Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp19 Na. 1 uku. 15
  • Utanufaikaje kwa Kumjua Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Utanufaikaje kwa Kumjua Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
  • Habari Zinazolingana
  • Kaa Karibu na Yehova
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Unaweza Kufanya Nini Ili Umjue Mungu Kibinafsi?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Mungu Ndiye Rafiki Bora Uwezaye Kuwa Naye
    Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Hii Ni Njia Bora ya Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
wp19 Na. 1 uku. 15
Watu wakifurahia maisha katika Paradiso

Utanufaikaje kwa Kumjua Mungu?

Kufikia sasa, tumechunguza hatua kadhaa zinazoweza kutusaidia kumjua Mungu. Kwanza, tuliona Biblia inasema kwamba jina lake ni Yehova na upendo ndio sifa yake kuu zaidi. Pia, tuliona mambo ambayo tayari amefanya na yale atakayofanya ili kuwanufaisha wanadamu wote. Ingawa bado kuna mambo mengi ya kujifunza kumhusu Mungu, bila shaka ungependa kujua jinsi utakavyonufaika kwa kumjua vizuri zaidi.

Yehova anaahidi kwamba “ukimtafuta, atakuruhusu umpate.” (1 Mambo ya Nyakati 28:9) Ukimtafuta Mungu na kumjua, utapata zawadi yenye thamani sana—“urafiki wa karibu pamoja na Yehova”! (Zaburi 25:14) Uhusiano huo utakunufaishaje?

Utapata furaha ya kweli. Biblia inasema kwamba Yehova ni “Mungu mwenye furaha.” (1 Timotheo 1:11) Kuwa rafiki yake wa karibu na kuiga njia zake kutafanya uwe na furaha ya kweli itakayokunufaisha kihisia, kiakili, na kimwili pia. (Zaburi 33:12) Vilevile, utakuwa na maisha yenye furaha ikiwa utaepuka mazoea yasiyofaa, utasitawisha mazoea mazuri, na kudumisha uhusiano mzuri na wengine. Hatimaye, utakuwa na mtazamo kama wa mtunga zaburi aliyesema: “Kumkaribia Mungu ni jambo jema kwangu.”—Zaburi 73:28.

Mungu atakutunza na kukujali. Yehova aliwaahidi hivi watumishi wake: “Nitakupa ushauri jicho langu likikutazama.” (Zaburi 32:8) Hiyo inamaanisha kwamba Yehova anamjali kila mtumishi wake, na humtegemeza kila mmoja wao kulingana na uhitaji wake. (Zaburi 139:1, 2) Ukisitawisha uhusiano mzuri na Yehova, utatambua kwamba yeye ni mshikamanifu na hatakuacha kamwe.

Utakuwa na maisha mazuri wakati ujao. Zaidi ya kukuonyesha jinsi unavyoweza kuwa na maisha yenye furaha na yanayoridhisha sasa, Yehova Mungu anataka uwe na maisha mazuri wakati ujao. (Isaya 48:17, 18) Biblia inasema: “Uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na yule uliyemtuma, Yesu Kristo.” (Yohana 17:3) Katika siku hizi zenye misukosuko, tumaini ambalo Mungu ametupatia linaweza kuwa kama nanga inayotuwezesha kubaki tukiwa “hakika na imara.”—Waebrania 6:19.

Makala hii imetaja sababu chache tu kati ya sababu nyingi za msingi zinazotuchochea kujifunza kumhusu Mungu na kusitawisha uhusiano wa karibu na yeye. Ili kupata habari zaidi, unaweza kuzungumza na Shahidi wa Yehova au kutembelea tovuti ya jw.org.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki