Mnara wa Mlinzi na Amkeni!—Magazeti ya Nyakati Zetu Zenye Uharaka!
1 Kwa kutimiza unabii wa Biblia, matukio yenye kushtua ya ulimwengu yanaendelea kuwapo! Tunapofikiria kwa uzito yanayotukia kati yetu ulimwenguni na pia ndani ya tengenezo la kitheokrasi, twaweza kuelewa kabisa jinsi kulivyo na uharaka kwamba tuhubiri ‘habari njema’ za Ufalme. (Mk. 13:10) Hili hutupa sababu ya kuendelea na huduma yetu kwa bidii wakati wa mwezi wa Aprili.
2 Umaana wa ujumbe wetu wakaziwa na kazi ya pekee tutakayofanya mwezi huu. Kwa matazamio yenye hamu twangojea kutolewa kwa trakti Habari za Ufalme ambayo tutagawanya wakati wa Aprili na Mei. Ili kujenga idili yetu kwa kazi hii na vilevile kusitawisha kupendezwa katika eneo letu, Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yatakuwa na makala za wakati wake zinazokazia umuhimu wa kiunabii wa matukio ya ulimwengu yenye kusumbua. Twaweza kutayarishaje utoaji utakaochochea kupendezwa katika magazeti?
3 Yamkini utaweza kuanzisha utoaji wenye matokeo kwa kufuata hatua hizi za msingi: (1) Teua makala katika mojapo magazeti unayohisi yatavutia watu katika jamii yenu. (2) Chagua elezo au andiko lililonukuliwa katika makala hii unaloamini kwamba litahimiza kupendezwa kwa mwenye nyumba. (3) Tayarisha utoaji mfupi unaotia ndani salamu ya kirafiki, swali au elezo linalokazia wazo la Kimaandiko lenye kupendeza, na mwaliko mchangamfu wa kukubali magazeti. Kama unavyoweza kuona, huu ni sahili na usio tata. Labda mngeweza kukutana na mhubiri mwingine unayehubiri naye katika huduma nanyi mtayarishe utoaji.
4 Kwa kuwa Amkeni! la Machi 8 lina makala “Je, Mungu Apendezwa Kutuona Tukiteseka?” unaweza kutumia maswali yaliyo kwenye ukurasa wa 2 ili kuanza mazungumzo yako. Baadaye unaweza kuteua jambo moja au mawili kutoka kitabu Kutoa Sababu, kurasa 131-133. Kwa kumalizia waweza kutumia maelezo fulani kutoka ukurasa 11 wa makala hiyo kuonyesha kwamba Mungu hafurahii kuteseka kwa binadamu iwe ni taabu ya kujiletea au kutoka vyanzo vya nje.
5 Mnara wa Mlinzi la Machi 15 hutokeza swali: “Unaweza Kutajirishaje Sala Zako?” unaweza kutumia mojapo mawazo kutoka kitabu Kutoa Sababu, kurasa 276-277 ili kuanzisha mazungumzo juu ya mada ya sala.
6 Kabla ya kwenda katika kazi ya kuhubiri, kwa nini usijizoeze utoaji wako na mhubiri mwingine ili uufahamu? Yamkini mtaweza kushiriki madokezo yenye kusaidia kila mmoja wenu yatakayoongeza matokeo yenu na kuwapatia uhakika zaidi.
7 Kadiri mwisho wa mfumo huu wa mambo ukaribiapo, na tuongeze juhudi yetu ili kusaidia wenye mioyo minyoofu wakimbie kutoka Babiloni Mkubwa. (Ufu. 18:4) Mnara wa Mlinzi na Amkeni! hutimiza sehemu muhimu zaidi katika kazi hii ambayo haitarudiwa kamwe. Twashukuru kwamba Yehova ameandaa zana hizi nzuri kwa matumizi yetu!