​—The New Encyclopædia Britannica.

UKWELI WA BIBLIA

Yesu, Mwana wa Mungu, hakuwahi kamwe kusema kwamba yeye na Baba yake wako sawa au kwamba ni mtu yuleyule. Badala yake, alisema hivi: “Ninaenda kwa Baba, kwa sababu Baba ni mkuu kuliko mimi.” (Yohana 14:28) Hata alimwambia hivi mmoja wa wanafunzi wake: “Mimi ninapanda kwenda kwa Baba yangu na Baba yenu na kwa Mungu wangu na Mungu wenu.”​—Yohana 20:17.

Roho takatifu si mtu. Wakristo wa karne ya kwanza ‘walijazwa roho takatifu,’ na Yehova alisema hivi: “Nitaimimina sehemu ya roho yangu juu ya kila namna ya mwili.” (Matendo 2:1-4, 17) Roho takatifu si sehemu ya Utatu. Ni nguvu ya utendaji ya Mungu.

KWA NINI NI MUHIMU?

Kulingana na wasomi wa Kikatoliki Karl Rahner na Herbert Vorgrimler, fundisho la Utatu “haliwezi kueleweka hadi mtu apate ufunuo, na hata akiupata hawezi kuuelewa Utatu kikamili.” Je, unaweza kumpenda mtu ambaye huwezi kumjua au kumwelewa? Hiyo ndiyo sababu fundisho la Utatu huzuia mtu kumjua Mungu na kumpenda.

Marco, aliyetajwa katika makala ya kwanza hakuelewa fundisho la Utatu. Alisema,“Nilifikiri kwamba Mungu hakutaka nimjue na hilo lilinifanya nimwone Mungu kuwa asiyejali na asiyeeleweka.” Hata hivyo, “Mungu si Mungu wa machafuko.” (1 Wakorintho 14:33) Mungu anataka tumjue. Yesu alisema hivi: “Sisi tunaabudu tunachokijua.”​—Yohana 4:22.

Marco anasema hivi: “Nilipojifunza kwamba Mungu si sehemu ya Utatu, ndipo nilipoweza kuanzisha urafiki na Mungu.” Tukimwona Mungu kuwa halisi badala ya kufikiri Yeye ni fumbo lisiloeleweka, ni rahisi kumpenda. Biblia inasema hivi: “Yeye ambaye hapendi hajamjua Mungu, kwa sababu Mungu ni upendo.”​—1 Yohana 4:8.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki