Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp16 Na. 2 kur. 11-13
  • Kutii Onyo Kunaweza Kuokoa Uhai Wako!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutii Onyo Kunaweza Kuokoa Uhai Wako!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TAMBUA HARAKA MABADILIKO
  • KUDHIHIRISHWA KWA UPENDO WA MUNGU
  • KIMBILIA MAHALI SALAMA!
  • Mawimbi Yanayofisha Hekaya na Ukweli
    Amkeni!—2001
  • Yesu Alisema Mwisho Utakuja Lini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
  • Maswali Manne Kuhusu Mwisho Yajibiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Tsunami ya 2011 Nchini Japani—Masimulizi Kutoka kwa Waokokaji
    Amkeni!—2011
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
wp16 Na. 2 kur. 11-13
Ukanda wa pwani ya Sumatra, nchini Indonesia iliyoharibiwa na tsunami

Kutii Onyo Kunaweza Kuokoa Uhai Wako!

Desemba 26, 2004, tetemeko kubwa la kipimo cha 9.1 lilitikisa mji wa Simeulue, uliopo kaskazini-magharibi mwa pwani ya Sumatra, Indonesia. Watu wote waliokuwa pwani walitazama baharini. Maji yalirudi nyuma kuliko ilivyo kawaida. Punde si punde, watu walianza kukimbilia maeneo yenye miinuko huku wakipiga kelele na kusema “Smong! Smong!” neno la lugha ya kienyeji linalomaanisha tsunami. Kwa dakika 30, mawimbi makubwa yenye nguvu yalipiga pwani, yakaharibu nyumba nyingi na vijiji vingi.

Kisiwa cha Simeulue kilikuwa cha kwanza kukumbwa na tsunami. Kati ya wakazi 78,000 wa kisiwa hicho, ni saba tu waliokufa. Kwa nini walikufa wachache hivyo?a Watu wa kisiwa hicho husema hivi: ‘Kukiwa na tetemeko kubwa na maji ya bahari yanarudi nyuma, kimbilia kwenye eneo lenye mwinuko, kwa kuwa baada ya muda mfupi pwani itapigwa na mawimbi makubwa.’ Matukio yaliyopita yaliwafunza watu wa Simeulue kutambua dalili za tsunami kwa kuangalia mabadiliko ya bahari. Kutii onyo kuliokoa maisha yao.

Biblia inaeleza kuhusu janga baya litakalotukia hivi karibuni, “dhiki kuu ya namna ambayo haijapata kutukia tangu mwanzo wa ulimwengu mpaka sasa, hapana, wala haitatukia tena.” (Mathayo 24:21) Kwa kuwa Mungu amekusudia dunia iwepo milele, dhiki hiyo haimaanishi uharibifu wa sayari yetu Dunia kupitia wanadamu au janga fulani la asili. (Mhubiri 1:4) Badala yake, dhiki hiyo itakuja ili Mungu ‘awaharibu wale wanaoiharibu dunia.’ Huo utakuwa mwisho wa uovu na mateso. (Ufunuo 11:18; Methali 2:22) Itakuwa baraka iliyoje!

Tofauti na tsunami, matetemeko ya ardhi, au milipuko ya volkeno, uharibifu unaokuja hautaua watu wazuri. Biblia inasema “Mungu ni upendo,” na Mungu ambaye jina lake ni Yehova, ameahidi kwamba “waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.” (1 Yohana 4:8; Zaburi 37:29) Hata hivyo, unawezaje kuokoka dhiki kuu na kufurahia baraka zilizoahidiwa? Siri ni: Kutii maonyo!

TAMBUA HARAKA MABADILIKO

Hatuwezi kujua tarehe hususa ya kuondolewa kwa uovu na mateso, kwa kuwa Yesu alisema hivi: “Kuhusu siku ile na saa ile hakuna mtu anayejua, wala malaika wa mbinguni wala Mwana, ila Baba tu.” Halafu akatutia moyo kwa maneno haya, “endeleeni kukesha.” (Mathayo 24:36; 25:13) Jinsi gani? Biblia inatueleza jinsi hali za ulimwengu zitakavyokuwa kabla Mungu hajaleta mwisho. Kama vile wakazi wa Simeulue walivyotambua kukaribia kwa tsunami kutokana na mabadiliko ya ghafula baharini, mabadiliko ya matukio ya ulimwengu huu yanatusaidia kutambua kwamba mwisho uko karibu. Sanduku linataja baadhi ya mabadiliko yanayozungumziwa katika Biblia.

Ni kweli kwamba baadhi ya matukio au hali hizo zilizoorodheshwa katika sanduku zilitokea kwa kiasi fulani wakati uliopita. Hata hivyo, Yesu anasema tunapoona “mambo yote hayo” tujue kwamba mwisho uko karibu sana. (Mathayo 24:33) Jiulize hivi, ‘Ni wakati gani mambo hayo yaliyotajwa (1) yalitukia ulimwenguni pote, (2) yalitukia kwa wakati mmoja, na (3) yalibadilika na kuwa mabaya zaidi?’ Kwa kweli, tunaishi wakati huo.

KUDHIHIRISHWA KWA UPENDO WA MUNGU

Rais wa zamani wa Marekani alisema, “kutoa onyo mapema . . . kunaokoa uhai.” Baada ya tsunami ya mwaka 2004, mfumo wa kutoa onyo uliwekwa katika eneo lote lililoathiriwa ili kuzuia vifo vya watu wengi wakati ujao. Vivyo hivyo Mungu ametoa onyo mapema. Biblia ilitabiri hivi: “Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.”—Mathayo 24:14.

Mwaka uliopita, Mashahidi wa Yehova walitumia saa bilioni 1.9 kuhubiri habari njema kwenye nchi 240 kwa lugha zaidi ya 700. Maendeleo hayo ya kazi ya kuhubiri yanathibitisha kwamba mwisho upo karibu. Wakichochewa na upendo wao kwa jirani, Mashahidi wa Yehova wanajitahidi kuwaonya kuhusu siku ya hukumu ambayo inakaribia sana. (Mathayo 22:39) Yehova anathibitisha kwamba anakupenda kwa kukupatia habari hizi zenye faida. Kumbuka, “[Mungu] hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.” (2 Petro 3:9) Je, utathamini upendo wa Mungu na kutii onyo?

KIMBILIA MAHALI SALAMA!

Wakumbuke wakazi wa kijiji cha Simeulue, walipoona maji katika bahari yamerudi nyuma walikimbilia maeneo yaliyoinuka, hawakusubiri maji yarudi. Uamuzi mzuri waliofanya uliokoa uhai wao. Ili tuokoke dhiki inayokuja, tunapaswa kukimbilia maeneo yaliyoinuka kwa njia ya mfano kabla haijawa kuchelewa mno. Jinsi gani? Nabii Isaya aliandika kuhusu mwaliko wenye kuvutia ambao ungetolewa “katika siku za mwisho,” yaani, wakati huu tunaoishi. Mwaliko huo unasema hivi: “Njooni, twendeni juu kwenye mlima wa Yehova . . . naye atatufundisha njia zake, nasi tutatembea katika mapito yake.”—Isaya 2:2, 3.

Ukiwa juu ya mlima unakuwa katika eneo lililoinuka na ambalo ni salama. Vivyo hivyo, kujua njia za Mungu kupitia kujifunza Biblia kumewasaidia watu wengi ulimwenguni wanufaike kwa kubadili maisha yao. (2 Timotheo 3:16, 17) Kwa kufanya hivyo, wanaanza ‘kutembea katika mapito ya [Mungu]’ na kufurahia baraka na ulinzi wake.

Je, utakubali mwaliko wa Mungu na kunufaika na upendo wake katika siku hizi za mwisho? Tunakusihi uchunguze kwa uangalifu uthibitisho wa Maandiko kwamba tunaishi katika “siku za mwisho” unaoonyeshwa kwenye sanduku lililo katika makala hii. Mashahidi wa Yehova katika eneo unaloishi watafurahi kukusaidia uyaelewe vizuri maandiko na ujue jinsi ya kuyatumia. Au unaweza kupata majibu ya maswali yako kwa kutembelea tovuti yetu, www.jw.org/sw. Tafuta kwenye MAFUNDISHO YA BIBLIA > MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA.

a Tsunami hiyo ya mwaka 2004 ilikuwa janga baya zaidi katika historia ambalo liliua watu zaidi ya 220,000.

MATUKIO YA ULIMWENGU YANAYOONYESHA KWAMBA MWISHO UKO KARIBU

Mzinga

KUONGEZEKA KWA VURUGU NA VITA ULIMWENGUNI

“Mtasikia juu ya vita na habari za vita; angalieni kwamba msiogope. Kwa maana mambo hayo lazima yatukie, lakini ule mwisho bado. Kwa maana taifa litasimama kupigana na taifa na ufalme kupigana na ufalme . . . Mambo yote hayo ni mwanzo wa maumivu ya taabu.”—Mathayo 24:6-8.

Watoto wenye njaa

MAGONJWA NA NJAA ULIMWENGUNI

“Katika mahali pamoja baada ya pengine kutakuwa na tauni na upungufu wa chakula.” —Luka 21:11.

Kasisi amefungwa pingu

KUONGEZEKA KWA UASI-SHERIA NA DINI ZA UWONGO

“Na manabii wengi wa uwongo watatokea na kuwapotosha wengi na kwa sababu ya kuongezeka kwa uasi-sheria upendo wa walio wengi zaidi utapoa.”—Mathayo 24:11, 12.

Kasisi akifungisha ndoa ya watu wa jinsia moja

KUPOROMOKA KWA MAADILI YA JAMII KWA KIWANGO KIKUBWA

“Katika siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda pesa, . . . wasio washikamanifu, wasio na upendo wa asili, wasiotaka makubaliano yoyote, wachongezi, wasiojizuia, wakali, wasiopenda wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kujivuna kwa kiburi.”— 2 Timotheo 3:1-4.

Mashahidi wa Yehova wakihubiri hadharani

KUHUBIRIWA KWA HABARI NJEMA YA UFALME ULIMWENGUNI POTE

“Hii habari njema ya ufalme itahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote na ndipo ule mwisho utakapokuja.”—Mathayo 24:14.

Mwanamke amenyoosha mkono wako kupinga habari njema

WADHIHAKI WANAOPINGA KWAMBA MWISHO UKO KARIBU

“Katika siku za mwisho watakuja wadhihaki na dhihaka zao, . . . na kusema: ‘Huku kuwapo kwake kulikoahidiwa kuko wapi? Kwani, tangu siku mababu zetu walipolala katika kifo, mambo yote yanaendelea sawasawa kama tangu mwanzo wa uumbaji.’”—2 Petro 3:3, 4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki