Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w16 Aprili uku. 32
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Habari Zinazolingana
  • Mihuri ya Kale Ilikuwa Nini?
    Habari Zaidi
  • “Roho Yenyewe Hutoa Ushahidi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Je, Ni Sili wa Maji-Ujotojoto?
    Amkeni!—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
w16 Aprili uku. 32

MASWALI KUTOKA KWA WASOMAJI

“Rehani” na “muhuri” ambao kila Mkristo mtiwa mafuta anapokea kutoka kwa Mungu ni nini?—2 Kor. 1:21, 22.

Mtu akikandamiza pete ya muhuri kwenye udongo juu ya hati fulani

Zamani, pete ya muhuri ilikandamizwa kwenye udongo wa mfinyanzi au nta ili kuhalalisha hati

Rehani: Kulingana na kitabu fulani cha marejeo, neno la Kigiriki linalotafsiriwa “rehani” kwenye 2 Wakorintho 1:22 lilikuwa “neno la kisheria na la kibiashara” likimaanisha “malipo ya awali, advansi, dhamana, ambayo inalipia mapema kiasi fulani cha gharama ya ununuzi, na hivyo inalinda haki ya kisheria ya kumiliki kitu kinachonunuliwa, au kuhalalisha mkataba.” Katika kisa cha watiwa mafuta, malipo kamili, au thawabu, yanafafanuliwa katika 2 Wakorintho 5:1-5 kuwa yanahusisha kuvaa mwili wa mbinguni usioweza kuharibika. Thawabu hiyo pia inahusisha kupokea zawadi ya kutoweza kufa.—1 Kor. 15:48-54.

Kigiriki cha kisasa kinatumia neno kama hilo kurejelea pete ya uchumba. Huo ni mfano mzuri sana kwa wale ambao watakuwa sehemu ya mke wa mfano wa Kristo.—2 Kor. 11:2; Ufu. 21:2, 9.

Muhuri: Zamani, muhuri ulitumika kama sahihi inayothibitisha umiliki, uhalali, au makubaliano. Katika kisa cha watiwa mafuta, kwa njia ya mfano ‘wanatiwa muhuri,’ au alama, na roho takatifu ili wawe mali ya Mungu. (Efe. 1:13, 14) Hata hivyo, hawatiwi muhuri wa kudumu hadi wakati fulani kabla ya mtiwa mafuta kufa akiwa mwaminifu au wakati fulani kabla ya dhiki kuu kuanza.—Efe. 4:30; Ufu. 7:2-4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki