Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 12/1 kur. 4-5
  • Kitabu Kinachoeleweka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kitabu Kinachoeleweka
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KITABU KINACHOELEWEKA
  • KINAPATIKANA KWA WOTE
  • Je! Kweli Biblia Ilitoka kwa Mungu?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Biblia Ni Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Kwa Nini Upendezwe na Ujumbe wa Biblia?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Unaweza Kupata Wapi Uongozi?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 12/1 kur. 4-5
Reading the Bible in printed form and on a mobile phone

HABARI KUU | UNAWEZA KUIELEWA BIBLIA

Kitabu Kinachoeleweka

Kwa kweli, Biblia ni kitabu cha kale. Kina umri gani? Biblia ilianza kuandikwa miaka 3,500 hivi iliyopita huko Mashariki ya Kati. Kipindi hicho utawala wenye nguvu wa ukoo wa Shang ulikuwa ukitawala nchini China na karne kumi hivi baadaye dini ya Budha ilianza nchini India. —Tazama sanduku “Taarifa Fupi Kuhusu Biblia.”

Biblia inatoa majibu yenye kuridhisha ya maswali muhimu sana kuhusu maisha

Ili kitabu kiwanufaishe na kuwasaidia watu, lazima kieleweke na kuwafaa. Ndivyo ilivyo Biblia. Inatoa majibu yenye kuridhisha ya maswali muhimu sana kuhusu maisha.

Kwa mfano, umewahi kujiuliza, ‘Kwa nini tuliumbwa?’ Swali hilo limewasumbua wanadamu kwa maelfu ya miaka, na bado linawasumbua. Hata hivyo, jibu la swali hilo linaweza kupatikana katika sura mbili za kwanza za kitabu cha kwanza cha Biblia, kitabu cha Mwanzo. Simulizi la Biblia katika sura hizo linaanza na “mwanzo,” yaani, mabilioni ya miaka iliyopita, wakati ulimwengu wetu unaotia ndani nyota na dunia ulipoumbwa. (Mwanzo 1:1) Kisha simulizi hilo linaeleza hatua kwa hatua jinsi dunia, viumbe mbalimbali, na wanadamu walivyoumbwa na pia kwa nini vitu hivyo vimeumbwa.

KITABU KINACHOELEWEKA

Biblia inatoa ushauri unaotusaidia kutatua matatizo ya kila siku. Ushauri huo unaeleweka kwa urahisi. Kuna mambo mawili yanayofanya ushauri wa Biblia ueleweke.

Kwanza, lugha ya Biblia iko wazi na inavutia. Badala ya kutumia maneno mengi yasiyoeleweka au magumu, Biblia hutumia maneno tunayoelewa. Mawazo magumu yanasimuliwa kwa maneno tunayotumia kila siku.

Kwa mfano, Yesu alifundisha mambo yaliyogusa mioyo ya watu kwa kuwasimulia mifano mingi rahisi iliyohusu mambo ya kawaida maishani. Baadhi ya mifano hiyo inapatikana katika Mahubiri ya Mlimani, yaliyoandikwa kwenye kitabu cha Biblia cha Mathayo, sura ya 5 hadi 7. Mchambuzi mmoja wa Biblia aliyeita mahubiri hayo “masomo yanayofaa,” alisema kwamba lengo lake “si kujaza habari nyingi akilini mwetu, bali kutuongoza na kutusaidia kutenda ifaavyo.” Huenda utatumia dakika 15 mpaka 20 ukisoma sura hizo, hata hivyo utashangaa jinsi maneno ya Yesu yalivyo rahisi kueleweka na yenye nguvu.

Sababu nyingine inayofanya Biblia iwe rahisi kueleweka ni habari zilizo ndani yake. Si kitabu cha hekaya au mambo ya kubuniwa. Badala yake, kulingana na The World Book Encyclopedia kwa sehemu kubwa kitabu hicho kinazungumzia “kuhusu watu wakuu na wa kawaida” na pia “changamoto, matumaini, makosa, na mafanikio yao.” Ni rahisi kwetu kuelewa vizuri masimulizi hayo ya watu na matukio halisi na kujifunza masomo muhimu.—Waroma 15:4.

KINAPATIKANA KWA WOTE

Ni lazima kitabu kiwe katika lugha unayojua ili uweze kukielewa. Hata iwe unaishi wapi au unatoka taifa gani, huenda Biblia inapatikana katika lugha unayoelewa. Fikiria mambo yanayohusika ili jambo hilo liwezekane.

Utafsiri. Awali Biblia iliandikwa katika lugha ya Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki. Jambo hilo lilifanya watu wengi wasiojua lugha hizo washindwe kuisoma. Jitihada nyingi zimefanywa na watafsiri wanyoofu ili Biblia ipatikane katika lugha nyingi zaidi. Kwa sababu ya jitihada zao, leo Biblia imetafsiriwa ikiwa nzima au kwa sehemu katika lugha 2,700 hivi. Hilo linamaanisha kwamba zaidi ya asilimia 90 ya watu wanaweza kusoma sehemu fulani za Biblia katika lugha yao ya asili.

Uchapishaji. Awali, maandishi ya Biblia yaliandikwa katika vitu vinavyoweza kuharibika kama vile mafunjo na ngozi. Ili kufikisha ujumbe, maandishi hayo yalinakiliwa kwa uangalifu. Nakala hizo zilikuwa ghali sana na ni watu wachache tu walioweza kununua. Hata hivyo, baada ya uvumbuzi wa mashine ya kuchapa ya Gutenberg miaka 550 iliyopita, uchapishaji wa Biblia uliongezeka sana. Kulingana na ripoti moja, inakadiriwa kwamba nakala zaidi ya bilioni tano za Biblia, zikiwa nzima au kwa sehemu, zimegawanywa.

Hakuna kitabu chochote cha dini kinacholingana na Biblia. Kwa kweli, Biblia ni kitabu kinachoweza kueleweka. Hata hivyo, huenda isiwe rahisi kwako kuielewa. Lakini, unaweza kusaidiwa. Unaweza kupata wapi msaada huo? Utanufaikaje? Majibu yanapatikana katika makala inayofuata.

Taarifa Fupi Kuhusu Biblia

  • Biblia ni mkusanyiko wa vitabu vitakatifu 66.

  • Habari zinazopatikana katika Biblia zinatia ndani historia, sheria, unabii, ushairi, methali, nyimbo, na barua.

  • Ilianza kuandikwa mwaka wa 1513 K.W.K. na kumalizika mwaka wa 98 W.K., kwa kipindi cha miaka zaidi ya 1,600.

  • Wanaume 40 hivi waliandika Biblia wakiongozwa na roho ya Mungu.

Was Life Created?

Kwa habari zaidi kuhusu chanzo cha uhai, tazama broshua Uhai—Ulitokana na Muumba? iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Inapatikana pia katika www.jw.org/sw

Biblia—Ina ujumbe Gani?

Ili kujifunza mengi zaidi kuhusu Biblia, tazama broshua Biblia—Ina Ujumbe Gani? iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Pia, inapatikana kwenye www.jw.org/sw.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki