Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 9/1 uku. 7
  • Kwa Nini Tunahubiri?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Tunahubiri?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Msaada Zaidi Kwa Ajili ya Familia
    Amkeni!—2018
  • Tutapata Wapi Majibu ya Maswali Muhimu Maishani?
    Tutapata Wapi Majibu ya Maswali Muhimu Maishani?
  • Kupata Msaada wa Kuielewa Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma​—Kutumia JW.ORG
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2018
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 9/1 uku. 7
Mashahidi wa Yehova wawili wakihubiri kwenye maeneo ya makazi ya watu

HABARI KUU | MASHAHIDI WA YEHOVA NI NANI?

Kwa nini tunahubiri?

Tunatambuliwa sana kutokana na kazi yetu ya kuhubiri inayofanywa ulimwenguni pote katika nyumba za watu, hadharani, na popote ambapo watu wanapatikana. Kwa nini tunahubiri?

Mashahidi wa Yehova wanahubiri ili kumtukuza Mungu na kuwaambia watu jina lake. (Waebrania 13:15) Pia, tunamtii Kristo Yesu aliyeagiza hivi: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, . . . na kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.”—Mathayo 28:19, 20.

Zaidi ya hilo, tunahubiri kwa sababu tunawapenda jirani zetu. (Mathayo 22:39) Tunajua kwamba watu wengi wana imani zao na kwamba si kila mtu anapenda ujumbe wetu. Hata hivyo, tunaamini kwamba mafundisho ya Biblia yanaokoa uhai. Ndio maana tunaendelea “bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema juu ya Kristo,” kama walivyofanya Wakristo wa karne ya kwanza.—Matendo 5:41, 42.

Mtaalamu wa elimu ya jamii, Antonio Cova Maduro aliandika kuhusu “jitihada nyingi sana ambazo Mashahidi wa Yehova wanafanya . . . , ili neno takatifu lifike maeneo ya mbali zaidi duniani.”—Gazeti la Venezuela linaloitwa El Universal

Wasomaji wengi wa machapisho yetu si Mashahidi wa Yehova. Na watu wengi tunaowafundisha Biblia ni waumini wa dini nyingine. Hata hivyo, wanathamini Mashahidi wa Yehova wanapowatembelea.

Bila shaka, huenda ukawa na maswali mengine kuhusu Mashahidi wa Yehova. Tunakutia moyo utafute majibu ya maswali hayo kwa

  • Kumuuliza Shahidi wa Yehova.

  • Kutembelea tovuti yetu ya www.jw.org/sw.

  • Kuhudhuria mikutano yetu ambayo haina kiingilio na kila mtu anaalikwa.

Yesu akiwatuma wanafunzi wake wawili wakahubiri
mlima-wenye-theluji

Kwa habari zaidi kuhusu Mashahidi wa Yehova, tazama video yenye kichwa Mashahidi wa Yehova—Tengenezo Linalohubiri Habari Njema, katika www.jw.org/sw. (Tafuta kwenye MACHAPISHO > VIDEO)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki