‘Mengi ya Kufanya Katika Kazi ya Bwana’
1 Kwa hakika tuna ratiba iliyojaa utendaji wa kitheokrasi ya kutazamia wakati wa Aprili na Mei! Aprili 14 tutaadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Watu wengi iwezekanavyo wapaswa kutiwa moyo wawepo kwa ajili ya pindi hiyo ya maana: tufahamianao kibiashara, watu wa ukoo wasioitikadi, wanashule wenzi, watu wapya wenye kupendezwa, na mafunzo ya Biblia. Weka orodha ya wale unaopanga kualika ili kwamba yeyote asikose.
2 Juma lifuatalo tutatia moyo wote waliohudhuria Ukumbusho wasikie hotuba ya pekee Aprili 23, juu ya “Mwisho wa Dini Bandia U Karibu.” Yatumainiwa kwamba wenye kupendezwa wengi wanaosikia ujumbe huu wa moja kwa moja wataona uhitaji wa kushirikiana na kutaniko kwa ukawaida, si kwa pindi za pekee tu.
3 Trakti ya Pekee Habari za Ufalme Kutolewa:
Jambo kuu la mkutano wa Aprili 23 litakuwa kutolewa kwa trakti ya wakati unaofaa yenye kurasa nne Habari za Ufalme Na. 34 ambayo itagawanywa kwa wingi hadi Mei 14. Je, hukubali kwamba kutakuwa na ‘mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana’ wakati wa kipindi hiki cha Ukumbusho?—1 Kor. 15:58.
4 Ugavi wa trakti Habari za Ufalme utapewa kila kutaniko. Makatoni yenye trakti Habari za Ufalme yapaswa kuwekwa mahali salama na hayapaswi kufunguliwa hadi umalizio wa programu katika Aprili 23. Wakati huo trakti Habari za Ufalme itapatikana kwa ajili ya kugawanya kwa akina ndugu na kwa umma. Kwenye umalizio wa mikutano ya kutaniko, makusanyiko ya mzunguko, au programu ya siku ya kusanyiko la pekee katika Aprili 23, wenye kuhudhuria watapokea nakala moja ili wafahamu yaliyomo nao wawe tayari kwa ugawanyaji.
5 Wazee Watakuwa na Mengi ya Kufanya: Mapema mwezi huu baraza la wazee lapaswa kukutana ili kuzungumzia mambo ya kampeni hiyo ya pekee. Makutaniko yapaswa kujitahidi kukamilisha eneo lao walilogawiwa. Kabla ya kampeni kwisha, fanya jitihada za pekee kuhubiri maeneo ambayo hayajashughulikiwa kwa miezi sita. Kuhusu umaana wa kazi hiyo, tutataka kuweka kando wakati mwingi iwezekanavyo kwa ajili ya huduma. Bila shaka wahubiri wengi kuliko kawaida watajiandikisha wawe mapainia-wasaidizi. Yamkini wanafunzi wengi wa Biblia watajiunga nasi wakiwa wahubiri wapya wasiobatizwa waliopendekezwa. Ni wakati wenye kupendeza kama nini tutakaokuwa nao tunapofanya kazi pamoja katika kazi ya Bwana!
6 Viongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko wanapaswa kufanya mipango hususa kwa ajili ya mahubiri ya kikundi Jumamosi na Jumapili. Kila mtu apaswa kutiwa moyo awe na ushirika wenye kutenda. Kuongezea utendaji wa mwisho-juma, ushahidi wa jioni wapaswa kuratibiwa angalau mara moja kwa juma wakati wa kampeni. Mipango ya pekee ya utumishi wa shambani yaweza kufanywa kwa wanafunzi na wengine walio likizoni wakati wa mwezi huu.
7 Mikutano ya utumishi wa shambani yapaswa kuratibiwa ili kwamba wahubiri na mapainia waweze kuanza mapema huduma kila siku. Mikutano hii yapasa kuwa mifupi. Kila mtu apaswa kuwa na utoaji sahili wa trakti Habari za Ufalme. Mikutano ya alasiri ya utumishi wa shambani yaweza kutia ndani dokezo moja au mawili ya kufanya ziara za kurudia kwa wale waliokubali trakti Habari za Ufalme. Hata hivyo, wahubiri fulani hupenda kujihusisha katika ugawanyaji asubuhi na alasiri pia. Kwa kusudi hilo, mwangalizi wa utumishi atataka kuhakikisha kwamba kuna eneo la kutosha. Jina na anwani ya mtu yeyote aonyeshaye kupendezwa yapaswa kuandikwa kwenye rekodi ya nyumba kwa nyumba. Mambo makuu ya mazungumzo mafupi yanaweza kutiwa ndani ya mahali pa maelezo. Hili litatayarisha njia ya ziara ya kurudia baadaye kwenye juma au mwezi.
8 Kutaniko moja likisaidia jingine kushughulikia eneo lao, majina na anwani za watu wenye kupendezwa zapasa kurudishwa kwenye kutaniko linalotunza eneo hilo.
9 Wazazi, je, watoto wenu wanajitahidi kuwa wahubiri wasiobatizwa? Imeonekana kwamba katika makutaniko fulani, watoto wenye tabia nzuri wameandamana na wazazi wao waliojitoa wakfu katika huduma kwa miaka kadhaa, nao watoto wafanya vema sana, ingawa bado si wahubiri wa habari njema. Wazazi wapaswa kufikiria kama watoto wao kwa kweli wanastahili pendeleo hili. Wazee wawili wanaweza kuzungumza mambo yote na kichwa cha familia na waamue kama mtoto aweza kuhesabiwa kuwa mhubiri asiyebatizwa.—om-SW kur. 99-100.
10 Je, kuna wahubiri wowote katika eneo la kutaniko lenu wasiotenda tena katika kutoa dhabihu ya sifa kwa Yehova? (Ebr. 13:15) Wengine wasiotenda huenda wameshindwa na kuvunjika kwa moyo au mahangaiko ya maisha, ingawa waendelea kushikamana na viwango vya Biblia vya adili. Ziara ya kirafiki ya wazee huenda ikawafanya watende ili kurudia ushirika wao na kutaniko na, kwa wakati ufaao, kwa utendaji uliofanywa upya katika huduma.
11 Wote Wanaostahili Wanaweza Kushiriki Katika Kazi Hii Yenye Kufurahisha: Je, baadhi yenu watoto au matineja mnaona ikiwa vigumu kushiriki katika huduma ya nyumba kwa nyumba? Vipi juu yenu ninyi mlio wapya ambao uzoefu wenu katika kazi ya kuhubiri ni wa kadiri? Mtaona kufanya kazi na trakti hii ya pekee Habari za Ufalme kuwa yenye kufurahisha zaidi! Utoaji sahili ndio unaohitajiwa tu.
Unaweza kusema jambo kama hili:
◼ “Mwezi huu tunagawanya ujumbe wa maana katika mabara 232 kuzunguka ulimwengu. Ujumbe huu ni wa maana kwa sababu unatoa sababu zenye uzito za kuamini kwamba kuna suluhisho kwa matatizo tunayokabili leo. Tungependa uwe na nakala yako ya kibinafsi.”
Au unaweza kujaribu hili:
◼ “Mwezi huu wajitoleaji wapatao milioni tano wanagawanya ujumbe wa maana kwa lugha nyingi. Imetayarishiwa watu ambao wangependa kuona mwisho wa matatizo tunayokabili sote leo. Hii ni nakala yako ya kibinafsi.”
Utoaji huu sahili huenda ukakufaa:
◼ “Twatia moyo kila mtu kusoma ujumbe huu wa maana wenye kichwa [soma kichwa cha trakti Habari za Ufalme]. Angalia inavyosema hapa kwenye ukurasa wa 2 kuhusu matatizo ya . . . [soma sentensi iliyochaguliwa kutoka trakti Habari za Ufalme]. Tuna uhakika utafurahia kusoma sehemu iliyobaki ya ujumbe huu wa wakati unaofaa. Hii ni nakala yako.”
12 Pendezwa kibinafsi na kila mtu anayekubali trakti Habari za Ufalme. Ongea polepole na waziwazi; hakuna haja ya kuharakisha utoaji wako. Twataka kutimiza eneo letu kikamili na kuona kwamba wote wanaoonyesha kupendezwa kusoma trakti Habari za Ufalme wanapewa nakala ya kibinafsi. Wakati hakuna mtu nyumbani, tia alama katika rekodi yako ya nyumba kwa nyumba ili uweze kurudi wakati ufaao umtolee mwenye nyumba trakti Habari za Ufalme. Hii trakti Habari za Ufalme yaweza kutumiwa katika ushahidi wa barabarani mtu aonyeshapo kupendezwa katika kusoma habari hiyo. Nakala hazipasi kutolewa kihivi-hivi kana kwamba ni vikaratasi vya mwaliko. Badala yake, mfikie mpita-njia, na ueleze umaana wa ujumbe unaotolewa. Tumia trakti Habari za Ufalme katika ushahidi wa vivi-hivi, kama vile unaposafiri au unapotolea wafanyakazi wenzi ushahidi wakati wa mapumziko ya chakula cha mchana. Wale wenye kukaa ndani au wasio wagonjwa sana wanaweza kuwatolea wageni, madaktari na wauguzi, wafanya biashara, na wengine wanaokuja nyumbani mwao.
13 Utafanya ziara ngapi za kurudia wakati wa kampeni? Bila shaka nyingi zaidi, kwa kuwa wale wote wameonyesha kupendezwa katika trakti Habari za Ufalme wapaswa kutembelewa tena. Kwenye ziara ya kwanza yafaa kutoa tu trakti Habari za Ufalme. Kisha, unaporudi, toa maelezo machache juu ya jinsi ujumbe katika trakti Habari za Ufalme ni wa wakati ufaao. Sikiliza kwa makini mwenye nyumba aelezapo maoni yake kuhusu yale amesoma. Maelezo yake yatakusaidia kujua utakachotoa katika magazeti ya karibuni na labda jinsi ya kujitayarisha kwa ajili ya mazungumzo zaidi. Ukipata itikio zuri kwenye ziara ya kurudia, jaribu kuanzisha funzo la Biblia.—1 Kor. 3:6, 7.
14 “Taabu Yenu Siyo Bure”: Je, kazi yote hii itastahiki? Paulo alihakikishia Wakorintho: “Taabu yenu siyo bure katika Bwana.” (1 Kor. 15:58) Kwa miaka mingi, jitihada zetu za kugawanya trakti Habari za Ufalme zimebarikiwa zaidi. Wenzi wa ndoa waliokuwa wakihamia nyumba iliyokuwa tupu walipata nakala nzee-nzee ya trakti Habari za Ufalme ndani ya kisanduku cha kabati. Ilikuwa ndicho kitu kilichoachwa tu katika nyumba yote. Baada ya kuisoma, waliwasiliana na kutaniko la mahali hapo na kuomba funzo la Biblia. Walianza kuhudhuria mikutano yote na baadaye wakaonyesha tamaa ya kubatizwa. Labda nakala unayoacha italeta matokeo kama hayo!—Ona Amkeni!, Novemba 8, 1976, ukurasa 15, (Kiingereza).
15 Tuna kazi kubwa ajabu mbele yetu. Mradi wetu ni kila kutaniko litimize mgawo wa eneo lake kufikia Mei 14 au kufikia mwisho wa mwezi ikiwa ni lazima kuendeleza wakati wa ugawanyaji wa trakti Habari za Ufalme. Upakizi umefanywa ili kwamba mapainia wa kawaida na wasaidizi wapokee nakala 250 za trakti Habari za Ufalme. Kila mhubiri wa kutaniko atapata nakala 50. Trakti hii ya pekee yapatikana kwa wahubiri na mapainia kwa bei ya kawaida ya trakti. Ushirikiano mzuri utahakikisha ugawanyaji mkubwa zaidi wa ujumbe huu wa maana. Ikiwa kwa sababu ya kuwa na eneo kubwa makutaniko fulani hayajamaliza eneo lao kufikia katikati ya Mei na nakala bado zipo, ingekuwa jambo linalofaa kualika makutaniko mengine yasaidie. Katika makutaniko mengine uhitaji waweza kutimizwa mahali penu ikiwa wahubiri wanaongeza utendaji wao kwa kujiandikisha wawe mapainia-wasaidizi au kwa kujiingiza kwenye huduma mara nyingi.
16 Ujitoaji wa nafsi yote kwa Yehova utahitajiwa ikiwa tutatimiza kazi yetu. (Kol. 3:23) Maisha zahusika. Watu hawawezi kupuuza maana ya hali za ulimwengu leo. Wakati unaisha. Ni lazima watambue uhakika kwamba mwanadamu hana suluhisho la matatizo ya ulimwengu huu. Mungu analo. Wale wanaotamani kupata baraka za Mungu lazima watende kwa kuazimia, bila kuchelewa, kupatana na matakwa yake.
17 Kwenye umalizio wa kampeni hii ya pekee katika Mei 14, je, tutaacha mkono wetu upumzike? La! Tutaendelea kuwa wenye shughuli kupatana na shauri la Paulo lililopuliziwa.