Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp16 Na. 4 kur. 14-15
  • Uchunguzi Muhimu Zaidi Unaoweza Kufanya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uchunguzi Muhimu Zaidi Unaoweza Kufanya
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JINSI YA KULINGANISHA MAMBO TUNAYOAMINI NA MAFUNDISHO YA BIBLIA
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Ni Nani Wanaoenda Mbinguni, na kwa Sababu Gani?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
wp16 Na. 4 kur. 14-15

Uchunguzi Muhimu Zaidi Unaoweza Kufanya

JE, WEWE ni Mkristo? Ikiwa ndivyo, wewe ni miongoni mwa watu zaidi ya bilioni mbili duniani pote wanaodai kuwa wafuasi wa Kristo. Leo, kuna maelfu ya dini zinazodai kuwa za Kikristo, hata hivyo, maoni na mafundisho yao yanatofautiana. Hivyo, mambo unayoamini yanaweza kutofautiana na ya Wakristo wengine. Je, ni muhimu kuchunguza yale unayoamini? Ndiyo, ni muhimu, ikiwa unataka kufuata mambo ambayo Biblia inafundisha kuhusu Ukristo.

Wafuasi wa Yesu Kristo wa mapema walijulikana kuwa “Wakristo.” (Matendo 11:26) Hakukuwa na haja ya kutumia majina mengine ili kuwatambulisha, kwa kuwa kulikuwa na imani moja tu ya Kikristo. Wakristo hao wenye umoja walifuata mafundisho na maagizo ya Yesu Kristo, Mwanzilishi wa Ukristo. Namna gani dini yako? Je, unaamini kwamba dini yako inafuata yale ambayo Kristo alifundisha, na yale ambayo wafuasi wa mapema wa Kristo waliamini? Unawezaje kujua mambo hayo? Kuna njia moja tu, nayo ni kuitumia Biblia kuwa kifaa cha kufanyia uchunguzi.

Fikiria jambo hili: Yesu Kristo aliheshimu sana Maandiko kwa sababu ni Neno la Mungu. Aliwapinga wale waliopuuza mafundisho ya Biblia na kufuata mapokeo ya wanadamu. (Marko 7:9-13) Hivyo, tunaweza kufikia mkataa kwamba imani ya wafuasi wa kweli wa Yesu inapaswa kutegemea Biblia. Kwa hiyo kila Mkristo anahitaji kujiuliza hivi, ‘Je, mafundisho ya dini yangu yanapatana na Biblia?’ Ili kujibu swali hilo, inafaa kulinganisha mafundisho ya dini yako na mambo ambayo Biblia inafundisha.

Yesu alisema kwamba ibada yetu kwa Mungu inapaswa kutegemea kweli, na kweli hiyo inapatikana katika Biblia. (Yohana 4:24; 17:17) Mtume Paulo alisema kwamba wokovu wetu hutegemea kupata “ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Timotheo 2:4) Kwa hiyo, ni muhimu imani yetu itegemee ujuzi sahihi wa Biblia. Wokovu wetu unategemea jambo hilo!

JINSI YA KULINGANISHA MAMBO TUNAYOAMINI NA MAFUNDISHO YA BIBLIA

Tunakualika usome maswali sita yafuatayo na uchunguze majibu ya Biblia kwa maswali hayo. Soma mistari ya Biblia iliyoonyeshwa, na utafakari majibu yake. Kisha jiulize hivi, ‘Je, mafundisho ya dini yangu yanapata na mafundisho ya Biblia?’

Maswali haya machache yanaweza kukusaidia kufanya uchunguzi muhimu zaidi maishani. Je, ungependa kulinganisha mafundisho mengine ya dini yako na mafundisho ya Biblia? Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia kuchunguza kweli za Biblia. Wasiliana na Mashahidi ili kujifunza Biblia bila malipo! Au tembelea tovuti yetu, jw.org/sw.

1 SWALI: Mungu ni Nani?

JIBU: Yehova, Baba ya Yesu, ni Mungu wa milele, mweza-yote na Muumba wa vitu vyote.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA:

“Sikuzote sisi humshukuru Mungu Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo tunaposali kwa ajili yenu.”—Wakolosai 1:3.

“Unastahili, Ee Yehova, naam, Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako navyo vikaumbwa.”—Ufunuo 4:11.

Pia soma Waroma 10:13; 1 Timotheo 1:17.

2 SWALI: Yesu Kristo ni Nani?

JIBU: Yesu ni Mwana mzaliwa wa kwanza wa Mungu. Yesu aliumbwa, kwa hiyo yeye ana mwanzo. Yesu humtii Mungu na kufanya mapenzi Yake.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA:

“Baba ni mkuu kuliko mimi.”—Yohana 14:28.

“[Yesu] ndiye mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.” —Wakolosai 1:15.

Pia soma Mathayo 26:39; 1 Wakorintho 15:28.

3 SWALI: Roho takatifu ni nini?

JIBU: Roho takatifu ni nguvu ya Mungu ambayo huitumia kutimiza mapenzi yake. Roho takatifu si mtu. Watu wanaweza kujazwa na kutiwa nguvu na roho takatifu.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA:

“Elisabeti aliposikia salamu za Maria, yule mtoto mchanga katika tumbo lake la uzazi akaruka; na Elisabeti akajazwa roho takatifu.”—Luka 1:41.

“Mtapokea nguvu wakati roho takatifu itakapofika juu yenu.”—Matendo 1:8.

Pia soma Mwanzo 1:2; Matendo 2:1-4; 10:38.

4 SWALI: Ufalme wa Mungu ni nini?

JIBU: Ufalme wa Mungu ni serikali ya mbinguni. Yesu ni Mfalme wa Ufalme wa Mungu. Hivi karibu Ufalme huo utafanya mapenzi ya Mungu yatendeke duniani pote.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA:

“Malaika wa saba akaipiga tarumbeta yake. Na sauti kubwa zikatokea mbinguni, zikisema: “Ufalme wa ulimwengu umekuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake, naye atatawala akiwa mfalme milele na milele.’”—Ufunuo 11:15.

Pia soma Danieli 2:44; Mathayo 6:9, 10.

5 SWALI: Je, watu wote wema huenda mbinguni?

JIBU: Hapana. Wanadamu waaminifu wachache, yaani, “kundi dogo,” wamechaguliwa na Mungu ili kwenda mbinguni. Watatawala wakiwa wafalme pamoja na Yesu juu ya wanadamu.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA:

“Msiogope, kundi dogo, kwa sababu Baba yenu amekubali kuwapa ninyi ufalme.”—Luka 12:32.

“Watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala wakiwa wafalme pamoja naye.”—Ufunuo 20:6.

Pia soma Ufunuo 14:1, 3.

6 SWALI: Ni nini kusudi la Mungu kwa dunia na wanadamu?

JIBU: Ufalme wa Mungu utakapotawala, dunia itakuwa paradiso na wanadamu waaminifu watafurahia afya kamilifu, amani ya kudumu, na uzima wa milele.

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA:

“Wapole wataimiliki dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.”—Zaburi 37:10, 11.

“Naye atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”—Ufunuo 21:3, 4.

Pia soma Zaburi 37:29; 2 Petro 3:13.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki