Gawanya Trakti Habari za Ufalme Na. 35 kwa Kuieneza Sana
1 Oktoba na Novemba itakuwa miezi yenye shughuli nyingi kwetu sote. Wakati wa siku 11 za kwanza za Oktoba, tutatoa maandikisho ya magazeti yote mawili Mnara wa Mlinzi na Amkeni! au nakala mojamoja za magazeti hayo mahali ambapo andikisho halichukuliwi. Kisha, kuanzia Jumapili, Oktoba 12, hadi Jumapili, Novemba 16, tutajiunga na ulimwengu mzima kugawanya trakti Habari za Ufalme Na. 35. Litakuwa pendeleo letu kupeleka ujumbe kwa watu walio mahali petu. Ni jibu la swali hili, “Je, Watu Wote Watapata Kupendana?” Wakati wa kampeni hii ya pekee, tutagawanya trakti Habari za Ufalme Na. 35 siku za katikati ya juma. Kwenye miisho-juma, pamoja na kutoa trakti Habari za Ufalme, tutatoa andikisho la magazeti.
2 Ni Nani Wanaoweza Kushiriki? Kama ilivyo kawaida, wazee watakuwa kwenye mstari wa mbele katika kazi hiyo. Kila mtu hufurahia kugawanya trakti Habari za Ufalme, na hapana shaka wahubiri wengi zaidi watajiandikisha wawe mapainia-wasaidizi wakati wa mwezi mmoja au miwili ya kampeni hiyo. Wahubiri wengine watataka kutumia wakati zaidi katika huduma kuliko ilivyo kawaida.
3 Je, una mwanafunzi wa Biblia ambaye ameendelea sana katika kujifunza kitabu Ujuzi na ambaye hivi karibuni atastahili kuingia katika utumishi wa shambani? Labda angeweza kuwa mhubiri asiyebatizwa mapema ifaavyo kuingia katika kampeni ya trakti Habari za Ufalme. Utoaji sahili ndio unaohitajiwa tu ili kutoa trakti hiyo. Kwa mfano, huenda mtu akasema: “Ujumbe huu ni wa maana sana hivi kwamba unagawanywa ulimwenguni pote mwezi huu katika lugha 169. Ningependa uwe na nakala yako mwenyewe.” Hata watoto wachanga wanaweza kushiriki ifaavyo katika kazi hii yenye kusisimua.
4 Viongozi wa funzo la kitabu wanapaswa kumtia moyo kila mshiriki wa kikundi chao ashiriki kikamili katika ugawanyaji wa trakti Habari za Ufalme Na. 35. Pia huenda kukawa na wahubiri ambao wamekuwa wasiotenda lakini wanaoweza kuwa wenye kutenda tena katika utumishi ikiwa wangepokea kitia-moyo kinachohitajiwa. Kabla ya kampeni hiyo, wazee wapaswa kumtembelea kila mmoja wao kuona kinachoweza kufanywa ili kuwasaidia wajiunge na wahubiri wenye uzoefu katika sehemu hii ya huduma.
5 Tukutane Lini kwa Ajili ya Utumishi? Utendaji huu wote utahitaji mipango yenye kufaa na yenye kutumika ya kutoa ushahidi wa kikundi. Iwezekanapo, mikutano ya utumishi yapasa kupangwa kila siku ya katikati ya juma, miisho-juma, na jioni mahali panapofaa kufanya hivyo. Yapasa kufanywa nyakati ambazo zitawezesha wahubiri na mapainia kutumia kwa manufaa kipindi cha kutoa ushahidi. Pia mipango yaweza kufanywa ya kukutana nyakati zinazokaribia jioni kwa manufaa ya wanafunzi wa shule, wafanyakazi wa zamu, na wengine. Mwangalizi wa utumishi atahakikisha kwamba kutakuwa na eneo la kutosha la nyumba hadi nyumba na la biashara ili kila mtu ashiriki kikamili katika mahubiri. Palipo na wahubiri wengi katika sehemu fulani, watalazimika kuwa wenye busara kuhusu idadi itakayohubiri katika sehemu waliyopewa ya eneo.
6 Vipi Wasiokuwako Nyumbani? Twataka kuongea na watu wengi kibinafsi iwezekanavyo tuwaeleze kwa nini wasome trakti Habari za Ufalme Na. 35. Kwa hiyo ikiwa hakuna mtu nyumbani unapozuru, andika anwani na urudi tena wakati tofauti wa siku. Ikiwa jitihada zako za kufikia wenye nyumba hawa hazijafaulu kufikia juma la mwisho la kampeni, unaweza kuacha nakala ya trakti Habari za Ufalme mlangoni mahali ambapo haitaonwa na mpitanjia. Katika maeneo ya wakazi, kaa chonjo kutolea trakti Habari za Ufalme watu ambao huenda ikawa wanatembea barabarani. Unapohubiri maeneo ya vijijini na ambako kuna eneo la kutosha lisiloweza kumalizwa wakati wa kampeni, nakala ya trakti Habari za Ufalme yaweza kuachwa mahali pasipokuwa na watu nyumbani kwenye ziara ya kwanza.
7 Lengo Letu Ni Nini? Makutaniko hayana budi kujitahidi sana kutumia ugavi wao wote wa trakti Habari za Ufalme ili kumaliza eneo lao lote kabla ya kampeni kwisha Novemba 16. Ikiwa mgawo wa eneo la kutaniko lako ni mkubwa sana na ikiwa kuhubiri peke yako ni salama kuliko kuhubiri na mwenzi, huenda ukaona kufanya hivyo kuwa jambo lenye kutumika. Hilo litakuwezesha kufikia watu wengi wenye kustahili kadiri iwezekanavyo kwa habari njema. (Mt. 10:11) Huenda likawa jambo lenye faida kubeba baadhi ya trakti mkononi mwako. Hakikisha kuandika vizuri majina na mahali pa wale wanaoonyesha kupendezwa.
8 Je, Uko Tayari Kuanza? Magazeti ya ziada yakihitajiwa, yanaweza kupatikana kutoka makutaniko jirani. Hakuna haja ya kuagiza trakti Habari za Ufalme Na. 35, kwa kuwa upakizi unapelekwa kwenye kila kutaniko. Mapainia wa pekee, wa kawaida, na wasaidizi watapata nakala 250 kila mmoja wao za kugawanya, huku wahubiri wa kutaniko wakigawiwa nakala 50 kila mmoja wao. Tumekwisha kuelezwa jinsi tutakavyoifanya kazi yetu. Je, una hamu ya kushiriki utendaji huu wenye kupendeza sana? Bila shaka. Acheni tugawanye kwa kuieneza sana trakti Habari za Ufalme Na. 35 yenye ujumbe wa maana unaotegemea Biblia.