Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w17 Mei uku. 30
  • Shangwe ya Kuishi Maisha Rahisi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Shangwe ya Kuishi Maisha Rahisi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KWANZA CHANGAMOTO, KISHA HABARI ZENYE KUSISIMUA
  • SHANGWE YAO KUBWA ZAIDI
  • “Mwimbieni Yehova”!
    Igeni Imani Yao
  • Yehova Amwahidi Danieli Thawabu ya Ajabu
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Jinsi Kitabu Cha Danieli Kinavyokuhusu
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Watiwa Nguvu na Mjumbe Kutoka Kwa Mungu
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
w17 Mei uku. 30
Daniel na Miriam wakimhubiria mwanamume fulani nchini Panama

Shangwe ya Kuishi Maisha Rahisi

DANIEL NA MIRIAM walifunga ndoa Septemba 2000 na kuishi katika jiji la Barcelona, Hispania. Daniel anaeleza hivi: “Tuliishi maisha ya kawaida. Kazi zetu zilituwezesha kula katika mikahawa mizuri, kusafiri ng’ambo, na kuvaa mavazi ya bei ghali. Pia, tulishiriki kwa ukawaida katika huduma ya shambani.” Lakini mambo yakabadilika.

Katika kusanyiko la mwaka 2006, Daniel aliguswa moyo sana na hotuba ambapo swali hili liliulizwa: “Je, tunafanya yote tuwezayo ili kuwasaidia wale ‘wanaopepesuka wakielekea kuchinjwa’ ili waingie katika barabara inayoongoza kwenye uzima wa milele?” (Met. 24:11) Ilikazia jukumu la kueneza ujumbe wenye kuokoa uhai wa Biblia. (Mdo. 20:26, 27) Daniel anakumbuka hivi: “Nilihisi kana kwamba Yehova alikuwa akizungumza nami.” Hotuba hiyo ilitaja pia kwamba mtu hupata shangwe zaidi anapoongeza huduma yake. Daniel alijua hilo ni kweli. Tayari Miriam alikuwa ameanza upainia na alikuwa anapata baraka nyingi zilizomletea shangwe.

Daniel anasema hivi: “Nilifikia mkataa wa kwamba nilipaswa kubadili maisha yangu kabisa.” Na alifanya hivyo. Alipunguza muda aliofanya kazi, akaanza kupainia, na akafikiria shangwe ambayo yeye na Miriam wangepata ikiwa wangetumikia mahali penye uhitaji mkubwa wa wahubiri wa Ufalme.

KWANZA CHANGAMOTO, KISHA HABARI ZENYE KUSISIMUA

Katika Mei 2007, Daniel na Miriam waliacha kazi zao na kwenda Panama, nchi waliyowahi kutembelea. Eneo lao jipya lilitia ndani visiwa kadhaa kati ya visiwa vya Bocas del Toro vilivyo katika Bahari ya Karibea, ambavyo wakazi wengi ni Wangabe. Daniel na Miriam walifikiri kwamba wangetumia pesa walizoweka akiba ili waishi Panama kwa miezi minane.

Walisafiri katika visiwa hivyo kwa mashua na baiskeli, na wanakumbuka vizuri siku ya kwanza waliyosafiri kwa baiskeli ambapo walisafiri kwa kilomita 32 hivi, na kupanda milima mirefu kukiwa na jua kali. Daniel alikuwa karibu kuzimia kwa uchovu. Hata hivyo, familia za Wangabe zilizoishi karibu na njia waliyopitia, ziliwaonyesha ukarimu, hasa wenzi hao walipojifunza maneno kadhaa ya lugha ya wenyeji. Muda si muda, walikuwa wakiongoza mafunzo ya Biblia 23.

Lakini akiba yao ilipoisha, shangwe yao iligeuka kuwa huzuni. Daniel anakumbuka hivi: “Kwa machozi, tulianza kufikiria kurudi Hispania. Tulihuzunika sana kuacha mafunzo yetu ya Biblia.” Lakini mwezi mmoja baadaye, walipokea habari zenye kusisimua. Miriam anasema hivi: “Tuliombwa kutumikia tukiwa mapainia wa pekee. Tulipata shangwe kubwa kubaki katika mgawo wetu!”

SHANGWE YAO KUBWA ZAIDI

Katika 2015, kwa sababu ya mabadiliko katika tengenezo, Daniel na Miriam waliombwa waendelee kutumikia wakiwa mapainia wa kawaida. Wangefanya nini? Waliamini ahadi hii inayopatikana katika Zaburi 37:5: “Mkabidhi Yehova njia yako, na kumtegemea, naye mwenyewe atatenda.” Walipata kazi iliyowategemeza, na sasa wanatumikia wakiwa mapainia katika kutaniko fulani mkoani Veraguas, Panama.

Daniel anaeleza hivi: “Kabla ya kuondoka Hispania, hatukuwa na uhakika ikiwa tungeweza kuishi maisha rahisi. Sasa tumefaulu, na hatukosi kitu chochote muhimu.” Shangwe yao kubwa zaidi inatokana na nini? Wanasema hivi: “Kuwasaidia watu wanyenyekevu wajifunze kumhusu Yehova ni shangwe isiyo na kifani!”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki