Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 12/1 uku. 7
  • Hii Ni Njia Bora ya Maisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hii Ni Njia Bora ya Maisha
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Unahisi Uko Karibu na Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Kwa Nini Uendelee Kujifunza Kuhusu Habari Njema?
    Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Unaweza Kumkaribia Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu Wote)—2019
  • Uhusiano Wako na Yehova Ni Halisi Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 12/1 uku. 7
Mwanamume akisoma Biblia

HABARI KUU | UNAWEZA KUMKARIBIA MUNGU

Hii Ni Njia Bora ya Maisha

Unapaswa kufanya nini ili umkaribie Mungu? Tumechunguza hatua kadhaa unazoweza kuchukua ili uwe rafiki ya Mungu:

  1. Unahitaji kujua na kulitumia jina la Mungu, Yehova.

  2. Zungumza naye kwa ukawaida kwa kusali na kusoma Neno lake, Biblia.

  3. Endelea kufanya mambo yanayompendeza Yehova.

Mwanamume akisali

Ili umkaribie Mungu unahitaji kutumia jina lake, usali kwake, kujifunza Biblia, na kufanya mambo yanayompendeza

Kwa msingi wa mambo hayo, je, unafikiri kwamba unafanya mambo yanayohitajika ili kumkaribia Mungu? Je, unahisi kuna mambo unayohitaji kurekebisha? Kwa kweli, jitihada inahitajika, lakini utapata matokeo mazuri.

Jennifer mwanamke anayeishi Marekani anasema hivi: “Kila jitihada unayofanya ili kumkaribia Mungu ina faida. Urafiki na Mungu unaleta baraka nyingi kutia ndani: kumtumaini, kumjua vizuri zaidi, na zaidi ya yote, kumpenda. Hii ni njia bora ya maisha!”

Ikiwa ungependa kuwa na uhusiano mzuri na Mungu, Mashahidi wa Yehova watafurahia kukusaidia ufanye hivyo. Watapanga kujifunza Biblia pamoja nawe, bila malipo. Pia unakaribishwa kuhudhuria mikutano yao ya Biblia kwenye Jumba la Ufalme, ambapo utafurahia kushirikiana na watu wanaothamini uhusiano wao na Mungu.a Unapoendelea kufanya hivyo, wewe pia utahisi kama alivyohisi mtunga-zaburi aliyeimba hivi: “Lakini mimi, kumkaribia Mungu ni kwema kwangu.”—Zaburi 73:28.

a Ili kuomba ufundishwe Biblia au kujua mahali lilipo Jumba la Ufalme lililo karibu nawe, tafadhali zungumza na mtu aliyekuletea gazeti hili au tembelea Tovuti yetu, www.jw.org/sw, na utazame kichwa WASILIANA NASI.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki