Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 1/15 kur. 5-6
  • Jinsi Roho Ya Mungu Inavyoweza Kukuathiri Wewe

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Roho Ya Mungu Inavyoweza Kukuathiri Wewe
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Roho Takatifu na Kazi ya Kuhubiri
  • Ubatizo na Roho Takatifu
  • Roho Takatifu Katika Maisha Yako
  • Roho ya Mungu na Wewe
  • ‘Kwa Jina la Roho Takatifu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Tembea kwa Roho na Uishi Kulingana na Wakfu Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Kuitambua Roho Takatifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Kuongozwa na Roho ya Mungu Katika Karne ya Kwanza na Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 1/15 kur. 5-6

Jinsi Roho Ya Mungu Inavyoweza Kukuathiri Wewe

“KATIKA mwanzo Mungu aliziumba mbingu na dunia. Dunia ilikuwa bila umbo na ubure, na giza lilikuwa juu ya uso wa kilindi; na Roho ya Mungu ilikuwa ikijongea juu ya uso wa maji.” (Mwanzo 1:1, 2, Revised Standard Version) Taarifa hii ya Kimaandiko inakazia njia fulani ya kutokeza ambayo kila mmoja aliye hai amenufaika kutokana na roho takatifu. Roho hiyo ilikuwa yenye utendaji wakati wa uumbaji, na kwa utendaji wayo, dunia ilipata kuwa makao yenye upendezi kwa ainabinadamu.

Lakini watu wanaweza kunufaika zaidi sana kutokana na roho takatifu. Mithali moja yenye uongozi wa Mungu inasema hivi: “Geukeni kwa ajili ya maonyo yangu; tazama, nitawamwagia roho yangu, na kuwajulisheni maneno yangu.” (Mithali 1:23) Katika siku yetu “maneno” ya Mungu yaliyokusanywa yanapatikana katika Biblia Takatifu, iliyoandikwa na wanadamu ‘waliochukuliwa na roho takatifu.’ (2 Petro 1:21, NW; Marko 12:36; 2 Timotheo 3:16, UV) Wakati wowote mtu msikivu anapoisoma Biblia, ananufaika kutokana na roho takatifu.

Roho Takatifu na Kazi ya Kuhubiri

Wakati mmoja wa Mashahidi wa Yehova anapokutembelea nyumbani kwako kuongea juu ya habari njema za Ufalme, roho takatifu inaweza kuathiri maisha yako kwa njia nyingine. Tunajuaje? Basi, Yesu Kristo alipoanza kuzihubiri habari njema, alitumia kwake mwenyewe maneno ya nabii Isaya, akisema hivi: “Roho wa Bwana [Yehova, NW] yu juu yangu, kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema . . . kutangaza mwaka wa Bwana [Yehova, NW] uliokubaliwa.” (Luka 4:18, 19; Isaya 61:1, 2) Ndiyo, Yesu alipakwa mafuta na roho takatifu kuzihubiri habari njema.

Zaidi ya hilo, Yesu alitabiri kwamba kuhubiriwa kwa habari njema kungeendelea baada ya kifo chake. Alitoa unabii hivi: “Habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia nzima yote inayokaliwa kwa ajili ya ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakuja.” (Mathayo 24:14, NW) Muda mfupi kabla Yesu hajapaa mbinguni, aliwapa wafuasi wake utume huu: “Nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru nyinyi.” (Mathayo 28:19, 20, NW) Kwa hiyo, baada ya kupaa kwa Kristo mbinguni wanafunzi wake waliendeleza ile kazi iliyoamrishwa na roho ya kuhubiri na kufundisha. Mashahidi wa Yehova leo wanaiga wanafunzi hao wa mapema katika kuzihubiri habari njema ulimwenguni pote.

Ubatizo na Roho Takatifu

Wakati mtu anapoitikia zile habari njema kwa upendelevu, Yesu alisema anapaswa kubatizwa “katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu.” Hivyo basi wanafunzi wapya wanaathiriwa zaidi na roho takatifu. Maneno “katika jina la” kwa kweli yanamaanisha “kwa mamlaka ya” au “kwa kutambua cheo cha.”a Hivyo, kubatizwa katika jina la Baba kunamaanisha kukubali enzi kuu ya Mungu katika maisha zetu bila kuitilia shaka. Ubatizo katika jina la Mwana unamaanisha kumkubali Yesu kuwa Mkombozi, Kielelezo, na Mfalme. Na ubatizo katika jina la roho takatifu unahusisha kuitegemea roho na kunyenyekea nguvu zayo.b

Roho Takatifu Katika Maisha Yako

Kwa kuhuzunisha, ukosefu wa kufuata haki, ukosefu wa maadili, jeuri, na kutotii sheria kwa ujumla ambako tunaona katika mabara “ya Kikristo” kwaonyesha uhakika wa kwamba walio wengi wa wale wanaodai kuwa Wakristo kwa kweli wanaikinza roho takatifu. Lakini wale wanaoinyenyekea wanabarikiwa sana. Kwanza, wao wanachukua kwa uzito mambo wanayosoma katika Biblia iliyoongozwa kwa roho na kuyatumia katika maisha zao. Hivyo, wana hekima, muono-ndani, uamuzi mzuri, akili chapuchapu, maarifa, na uwezo wa kufikiri. (Mithali 1:1-4) Haya ni majaliwa yenye thamani katika nyakati zetu zenye msukosuko.

Pia roho takatifu inasaidia watu hao mmoja mmoja kushinda matatizo magumu. Katika nyakati za kale, Mungu alionyesha watu wake jinsi wangeweza kutimiza kazi fulani ngumu sana. Yehova alisema kwamba ingefanywa “si kwa uwezo [jeshi la kivita, NW], wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho [yake].” (Zekaria 4:6) Tukinyenyekea Mungu na roho yake, tutasaidiwa pia kutimiza kazi mbalimbali na kushinda vipingamizi ambavyo ama sivyo vingekuwa vikubwa mno kwetu.—Mathayo 6:33; Wafilipi 4:13.

Zaidi ya hilo, roho ya Mungu inatusaidia tuuonee shangwe uhuru usiojulikana na ulimwengu kwa ujumla. Mtume Paulo aliandika hivi: “Mahali roho ya Yehova ipo, pana uhuru.” (2 Wakorintho 3:17, NW) Wale wanaonyenyekea roho ya Mungu wanauonea shangwe uhuru wa kutokuwa kwenye dini bandia, hofu za kishirikina, hofu juu ya wakati ujao, na mambo mengine mengi yanayotia utumwani. Kwa kweli roho ya Mungu ni nguvu ya kuleta wema! Inaweza hata kubadili watu. Biblia inagusia hilo inaposema hivi: “Tunda la roho ni upendo, shangwe, amani, ustahimilivu, fadhili, wema, imani, upole, kujidhibiti. Dhidi ya mambo hayo hakuna sheria.” (Wagalatia 5:22, 23, NW) Ulimwengu huu ungekuwa tofauti kama nini ikiwa kila mtu angenyenyekea uvutano wa roho ya Mungu!

Wakiwa kikundi, Wakristo wa kweli wanaounea shangwe pia ‘umoja wa roho katika kifungo cha amani.’ (Waefeso 4:3) Umoja na amani ni mambo haba leo. Lakini huwapo mahali ambapo roho ya Mungu inafanya utendaji. Kwa kweli, kati ya Mashahidi wa Yehova kile kifungo chenye kuunganisha cha roho takatifu kimeleta watu wa rangi zote, lugha, na mataifa yote ndani ya “ushirika wa ndugu” ulio wa kweli.—1 Petro 2:17, NW.

Roho ya Mungu na Wewe

Je! wewe unaona manufaa ya kuwa na hekima inayopewa na Mungu na ya kuuonea shangwe uhuru wa kweli? Je! haingekuwa vizuri ajabu kuwa na msaada wa kimungu katika kutatua matatizo na kusitawisha upendo, shangwe, amani, ustahimilivu, fadhili, wema, imani, upole, na kujidhibiti? Basi nyenyekea nguvu ya roho takatifu ya Mungu. Lakini mtu anawezaje kufanya hivi?

Acha Neno la Mungu, Biblia, livute akili na moyo wako. Shirikiana na wale wanaoacha roho takatifu ivute maisha zao. Chukua hatua sasa za kujifunza na kufanya mapenzi ya kimungu. Halafu, ‘Mungu ambaye hutoa tumaini na akujaze shangwe yote na amani kwa kuamini kwako, kwamba wewe upate kuwa mwingi katika tumaini kwa nguvu ya roho takatifu.’—Warumi 15:13, NW.

[Maelezo ya Chini]

a Linganisha maneno ya Kiingereza “katika jina la sheria.” Ona pia Mathayo 10:41 katika King James Version, ambapo Yesu alitumia maneno “katika jina la nabii” na “katika jina la binadamu mwadilifu.”

b Ona hotuba ya Petro kwa Wayahudi kwenye Pentekoste 33 W.K., ambapo alieleza pande nyingi za sehemu ya Yesu na roho takatifu katika maisha za waamini waliobatizwa. Baada ya hotuba yake, watu 3,000 walibatizwa katika jina la Baba, la Mwana, na la roho takatifu.—Matendo 2:14-42.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki