Yaliyomo
3 Walijitoa Wenyewe Kwa Hiari—Nchini Uturuki
JUMA LA AGOSTI 28, 2017–SEPTEMBA 3, 2017
Makala hii inazungumzia jinsi tunavyoweza kutumia vitu vyetu vya kimwili ‘kujifanyia rafiki’ mbinguni. (Luka 16:9) Pia inaeleza jinsi tunavyoweza kuepuka kuwa watumwa wa ulimwengu wa kibiashara wenye pupa na jinsi tunavyoweza kumtumikia Yehova kikamili kadiri tuwezavyo.
JUMA LA SEPTEMBA 4-10, 2017
12 “Lieni Pamoja na Watu Wanaolia”
Mkristo anaweza kukabilianaje na huzuni ya kufiwa na mpendwa wake? Yehova anaandaa faraja tunayohitaji kupitia Yesu Kristo, Maandiko, na kutaniko la Kikristo. Makala hii itatuonyesha jinsi tunavyoweza kupata faraja na vilevile kuwafariji wanaoomboleza.
JUMA LA SEPTEMBA 11-17, 2017
Zaburi ya 147 inawatia moyo watu wa Mungu wamsifu Yehova tena na tena. Ni nini kilichompendeza mtunga zaburi sana kumhusu Yehova hivi kwamba akataka Mungu asifiwe? Makala hii inazungumzia jambo hilo na inaonyesha kwa nini tunapaswa kuwa na tamaa kama yake ya kumsifu Mungu wetu.
JUMA LA SEPTEMBA 18-24, 2017
22 “Na Alitimize Kusudi Lako Lote”
Ndugu na dada wengi vijana wanajiunga kwa bidii na utumishi wa wakati wote. Je, unatamani kufanya hivyo? Makala hii inatoa ushauri mzuri wa Kimaandiko utakaokusaidia kupangia wakati ujao wenye furaha na mafanikio.