Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w17 Julai kur. 3-6
  • Walijitoa Wenyewe kwa Hiari​—Nchini Uturuki

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Walijitoa Wenyewe kwa Hiari​—Nchini Uturuki
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “KUNA NINI HAPA?”
  • KUMEKUWA NA MANUFAA YA MUDA MREFU
  • KUTUMIKIA KATIKA MSTARI WA MBELE
  • “MYATAZAME MASHAMBA”
  • Kampeni ya Pekee Nchini Bulgaria Yafanikiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Gawanya Trakti Habari za Ufalme Na. 35 kwa Kuieneza Sana
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Mwaliko wa Pekee
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Walijitoa Wenyewe kwa Hiari​—Madagaska
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
w17 Julai kur. 3-6
Alisa akimhubiria mwanamke kando ya treni

Alisa

Walijitoa Wenyewe Kwa Hiari​—Nchini Uturuki

WAKRISTO wa karne ya kwanza walijitahidi sana kuwafikia watu wengi iwezekanavyo na “habari njema ya ufalme.” (Mt. 24:14) Hata baadhi yao walisafiri kwenda nchi nyingine. Kwa mfano, mtume Paulo alisafiri kwenda kwenye eneo ambalo kwa sasa ni nchi ya Uturuki na akahubiri sana katika eneo hilo wakati wa safari zake za umishonari.a Miaka 2,000 hivi baadaye, katika mwaka 2014, kwa mara nyingine tena kampeni ya pekee ya kuhubiri ilifanywa nchini Uturuki. Kwa nini kampeni hiyo ilifanywa? Ni nani walioshiriki katika kampeni hiyo?

“KUNA NINI HAPA?”

NCHINI Uturuki, kuna wahubiri zaidi ya 2,800, lakini nchi hiyo ina watu milioni 79. Hilo linamaanisha kwamba uwiano nchini Uturuki ni mhubiri mmoja kwa watu 28,000 hivi. Kama unavyoweza kuwazia, wahubiri wamefaulu kuwahubiria wakazi wachache tu wa nchi hiyo na habari njema. Kusudi la kampeni hiyo ya pekee ya kuhubiri lilikuwa ni kuwafikia watu wengi iwezekanavyo ndani ya muda mfupi. Ndugu na dada 550 hivi wanaozungumza Kituruki walisafiri kwenda nchini humo na kujiunga na wahubiri wenyeji wakati wa kampeni hiyo. Matokeo yalikuwa nini?

Ushahidi mkubwa ulitolewa. Kutaniko moja jijini Istanbul liliandika hivi: “Watu walipotuona walituuliza, ‘Kuna kusanyiko la pekee hapa? Tunaona Mashahidi wa Yehova kila mahali!’” Kutaniko fulani jijini Izmir liliandika hivi: “Dereva mmoja wa teksi alimwendea mzee wa kutaniko na kumwuliza, ‘Kuna nini hapa? Inaonekana mmeongeza bidii sana!’” Naam, watu walitambua kampeni hiyo.

Steffen anamhubiria mwanamume ndani ya duka la mazulia

Steffen

Ndugu na dada waliosafiri kutoka nchi nyingine walifurahia sana kazi ya kuhubiri. Steffen, anayeishi Denmark, alisema hivi: “Kila siku tuliwahubiria watu ambao hawajawahi kusikia kumhusu Yehova. Nilihisi kwamba nimelitangaza jina la Yehova kwelikweli.” Jean-David anayeishi Ufaransa aliandika hivi: “Tulihubiri kwenye mtaa mmoja kwa saa nyingi. Tulifurahia sana! Watu wengi hawakuwafahamu Mashahidi wa Yehova. Tulifaulu kuanzisha mazungumzo karibu kwenye kila nyumba, kuonyesha moja kati ya video zetu, na kuwaachia wenye nyumba machapisho.”

Jean-David anawahubiria watu wakiwa nyumbani

Jean-David (katikati)

Wahubiri 550 waliwaachia watu machapisho 60,000 hivi ndani ya majuma mawili tu! Kwa kweli ushahidi mkubwa ulitolewa katika kampeni hiyo.

Bidii katika huduma iliongezeka. Kampeni hiyo ya pekee iliwachochea sana ndugu wenyeji. Wengi wao walianza kufikiria utumishi wa wakati wote. Kwa kweli, idadi ya mapainia wa kawaida nchini Uturuki iliongezeka kwa asilimia 24 ndani ya miezi 12 baada ya kampeni hiyo.

Şirin anamwonyesha trakti mwanamke fulani

Şirin

Walioshiriki katika kampeni hiyo walisema jinsi huduma yao ilivyoboreshwa hata baada ya kurudi katika nchi zao. Şirin, dada kutoka Ujerumani aliandika hivi: “Ni rahisi kwa akina ndugu nchini Uturuki kuhubiri isivyo rasmi. Mimi ni mwenye haya sana inapohusu kuhubiri isivyo rasmi. Lakini kwa sababu ya kampeni hiyo ya pekee, kielelezo cha ndugu wenyeji, na sala nyingi, nimefaulu kufanya jambo ambalo nisingeweza kufanya mwanzoni. Hata nilihubiri na kuacha trakti kwenye treni! Sasa mimi si mwenye haya kama zamani.”

Johannes anampa mwenye duka trakti

Johannes

Johannes anayeishi Ujerumani alisema hivi: “Nilijifunza mambo fulani ninayoweza kutumia katika huduma yangu. Akina ndugu nchini Uturuki wanajitahidi sana kuwaambia watu wengi iwezekanavyo kuhusu kweli. Wanahubiri kila wanapopata fursa. Niliamua kufanya vivyo hivyo nitakaporudi Ujerumani. Na sasa ninawahubiria watu wengi zaidi kuliko nilivyokuwa nikifanya.”

Zeynep anamhubiria mwanamke akiwa mahali pa umma

Zeynep

“Kampeni hiyo imebadili sana huduma yangu. Imenisaidia kuwa mwenye ujasiri na kumtegemea Yehova zaidi,” anasema Zeynep kutoka Ufaransa.

Wahubiri waliboresha uhusiano wao. Upendo na umoja miongoni mwa ndugu kutoka nchi mbalimbali uliwachochea sana. Jean-David aliyetajwa mwanzoni, alisema hivi: “‘Tulionja’ ukarimu wa ndugu zetu.” Kisha akaongeza hivi: “Walitukubali kuwa rafiki zao na kuwa sehemu ya familia zao. Walitukaribisha nyumbani kwao. Nilijua kwamba sisi ni undugu wa ulimwenguni pote; nilikuwa nimesoma kuhusu hilo mara nyingi kwenye machapisho yetu. Lakini pindi hii, nilijionea jambo hilo. Nilijivunia zaidi kuwa Shahidi wa Yehova, na ninamshukuru kwa pendeleo hilo la pekee.”

Claire anamhubiria mwanamke akiwa kwenye mkahawa

Claire (katikati)

“Iwe tulitoka Denmark, Ufaransa, Ujerumani, au Uturuki, sote tulikuwa familia moja. Ni kana kwamba Mungu alikuwa amefuta mipaka ya nchi zote,” alisema Claire kutoka Ufaransa.

Stéphanie anamhubiria mwanamke

Stéphanie (katikati)

Stéphanie anayeishi Ufaransa anaongeza hivi: “Kampeni hiyo ya pekee ilitufundisha kwamba kinachotuunganisha si utamaduni au lugha, bali ni upendo wetu kwa Yehova.”

KUMEKUWA NA MANUFAA YA MUDA MREFU

Wengi wa walioshiriki katika kampeni hiyo kutoka nchi nyingine walianza kufikiria kuhamia Uturuki ili kusaidia kazi nyingi inayohitaji kufanywa huko. Baadhi yao tayari wamehamia huko. Wahubiri wanaojitolea wanathaminiwa sana.

Kwa mfano, fikiria kikundi cha wahubiri 25 katika eneo fulani. Kwa miaka mingi, kikundi hicho kilikuwa na mzee mmoja tu. Wazia jinsi wahubiri hao walivyopata shangwe wakati wajitoleaji sita kutoka Ujerumani na Uholanzi walipohamia huko mwaka wa 2015!

KUTUMIKIA KATIKA MSTARI WA MBELE

Ndugu waliojitolea kwa muda katika eneo lenye uhitaji nchini Uturuki wanasema nini kuhusu kuishi huko? Ni kweli kwamba nyakati nyingine kuna changamoto, lakini maisha ya kujitolea yanaridhisha sana. Baadhi yao wanasema hivi:

Federico anamhubiria mwanamume bandarini

Federico

Federico, ndugu aliyeoa mwenye umri wa miaka 40 hivi, aliyehamia kutoka Hispania, anasema hivi: “Kutokuwa na vitu vingi vya kimwili vinavyoweza kuchukua muda wangu mwingi kunanifanya nihisi nikiwa huru, na kunisaidia kukazia fikira mambo muhimu zaidi maishani.” Je, angewapendekezea watu aina hiyo ya utumishi? Anajibu hivi: “Bila shaka! Unapohamia nchi nyingine kwa kusudi la kuwasaidia watu wamjue Yehova, kihalisi unajikabidhi mikononi mwake. Unahisi kwamba Yehova anakujali kuliko wakati mwingine wowote.”

Rudy anamhubiria mwanamume

Rudy

“Unaridhika sana unapotumika kwenye mstari wa mbele kwa njia ya mfano, na unaposhiriki kweli pamoja na watu wengi ambao hawajawahi kuisikia,” anasema Rudy, ndugu aliyeoa mwenye umri wa miaka 60 hivi kutoka Uholanzi. “Kuona jinsi watu wanavyofurahi wanapokubali kweli kunatuletea shangwe kubwa.”

Sascha anamsomea mwanamke Maandiko

Sascha

Sascha, ndugu aliyeoa mwenye umri wa miaka 40 hivi aliyehamia kutoka Ujerumani, anasema hivi: “Kila siku ninapokuwa utumishini, mimi hukutana na watu ambao wanasikia kweli kwa mara ya kwanza. Kuwapa watu wa namna hiyo fursa ya kumjua Yehova hunifanya nifurahi sana.”

Atsuko anahubiria mwanamke akiwa nyumbani

Atsuko

Atsuko, dada aliyeolewa mwenye umri wa miaka 35 hivi kutoka Japani, alisema: “Zamani nilitamani sana Har–​Magedoni ije haraka. Lakini baada ya kuhamia Uturuki, ninamshukuru Yehova kwamba bado yeye ni mwenye subira. Kadiri ninavyoona jinsi Yehova anavyoelekeza mambo, ndivyo ninavyotamani hata zaidi kumkaribia.”

Alisa, dada mwenye umri wa miaka 30 hivi kutoka Urusi, anasema hivi: “Kumtumikia Yehova katika maeneo yenye uhitaji kumenisaidia kuonja wema wake wote.” (Zab. 34:8) Anaongeza hivi: “Yehova si Baba yangu tu bali ni Rafiki yangu wa karibu, ambaye ninaendelea kumjua chini ya hali mbalimbali. Maisha yangu yamejaa pindi zenye furaha, mambo yaliyoonwa yenye kuchangamsha, na baraka nyingi sana!”

“MYATAZAME MASHAMBA”

Kupitia kampeni ya pekee ya kuhubiri nchini Uturuki, habari njema iliwafikia watu wengi zaidi. Lakini bado kuna eneo kubwa ambalo halijahubiriwa. Kila siku, wahubiri waliohamia nchini Uturuki wanakutana na watu ambao hawajawahi kusikia kumhusu Yehova. Je, ungependa kutumikia katika eneo kama hilo? Ikiwa ndivyo, tunakuhimiza: ‘Inua macho yako uyatazame mashamba, kwamba ni meupe kwa ajili ya kuvunwa.’ (Yoh. 4:​35) Je, unaweza kusaidia katika sehemu ya ulimwengu ambayo mashamba “ni meupe kwa ajili ya kuvunwa”? Ikiwa ndivyo, anza kuchukua hatua sasa ili ufikie mradi huo. Jambo moja ni hakika: Kushiriki kikamili zaidi kueneza habari njema “mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia” kutakuletea baraka nyingi ajabu!​—Mdo. 1:8.

a Tazama broshua “Ona Nchi Nzuri,” uku. 32-​33.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki