Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • fg somo la 15 maswali 1-4
  • Kwa Nini Uendelee Kujifunza Kuhusu Habari Njema?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Uendelee Kujifunza Kuhusu Habari Njema?
  • Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Habari Zinazolingana
  • Unaweza Kumkaribia Mungu Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Hii Ni Njia Bora ya Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Unaweza Kumkaribia Mungu Jinsi Gani?
    Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
fg somo la 15 maswali 1-4

SOMO LA 15

Kwa Nini Uendelee Kujifunza Kuhusu Habari Njema?

1. Kuendelea kujifunza Biblia kutakunufaishaje?

Wanawake wawili wakijifunza Biblia katika muda wa mapumziko kazini

Bila shaka, mafundisho haya ya msingi ya Biblia tuliyopitia yameimarisha upendo wako kwa Yehova. Upendo huo unahitaji kuendelea kusitawishwa. (1 Petro 2:2) Ili upate uzima wa milele lazima uendelee kumkaribia Mungu kwa kusoma Neno lake.​—Soma Yohana 17:3; Yuda 21.

Kadiri unavyoendelea kupata ujuzi juu ya Mungu ndivyo imani yako itakavyokuwa na nguvu zaidi. Imani itakusaidia kumpendeza Mungu. (Waebrania 11:1, 6) Itakuchochea utubu na kufanya mabadiliko muhimu katika maisha yako.​—Soma Matendo 3:19.

2. Ujuzi wako kumhusu Mungu unaweza kuwanufaishaje wengine?

Mwanamke akisali kwa Mungu

Unaweza kuwa na uhusiano wa pekee pamoja na Yehova

Bila shaka una hamu ya kuwaambia wengine mambo ambayo umejifunza—sisi sote hufurahia kuwaambia wengine habari njema. Kadiri unavyoendelea kusoma Biblia, utajifunza jinsi ya kuitumia kuwahubiria wengine kuhusu Yehova na habari njema.​—Soma Waroma 10:13-15.

Watu wengi huanza kwa kuwahubiria habari njema marafiki au watu wa ukoo. Uwe mwenye busara. Badala ya kuwaambia kwamba dini yao si ya kweli, waambie kuhusu ahadi za Mungu. Pia, kumbuka kwamba kwa kawaida watu watavutiwa na mwenendo wako mzuri kuliko hata yale unayosema.​—Soma 2 Timotheo 2:24, 25.

3. Unaweza kufurahia uhusiano gani na Mungu?

Kujifunza Neno la Mungu kunaweza kukusaidia kukua kiroho. Hatimaye, unaweza kuwa na uhusiano wa pekee sana na Yehova. Kwa kweli, unaweza kuwa mali yake ukiwa sehemu ya familia yake.​—Soma 2 Wakorintho 6:18.

4. Unaweza kufanya maendeleo ya kiroho jinsi gani?

Unaweza kufanya maendeleo ya kiroho kwa kuendelea kujifunza Neno la Mungu. (Waebrania 5:13, 14) Unaweza kumwomba Shahidi wa Yehova ajifunze Biblia pamoja nawe kwa kutumia kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Kadiri unavyoendelea kujifunza kutoka katika Neno la Mungu, ndivyo utakavyozidi kufanikiwa katika maisha.​—Soma Zaburi 1:1-3; 73:27, 28.

Mashahidi wa Yehova wakianzisha funzo la Biblia

Habari njema inatoka kwa Yehova, Mungu mwenye furaha. Unaweza kumkaribia kwa kushirikiana na watu wake. (Waebrania 10:24, 25) Unapoendelea kujikakamua kumpendeza Yehova, unajitahidi kuupata uzima ulio wa kweli, yaani, uzima wa milele. Kumkaribia Mungu ndilo jambo bora zaidi unaloweza kufanya.​—Soma 1 Timotheo 1:11; 6:19.

Unaweza kupata habari zaidi katika sura ya 18 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki