Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 12/1 uku. 4
  • Je, Unalijua na Kulitumia Jina la Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Unalijua na Kulitumia Jina la Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Jina la Mungu
    Amkeni!—2017
  • Kwa Nini Tunapaswa Kutumia Jina la Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Mungu Anaitwa Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
  • Kwa Nini Ni Lazima Tujue Jina la Mungu
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 12/1 uku. 4
Wanaume wawili wakiulizana majina

HABARI KUU | UNAWEZA KUMKARIBIA MUNGU

Je, Unalijua na Kulitumia Jina la Mungu?

Je, una rafiki ambaye hujui jina lake? Bila shaka hapana. Irina, mwanamke kutoka Bulgaria anasema, “Huwezi kuwa rafiki ya Mungu ikiwa hujui jina lake.” Kama ilivyotajwa kwenye makala iliyotangulia, inafurahisha kwamba Mungu anataka uwe rafiki yake. Hiyo ndiyo sababu katika Biblia, amejitambulisha kwako kwa maneno haya: “Mimi ni Yehova. Hilo ni jina langu.”—Isaya 42:8.

Kwenye Biblia, Mungu amejitambulisha kwako kwa maneno haya: “Mimi ni Yehova. Hilo ni jina langu.”—Isaya 42:8

Je, kweli Yehova anataka ujue na kulitumia jina lake? Fikiria jambo hili: Jina la Mungu, linaloandikwa kwa herufi nne za Kiebrania zinazojulikana kama Tetragramatoni, linapatikana katika maandishi ya awali ya Maandiko ya Kiebrania mara 7,000 hivi. Hakuna jina lingine lolote katika Biblia linalotajwa mara nyingi kadiri hiyo. Bila shaka hilo linatuthibitishia kwamba Yehova anataka tulijue na kulitumia jina lake.a

Kwa kawaida, ukitaka mtu awe rafiki yako, mnaanza kwa kujuana majina. Je, unalijua jina la Mungu?

Hata hivyo, baadhi ya watu wanahisi kwamba kwa sababu Mungu ni mtakatifu na mweza-yote, ni ukosefu wa heshima kutumia jina lake. Ni wazi kwamba haifai kutumia jina la Mungu katika njia isiyofaa, kama vile tu isivyofaa kutumia vibaya jina la rafiki yako mpendwa. Hata hivyo, ni mapenzi ya Yehova kwamba watu wanaompenda waliheshimu na kulitangaza jina lake. (Zaburi 69:30, 31; 96:2, 8) Kumbuka kwamba Yesu aliwafundisha wafuasi wake kusali hivi: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe.” Tunaweza kushiriki kulitakasa jina la Mungu kwa kuwaambia wengine kuhusu jina hilo. Kufanya hivyo kutatufanya tumkaribie.—Mathayo 6:9.

Biblia inaonyesha kwamba Mungu huwakazia fikira “wale wanaolifikiria jina lake.” (Malaki 3:16) Kuhusu mtu wa namna hiyo, Yehova anaahidi hivi: “Nitamlinda kwa sababu amelijua jina langu. Ataniitia, nami nitamjibu. Nitakuwa pamoja naye katika taabu.” (Zaburi 91:14, 15) Kujua na kutumia jina la Mungu, Yehova, ni muhimu ikiwa tunataka kufurahia uhusiano mzuri pamoja naye.

a Kwa kusikitisha, tafsiri nyingi za Biblia hazina jina la Mungu, licha ya kwamba linapatikana mara nyingi kwenye Maandiko ya Kiebrania yanayojulikana kama Agano la Kale. Badala yake jina la Mungu limeondolewa na mahali pake pakachukuliwa na majina ya cheo kama vile Bwana au Mungu. Kwa habari zaidi kuhusu jina la Mungu, ona ukurasa wa 195-197 kwenye kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki