Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/97 uku. 1
  • Mlango Mkubwa Uongozao Kwenye Utendaji Umefunguliwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mlango Mkubwa Uongozao Kwenye Utendaji Umefunguliwa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Njia za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Kabla ya Kuhubiri, Huenda Ukahitaji Kutafuta Kwanza
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Njia za Kupanua Huduma Yako
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Je, Kutaniko Lenu Lina Eneo Kubwa Mno?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 11/97 uku. 1

Mlango Mkubwa Uongozao Kwenye Utendaji Umefunguliwa

1 Akiwa mhubiri wa habari njema mwenye bidii, Paulo alitafuta kabisa kwa hamu maeneo yaliyokuwa na uhitaji mkubwa zaidi, moja ya hayo lilikuwa jiji la Efeso. Alikuwa na mafanikio mazuri akihubiri huko hivi kwamba aliandikia Wakristo wenzake hivi: “Nimefunguliwa mlango mkubwa uongozao kwenye utendaji.” (1 Kor. 16:9) Paulo aliendelea kutumikia akiwa katika eneo hilo naye akasaidia Waefeso wengi kuwa waamini.—Mdo. 19:1-20, 26.

2 Leo tumefunguliwa mlango mkubwa uongozao kwenye utendaji. Tuna mwaliko wa kusaidia makutaniko ambayo hayawezi kuhubiri eneo lao lote kikamili kila mwaka. Hivyo jitihada zetu zaweza kusawazisha uhitaji uliopo katika maeneo mengine.—Linganisha 2 Wakorintho 8:13-15.

3 Je, Waweza Kutumikia Mahali Palipo na Uhitaji Mkubwa Zaidi? Je, umefikiria kwa njia ya sala uwezekano wa kutumikia mahali penginepo? Huenda ukaweza kusaidia kutaniko fulani mjini mwako mwenyewe. Kwa nini usiongee na mwangalizi wa mzunguko kuhusu jambo hilo na uone atakayodokeza? Au huenda ikawa kwamba katika eneo la kutaniko lako mwenyewe, kuna idadi ya watu iliyo kubwa ya viziwi au watu wenye kuongea lugha ya kigeni ambayo hakuna mtu ambaye ameweza kuishughulikia. Ili kutimiza uhitaji huu, je, waweza kujikakamua ujifunze lugha yao? Kisha tena, labda tayari kuna kikundi cha lugha nyingine au kutaniko lililo karibu ambalo limekuwa ‘likimwomba Bwana-Mkubwa wa mavuno lipate wafanyakazi zaidi wa Ufalme.’ (Mt. 9:37, 38) Ikiwa ni hivyo, je, waweza kusaidia?

4 Miongo ya hivi majuzi, maelfu ya familia za Kikristo yamehamia nchi nyingine ili yashiriki kikamili zaidi katika kazi ya mavuno. Wenzi wa ndoa waliofanya hivi walisema: “Tulitaka kumtumikia Yehova mahali ambapo tungesaidia zaidi.” Ukiwa na tamaa hii na ukiona inawezekana kuhamia penginepo katika nchi yako au ukiwa na sifa ya ustahili kutumika katika nchi nyingine, kwanza zungumza matazamio yako na wazee wa kutaniko lako.

5 Ukitaka kuulizia habari kutoka kwa Sosaiti kuhusu mahali palipo na uhitaji, andalia Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko barua inayoonyesha tamaa yako mahususi. Wataambatisha maelezo yao na kuipelekea Sosaiti. Kwa vyovyote vile, maadamu mlango mkubwa uongozao kwenye utendaji unaendelea kuwa umefunguliwa, sisi sote na tuendelee kuwa wenye shughuli nyingi katika utumishi wa Yehova.—1 Kor. 15:58.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki