Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/07 uku. 6
  • Watolee Magazeti Yanayotoa Ushahidi Juu ya Ile Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watolee Magazeti Yanayotoa Ushahidi Juu ya Ile Kweli
  • Huduma ya Ufalme—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kutayarisha Utoaji wa Magazeti
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Jinsi ya Kutumia Mapendekezo ya Kutoa Vichapo
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Tumieni Magazeti Yetu Vema Kabisa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Magazeti Yatangaza Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2007
km 12/07 uku. 6

Watolee Magazeti Yanayotoa Ushahidi Juu ya Ile Kweli

1 Magazeti Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova na Amkeni! yanaendelea kuwa sehemu muhimu ya kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme na kufanya wanafunzi. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Tunafurahi sana kutoa magazeti hayo mawili kwa ukawaida tunaposhiriki katika sehemu mbalimbali za utumishi wetu wa Ufalme.

2 Kadiri ambavyo miaka imepita ndivyo kumekuwa na mabadiliko katika ukubwa na habari iliyomo katika magazeti hayo kutia ndani mbinu ya kutoa magazeti hayo. Mabadiliko hayo yamefanywa ili magazeti hayo yavutie na yawe na matokeo zaidi, ili ujumbe wa Ufalme ufikie mioyo ya ‘watu wa namna zote nao waweze kuokolewa na kupata ujuzi sahihi wa kweli.’—1 Tim. 2:4.

3 Tangu Januari 2006, tumezoea kutumia njia mbalimbali tunapotoa Amkeni! linalochapishwa mara moja kwa mwezi. Sasa tutatumia njia kama hizo tunapotoa moja kati ya matoleo mawili ya Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova katika huduma yetu. Utoaji unaoweza kutumiwa kwa ajili ya kila gazeti huwa kwenye ukurasa wa nyuma wa Huduma Yetu ya Ufalme. Utoaji huo huzungumzia moja kati ya makala za kwanza katika gazeti lakini nyakati nyingine makala nyingine zinazovutia huonyeshwa. Mapendekezo yaliyochapishwa yanaweza kutumiwa kwa njia inayofaa zaidi ikiwa tunafahamu vizuri makala inayozungumziwa na kutumia maneno yetu kuelezea utoaji huo katika eneo letu.

4 Ingawa Huduma Yetu ya Ufalme ina mapendekezo mawili tofauti kwa ajili ya kila gazeti, unaweza kutumia utoaji mwingine tofauti kabisa. Sababu moja ya kufanya hivyo inaweza kuwa kwamba watu katika eneo lenu wanavutiwa zaidi na makala tofauti na ile iliyozungumziwa. Au unaweza kuhisi kwamba unaweza kuzungumza vizuri zaidi ukitumia makala inayokupendeza zaidi.

5 Jinsi ya Kutayarisha Utoaji Wako: Kwanza, unapaswa kufahamu kabisa makala unayotaka kuzungumzia. Huenda usiweze kufahamu kabisa kila makala katika gazeti kabla ya kuanza kulitoa katika huduma ya shambani. Hata hivyo, unapaswa kuwa mchangamfu na mnyoofu kuhusu makala unayochagua kuzungumzia. Unaweza kufanya hivyo tu ikiwa unaifahamu vizuri habari unayozungumzia.

6 Kisha uwe mwenye kubadilikana unapotayarisha maneno yako ya utangulizi. Unaweza kutumia swali la moja kwa moja linalohusiana na makala ambalo linaamsha upendezi ili kuanzisha mazungumzo. Sikuzote tegemea nguvu za Neno la Mungu kugusa moyo. (Ebr. 4:12) Chagua andiko linalofaa linalohusiana na habari unayozungumzia, huenda hilo likawa andiko lililotajwa au kunukuliwa kwenye makala unayozungumzia. Fikiria jinsi unavyoweza kuunganisha andiko na makala hiyo.

7 Tumia Nafasi Zote: Ili utoaji uwe na matokeo mazuri, unapaswa kujaribiwa. Shiriki pamoja na kutaniko katika kutoa magazeti siku ya Jumamosi. Watolee magazeti watu ambao hapo awali wamechukua vichapo vingine. Sikuzote watolee magazeti wanafunzi wa Biblia na watu wengine unaowapata unapofanya ziara za kurudia. Unaweza kuwatolea magazeti watu unaokuta unapokwenda dukani, unaposafiri, au unaposubiri daktari. Boresha utoaji wako ili uutumie mwezi wote.

8 Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ni ya pekee. Yanamtukuza Yehova akiwa Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu. (Mdo. 4:24) Yanawapa watu faraja ya habari njema ya Ufalme wa Mungu na kuwatia moyo wawe na imani katika Yesu Kristo. (Mt. 24:14; Mdo. 10:43) Isitoshe, yanachunguza matukio ya ulimwengu ili kuona jinsi unabii wa Biblia utakavyotimizwa. (Mt. 25:13) Wasaidie watu katika eneo lenu wafaidike kutokana na magazeti hayo kwa kujitayarisha kuyatoa nafasi yoyote inapopatikana!

9 Unapofaulu kuacha gazeti, au ukiwa na mazungumzo yenye kupendeza, uwe tayari na swali au jambo lenye kuchochea fikira ambalo litakupa nafasi ya kufanya ziara ya kurudia na kuwa na mazungumzo mengine ya kiroho. Tukiwa na bidii ya kupanda mbegu za kweli, tunaweza kuwa na hakika Yehova atafungua mioyo ya wale wanaotamani kumjua na kumtumikia.—1 Kor. 3:6.

[Maswali ya Funzo]

1. Mnara wa Mlinzi na Amkeni! hutimiza fungu gani?

2. Ni mabadiliko gani ambayo yamefanywa katika Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, na kwa nini?

3. Magazeti yatatumiwaje katika huduma?

4. Kwa nini inaweza kufaa kutumia utoaji mwingine tofauti na ule uliozungumziwa katika Huduma Yetu ya Ufalme?

5. Kabla ya kutayarisha utoaji wa gazeti, unapaswa kufanya nini?

6. Tunaweza kutayarishaje utoaji wetu?

7. Tunaweza kuboresha utoaji wetu kwa njia gani?

8. Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ni magazeti ya pekee katika njia gani?

9. Tunaweza kuwekaje msingi kwa ajili ya ziara ya kurudia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki