Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 12/1 uku. 3
  • Je, Unahisi Uko Karibu na Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Unahisi Uko Karibu na Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • INAWEZEKANA KUMKARIBIA MUNGU
  • Hii Ni Njia Bora ya Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Je, Kweli Unaweza ‘Kumkaribia Mungu’?
    Mkaribie Yehova
  • Je, Unawasiliana na Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Mungu Ndiye Rafiki Bora Uwezaye Kuwa Naye
    Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 12/1 uku. 3
Mtu anayetafakari kumhusu Mungu

HABARI KUU | UNAWEZA KUMKARIBIA MUNGU

Je, Unahisi Mungu Yuko Karibu na Wewe?

“Kuwa na uhusiano mzuri na Mungu kunakufanya uhisi usalama, utulivu, na amani. Unahisi kwamba Mungu anakutakia mema siku zote.”—CHRISTOPHER, MWANAMUME KIJANA NCHINI GHANA.

“Mungu hukuona unapoteseka, naye anakupenda kuliko unavyoweza kuwazia.” —HANNAH, MSICHANA MWENYE UMRI WA MIAKA 13, ALASKA, MAREKANI.

“Inafariji na kufurahisha sana kutambua kwamba una uhusiano mzuri na Mungu!”—GINA, MWANAMKE KUTOKA JAMAIKA MWENYE UMRI WA MIAKA 40 HIVI.

Watu wengi huhisi kama Christopher, Hannah, na Gina. Wanaamini kwamba Mungu ni rafiki yao. Vipi wewe? Je, unahisi kwamba uko karibu na Mungu? Au, je, unataka kumkaribia au kuboresha uhusiano wako na Mungu? Huenda ukajiuliza hivi: ‘Inawezekanaje mwanadamu awe na uhusiano mzuri na Mungu Mweza-Yote? Ikiwa inawezekana, jinsi gani?’

INAWEZEKANA KUMKARIBIA MUNGU

Biblia inasema kwamba inawezekana kuwa na uhusiano mzuri na Mungu. Pia inasema kwamba Mungu alimwita Abrahamu, aliyekuwa Mwebrania ‘rafiki yake.’ (Isaya 41:8) Pia kumbuka mwaliko unaotolewa kwenye andiko la Yakobo 4:8: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.” Kwa hiyo, ni wazi kwamba inawezekana kuwa na uhusiano mzuri au urafiki na Mungu. Lakini kwa sababu hatuwezi kumwona Mungu, inawezekanaje ‘kumkaribia’ na kuwa na uhusiano mzuri pamoja naye?

Ili kupata jibu la swali hilo, fikiria jinsi urafiki kati ya wanadamu unavyositawishwa. Kwa kawaida, watu hujuana majina na kisha kuanzisha urafiki. Halafu, kadiri wanavyoendelea kuwasiliana ndivyo urafiki wao unavyositawi. Urafiki wao huzidi kuimarika wanapoendelea kutendeana mambo mema. Ndivyo ilivyo pia tunapotaka kuwa na uhusiano mzuri na Mungu. Acheni tuchunguze jinsi ya kufanya hivyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki