Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/98 uku. 1
  • Roho ya Yehova Iko Nasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Roho ya Yehova Iko Nasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Kwa Jina la Roho Takatifu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Kuongozwa na Roho ya Mungu Katika Karne ya Kwanza na Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Tembea kwa Roho na Uishi Kulingana na Wakfu Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Jinsi Roho Ya Mungu Inavyoweza Kukuathiri Wewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 5/98 uku. 1

Roho ya Yehova Iko Nasi

1 Tukiwa Mashahidi wa Yehova, tuna mgawo mkubwa. Yesu alisema: “Katika mataifa yote lazima habari njema ihubiriwe kwanza.” (Mr. 13:10) Kwa maoni ya kibinadamu, mgawo huo ungeonekana mgumu, lakini sivyo ilivyo. Twategemezwa na kani yenye nguvu zaidi ulimwenguni pote—roho ya Mungu.—Mt. 19:26.

2 Uthibitisho wa Karne ya Kwanza: Akiutumia unabii wa Isaya kujihusu, Yesu alisema: “Roho ya Yehova iko juu yangu, . . . kutangaza habari njema.” (Luka 4:17, 18) Kabla ya kupaa mbinguni, aliwaambia wafuasi wake kwamba wao vilevile wangepata nguvu kutokana na roho takatifu ili kutoa ushahidi “hadi sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.” Baada ya hapo, Filipo alielekezwa na roho takatifu amhubirie yule Mwethiopia aliyekuwa ofisa wa nyumba ya mfalme, roho ilimtuma Petro kwa ofisa Mroma, nayo ilimtuma Paulo na Barnaba kuyahubiria mataifa ya Wasio Wayahudi. Ni nani ambaye angewazia kwamba watu kutoka malezi hayo wangeikubali kweli? Lakini waliikubali.—Mdo. 1:8; 8:29-38; 10:19, 20, 44-48; 13:2-4, 46-48.

3 Uthibitisho wa Siku ya Kisasa: Kitabu cha Ufunuo hukazia kuhusika kwa roho takatifu katika kazi ya kuhubiri ya leo kwa kusema hivi: “Na roho na bibi-arusi hufuliza kusema: “Njoo!” . . . Acha yeyote atakaye achukue maji ya uhai bure.” (Ufu. 22:17) Roho imechochea jamii ya bibi-arusi wa Kristo na “kondoo wengine” walio waandamani wao wahubirie watu wote habari njema. (Yn. 10:16) Twapaswa kuwa wajasiri katika kuhubiri kwetu, bila kusita kuhubiria watu wa aina zote, tukiwa na uhakika sikuzote kwamba roho ya Mungu itatusaidia. Kichapo 1998 Yearbook chaandaa uthibitisho wenye kusadikisha wa kwamba roho ya Mungu yaendelea kuwa na watumishi wake. Tazama matokeo! Katika miaka miwili ya utumishi iliyopita, wastani wa watu zaidi ya 1,000 walibatizwa kila siku.

4 Uwe na hakika ya kwamba roho ya Mungu itaendelea kuwa nasi tuhubiripo ujumbe wa Ufalme kwa kadiri anayotaka Yehova. Ujuzi huu wapaswa kututia moyo na kutuchochea tuendelee kujikakamua wenyewe katika kazi ya maana zaidi ya Ufalme.—1 Tim. 4:10.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki