Magazeti Yatangaza Ufalme
1 Tukiwa Mashahidi wa Yehova, twajulikana zaidi kwa bidii yetu ya kuhubiri juu ya Ufalme wa Mungu. Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! tunayogawanya hutimiza fungu lenye nguvu katika kusaidia mamilioni ya watu wajifunze juu ya makusudi ya Mungu. Ujumbe ambao magazeti hayo yanao kwa kweli ni habari njema, kwa kuwa hutangaza Ufalme wa Mungu wa kimbingu kuwa tumaini pekee la wanadamu.
2 Magazeti hayo yanashughulikia mahitaji halisi ya watu, yaani, ya kihisia-moyo, ya kijamii, na ya kiroho. Maadili na viwango vya familia viharibikapo kila mahali, Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yanasaidia watu waboreshe hali ya maisha yao kwa kuwaonyesha jinsi ya kutumia kanuni za Biblia. Itakuwa furaha yetu kutoa magazeti hayo Aprili na Mei.
3 Yanavutia Kwelikweli: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yanapatikana katika karibu lugha zote za watu ulimwenguni. Kwa sababu hiyo, magazeti yetu yanajulikana zaidi. Hizi ni sababu zinazofanya watu wavutiwe nayo:
◼ Yakiwa magazeti yenye uaminifu-maadili na kweli, yanaonyesha waziwazi tofauti kati ya mema na mabaya.
◼ Yanatoa tumaini la paradiso ijayo yenye uadilifu, linalotegemea ahadi ya Mungu ya kuitiisha dunia chini ya utawala wa Ufalme.
◼ Mambo mbalimbali yanazungumziwa, yanayovutia watu wa malezi yote na tamaduni zote.
◼ Makala zilizomo ni fupi, zenye kuelimisha, zenye mambo hakika, na zisizo na ubaguzi wala zenye kuridhiana.
◼ Picha zenye kuvutia macho hutokeza upendezi wa mara moja na mtindo wa kuandika ulio wazi hufanya magazeti hayo yawe rahisi kuyasoma.
4 Yagawanye Kotekote: Ugawanyaji wa magazeti wenye matokeo hutegemea sana bidii yetu katika kutayarisha utoaji, kuweka ratiba ya wakati wetu, na kupanga utendaji wetu wa kuhubiri. Madokezo yenye kusaidia yalitolewa katika matoleo ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1995 na Oktoba 1996, ambayo itakuwa vizuri tukiyapitia na kuyatumia.
5 Pata Kuyafahamu Magazeti: Unaposoma kila toleo, fikiria mtu fulani ambaye ungependa awe na nakala. Tafuta mambo hususa au maandiko unayoweza kunukuu katika utoaji wako. Fikiria swali unaloweza kuuliza kuanzisha mazungumzo na kuchochea kupendezwa katika hilo somo.
6 Patanisha Utoaji na Huyo Mtu: Tayarisha utoaji sahili, wenye kubadilikana ambao waweza kurekebishwa ufaane na mwanamume, mwanamke, mtu mzee, au kijana, awe ni mtu unayemfahamu au usiyemfahamu.
7 Uwe Tayari Sikuzote Kuangusha Mnara wa Mlinzi na Amkeni!: Kwa kuwa magazeti hutoshea kwa urahisi mkobani, kibetini, au mfukoni, twaweza kubeba nakala kadhaa tunaposafiri au kufanya ununuzi. Yatoe unapoongea na jamaa zako, majirani, wafanyakazi wenzako, wanashule wenzako, au walimu. Tenga siku moja kila juma ili utoe ushahidi ukitumia magazeti.
8 Thamini Magazeti Hayo: Hayapotezi thamani yake kamwe. Magazeti ya zamani hayapunguzi umaana wa ujumbe uliomo. Bila shaka, tukijitahidi kipekee kuangusha magazeti yote tuliyo nayo, matoleo ya zamani hayatalundamana katika safu zetu.
9 Utoaji wa Ushahidi Barabarani Una Matokeo: Hii ni njia moja iliyo bora zaidi ya kutoa magazeti kwa idadi kubwa ya watu. Wahubiri fulani huhubiri kwenye barabara zilizo wazi katika muda wa kawaida siku za ununuzi.
10 Eneo la Biashara Ni Lenye Matokeo: Tunapotoa ushahidi duka hadi duka, tuna wachache wasiokuwapo. Watu wengi wa biashara ni wenye adabu, na wengi hukubali magazeti kwa furaha. Kazia makala zinazofaa biashara hiyo.
11 Njia za Kupelekea Watu Magazeti kwa Ukawaida Zina Uwezekano wa Matokeo: Kwa kuwa magazeti yanachapishwa mara mbili kwa mwezi, inafaa kurudia watu ambao huyasoma na kuwatolea matoleo yafuatayo. Twapaswa kufanya ziara za kurudia kwa ukawaida, si kuangusha magazeti tu bali pia kusitawisha kupendezwa kwa mtu huyo katika Biblia. Njia za kupelekea watu magazeti kwa ukawaida ni chanzo bora kabisa cha kuweza kupata mafunzo ya Biblia.
12 Yagawanye Zaidi Aprili na Mei: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yametumainiwa na mamilioni ya wasomaji wenye kuyathamini. Ni yenye matokeo zaidi katika kutangaza Ufalme hivi kwamba twapaswa kuyabeba na kuyatoa katika kila fursa. Miezi ya Aprili na Mei na ithibitike kuwa miezi yenye kutokeza katika ugawanyaji wa magazeti!