Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp16 Na. 3 uku. 16
  • Biblia Inasema Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia Inasema Nini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Mungu ana jina?
  • Je, ni kosa kutaja jina la Mungu?
  • Jina la Mungu
    Amkeni!—2017
  • Kwa Nini Tunapaswa Kutumia Jina la Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Kwa Nini Ni Lazima Tujue Jina la Mungu
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • Mungu Anaitwa Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
wp16 Na. 3 uku. 16
Jina la Mungu kama lilivyoandikwa katika hati za kale za Biblia

Jina la Mungu (lililowekewa alama) kama lilivyoandikwa katika hati za kale za Biblia

Biblia Inasema Nini?

Je, Mungu ana jina?

BAADHI YA WATU HUSEMA kwamba Mungu hana jina, wengine husema anaitwa Mungu au Bwana, na wengine husema Mungu ana majina mengi. Wewe una maoni gani?

BIBLIA INASEMA HIVI

“Wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”—Zaburi 83:18.

MAMBO MENGINE TUNAYOJIFUNZA KATIKA BIBLIA

  • Ingawa Mungu ana majina mengi ya cheo, amejipa jina moja tu.—Kutoka 3:15.

  • Mungu si fumbo; anataka tumjue. —Matendo 17:27.

  • Kujua jina la Mungu ni hatua ya kwanza ya kuwa rafiki yake.—Yakobo 4:8.

Je, ni kosa kutaja jina la Mungu?

UNGEJIBUJE SWALI HILO?

  • Ndiyo

  • Hapana

  • Labda

BIBLIA INASEMA HIVI

“Usilitumie jina la Yehova Mungu wako kwa njia isiyofaa.” (Kutoka 20:7) Ni vibaya kutumia jina la Mungu kwa njia inaonyesha kwamba huliheshimu.—Yeremia 29:9.

NI NINI KINGINE TUNACHOJIFUNZA KATIKA BIBLIA?

  • Yesu alilijua na kulitumia jina la Mungu. —Yohana 17:25, 26.

  • Mungu anataka tumwite kwa jina. —Zaburi 105:1.

  • Maadui wa Mungu hufanya yote wawezayo ili kuwafanya watu wasahau jina lake.—Yeremia 23:27.

Kwa habari zaidi, soma sura ya 1 ya kitabu hiki, Biblia Inafundisha Nini Hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Pia kinapatikana kwenye www.jw.org/sw

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki