Jitahidi Kufikilia Wenzi Wasio Mashahidi
1 Kuna sababu ya kuwa na shangwe kubwa wakati wenzi waliooana wanapoungana katika ibada ya kweli. Hata hivyo, katika familia nyingi ni mwenzi mmoja tu wa ndoa ambaye ameikubali njia ya kweli. Twaweza kujitahidije kufikilia wale wenzi wasio Mashahidi na kuwatia moyo wamwabudu Yehova pamoja nasi?—1 Tim. 2:1-4.
2 Elewa Kufikiri Kwao: Ijapokuwa baadhi ya wenzi wasio Mashahidi huenda wakawa wenye kupinga, mara nyingi tatizo ni ubaridi au kutoelewa. Huenda mtu akahisi kuwa amepuuzwa au huenda akawa mwenye wivu kuhusu kupendezwa kupya kwa kiroho kwa mwenzi wake. “Nikiwa peke yangu nyumbani, nilihisi nimeachwa,” mume mmoja akumbuka hivyo. “Nilihisi kana kwamba mke wangu na watoto wangu walikuwa wananiacha,” asema mwingine. Huenda wanaume wengine wakafikiri kwamba wanapoteza familia yao kwa sababu ya dini. (Ona Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 1990, ukurasa wa 20-23.) Ndiyo sababu ni bora zaidi, ikiwezekana, mume atiwe ndani ya mpango wa funzo la Biblia nyumbani tangu mwanzo pamoja na mke wake.
3 Fanyeni Mambo Pamoja: Wenzi fulani wa ndoa walio Mashahidi walifanya mambo pamoja kwa matokeo katika kusaidia watu waliooana waje katika kweli. Baada ya dada kuwa ameanzisha funzo na mke, ndugu angemtembelea mume. Mara nyingi angeweza kuanzisha funzo na mume.
4 Uwe Mwenye Urafiki na Mwenye Kukaribisha Wageni: Katika kutaniko familia zaweza kwa kupendezwa na familia ambazo bado hazijaungana katika ibada ya kweli. Ziara chache za kirafiki huenda zikamsaidia mwenzi asiye Shahidi aone Mashahidi wa Yehova kuwa Wakristo wachangamfu, wenye kujali wanaopendezwa sana na kila mtu.
5 Mara kwa mara, wazee wanaweza kupitia zile jitihada za juzijuzi ambazo zimefanywa ili kujitahidi kufikilia wenzi wasio Mashahidi na waamue linaloweza kufanywa hata zaidi kukiwa na matumaini ya kuwavuta kwa Yehova.—1 Pet. 3:1, kielezi-chini katika New World Translation of the Holy Scriptures—With References.