Mikutano Ya Utumishi Kwa Novemba
Juma Linaloanza Novemba 3
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. “Habari Njema Katika Internet.” Toa maelezo juu ya ripoti ya utumishi wa shambani ya Julai ya nchini na ya kutaniko la kwenu.
Dak. 15: “Mlango Mkubwa Uongozao Kwenye Utendaji Umefunguliwa.” Hotuba itolewe na mzee, kutia ndani mazungumzo na wasikilizaji. Tia moyo wote wanaoweza kujitahidi kufikilia ushiriki mkubwa zaidi katika kazi ya kuhubiri. Tia ndani ushauri uliotolewa katika Mnara wa Mlinzi la Agosti 15, 1988, ukurasa wa 22.
Dak. 20: “Fuatia Kupendezwa Kulikoonyeshwa Katika Trakti Habari za Ufalme.” Maswali na majibu. Toa wonyesho wa utoaji mbalimbali ulio katika fungu la 6. Katika moja ya utoaji huo, onyesha funzo la Biblia likianzishwa.
Wimbo 144 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 10
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Julisha kutaniko ni eneo gani linalobaki kuhubiriwa kwa kutumia trakti Habari za Ufalme Na. 35. Tia moyo wote washiriki kikamili katika juma la mwisho la kampeni ya pekee.
Dak. 15: Adabu Nzuri Kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko. Twathamini ukaribishaji-wageni wa familia zinazofanya nyumba zao zipatikane kwa ajili ya funzo la kitabu. Hilo huenda likatia ndani matayarisho makubwa ya kadiri na usumbufu. Tunapohudhuria, twapaswa kuonyesha adabu nzuri na kuonyesha staha na ufikirio, ambako kungetia ndani yafuatayo: (1) Twapaswa kupangusa miguu yetu kwa uangalifu kabla ya kuingia, ili kuepuka kuchafua sakafu au zulia. (2) Wazazi wapaswa kusimamia watoto wao, wakihakikisha kwamba wanajiendesha vizuri na kukaa sehemu iliyochaguliwa kwa ajili ya funzo la kitabu. (3) Ijapokuwa huenda kikundi kikawa kidogo na kwa kiasi fulani mazingira sio rasmi, huu ni mkutano wa kutaniko nasi twapaswa kuvalia kama tunavyovalia tuendapo kwenye Jumba la Ufalme. (4) Ushirika baada ya mkutano wapaswa kuwa mfupi ili watu wa nyumba hiyo wawe na wakati wao wa faragha. (5) Ijapokuwa mwenye nyumba wa mahali ambapo funzo lafanyiwa huenda akachagua mara kwa mara kutoa viburudisho baada ya funzo, watu wote wanapasa kuelewa kwamba hilo halitazamiwi wala halihitajiwi.
Dak. 20: “Jitahidi Kufikilia Wenzi Wasio Mashahidi.” Mazungumzo kati ya wazee wawili wanaohangaikia kujua kibinafsi mengi zaidi kuhusu wenzi wasioamini. Pia wanachunguza madokezo yaliyotolewa katika Mnara wa Mlinzi la Mei 15, 1989, ukurasa wa 17-18, fungu la 6-9. Tia ndani mambo yaliyoonwa kutoka Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, 1995, ukurasa wa 10-11, fungu la 11-12.
Wimbo 148 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 17
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Eleza mipango ya utumishi wa shambani ya mwisho-juma. Shiriki baadhi ya mambo yaliyoonwa ya kwenu kutoka katika kampeni ya trakti Habari za Ufalme Na. 35.
Dak. 20: Twaa Fursa Hii ya Pekee! Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi la Novemba 15, 1996, ukurasa wa 21-23.
Dak. 15: “Nitasema Nini?” Mazungumzo na wasikilizaji. Soma fungu la kwanza kwenye ukurasa wa 8 wa kitabu Kutoa Sababu, ukieleza jinsi ambavyo kitabu hiki kimekusudiwa kutusaidia kutoa ushahidi kwa matokeo juu ya habari mbalimbali za Biblia. Toa kielezi kwa kufanya wonyesho mmoja au mawili yaliyotayarishwa vizuri.
Wimbo 151 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Novemba 24
Dak. 8: Matangazo ya kwenu.
Dak. 15: “Biblia Katika Lugha ya Maisha ya Kila Siku.” Hotuba ikitegemea makala katika Amkeni! la Aprili 8, 1997. Jenga uthamini na tia moyo matumizi ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika makutaniko ya lugha ya Kiswahili na ya Kiingereza. Tia moyo watu wajitayarishe kutumia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya shambani mwezi ujao.
Dak. 22: Fanya Wanafunzi, Ukiwafundisha. Mzee aongoza mazungumzo na kikundi cha wahubiri watatu au wanne, akijibu maswali yanayotegemea kitabu Huduma Yetu, ukurasa wa 88-92: (1) Kwa nini kufanya ziara za kurudia ni muhimu kwa huduma yenye matokeo? Mtu anaweza kukabilianaje na ugumu wa kufanya ziara za kurudia? (2) Kwa nini sisi hukazia sana kuanzisha mafunzo? Twaweza kuwaje wenye ustadi katika kuongoza mafunzo ya Biblia? (3) Kwa nini ni jambo la maana kuelekeza wanafunzi kwenye tengenezo? Twaweza kufanyaje hivyo? Pia kikundi chasimulia jinsi ambavyo nyongeza za juzijuzi za Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni 1996 na Machi na Aprili 1997 zimewasaidia katika maeneo haya.
Wimbo 160 na sala ya kumalizia.