Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 12/1 uku. 3
  • Kwa Nini Uielewe Biblia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Uielewe Biblia?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kitabu Kinachoeleweka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Wasaidie Wale Ambao kwa Sasa Hawako Tayari Kujifunza Kitabu Biblia Inafundisha
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Mafundisho ya Kweli Yanayompendeza Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 12/1 uku. 3

HABARI KUU | UNAWEZA KUIELEWA BIBLIA

Kwa Nini Uielewe Biblia?

“Biblia ni kitabu cha dini kinachojulikana sana. Hata hivyo, ni kitabu cha kigeni na hakiwafai Wachina.”—LIN, CHINA.

“Hata vitabu vitakatifu vya dini yangu ya Kihindu sivielewi. Nitawezaje kuielewa Biblia Takatifu?” —AMIT, INDIA.

“Ninaiheshimu Biblia kwa kuwa ni kitabu cha zamani na nimesikia kwamba kimeuzwa zaidi kuliko vitabu vingine. Lakini, sijawahi kuiona.”—YUMIKO, JAPANI.

Watu wengi ulimwenguni wanaiheshimu sana Biblia. Hata hivyo, wengi wao hawajui yaliyomo katika Biblia. Hali iko hivyo kwa mamilioni ya watu wanaoishi barani Asia na hata katika nchi nyingi ambazo watu wengi wana Biblia.

Mwanamke akisoma Biblia

Huenda ukajiuliza hivi, ‘Kwa nini ninahitaji kuielewa Biblia?’ Kujifunza kuhusu kitabu hicho kitakatifu kunaweza kukusaidia:

  • Uridhike na uwe na furaha

  • Ushughulikie matatizo ya familia

  • Ukabiliane na mahangaiko

  • Uwe na uhusiano mzuri na watu

  • Utumie pesa kwa hekima

Mfikirie Yoshiko, anayeishi Japani. Alitaka sana kujua Biblia ina ujumbe gani, hivyo akaanza kuisoma. Matokeo yalikuwa nini? Anasema hivi: “Biblia imenisaidia kupata kusudi maishani na tumaini la wakati ujao. Sasa nimeridhika.” Amit aliyetajwa mwanzoni aliamua pia kuichunguza Biblia. Anasema: “Nilishangaa. Biblia ina habari zinazomfaa kila mtu.”

Biblia imeboresha sana maisha ya watu wengi. Kwa nini usiichunguze uone jinsi inavyoweza kukunufaisha?

Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha

Kwa habari zaidi kuhusu jinsi unavyoweza kunufaika kwa kusoma Biblia, tazama broshua Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha, iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki